Nyie wana JF endelezeni kwenu na sio kujichimbia Ulaya na Dar tu kwi kwi kwi!!!!
Waziri Mkuu ashawishi wazawa wa Rukwa kuwekeza kwao
Na Peter Edson
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amewataka wakazi wa mkoa wa Rukwa waishio katika jiji la Dar es Salaam na mikoa mingine kurudi katika mkoa wao na kuwekeza miradi mbalimbali ya kimaendeleo.
Akizungumza na wakazi wa mkoa huo wanaoishi Dar es Salaam katika mkutano wa kujadili mpango mkakati unaoweza kutatua kero zinazoukabili mkoa huo, Pinda alisema ili kuleta mabadiliko ya kiuchumi, wazawa wa Rukwa hawana budi kurudi katika mkoa kuwekeza.
揝ina maana ya ninyi kurudi kule na kuacha shughuli zenu hapa ila nasema sisi tunaokaa mbali na mkoa wetu, hatuna budi kurudi nyumbani kuwekeza miradi ya maendeleo kwa lengo la kuufanya mkoa wetu uwe na hadhi,攁lisema Pinda.
Alisema wazaliwa wa mkoa wa Rukwa, wana uwezo mkubwa wa kushughulikia matatizo ya mkoa huo ilimradi waongeze umoja na mshikamano.
揗koa wa Rukwa uko nyuma kimaendeleo, wawekezaji wengi wanashindwa kuwekeza kwa sababu za kijiografia na kuwepo kwa miundombinu mibovu. Ili kuwavutia, tunatakiwa kuwa mfano, turudi kuwekeza kwetu,攁lisema Pinda
Alisema pamoja na kuchelewa kwa maendeleo katika mkoa huo, jitihada za makusudi zinatakiwa kuchukuliwa kuanzia sasa ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu na kuipa elimu kipaombele.
Mbunge wa Kwela Crisant Mzindakaya aliwaeleza wazawa wa mkoa huo kuwa wakifanya mchezo wageni watauvamia na kuwekeza miradi yao.
揘yumbani ni nyumbani tu, ni vema tukarudi na kufanya maendeleo kwetu, siku zinazokuja tutashindwa kupata ardhi kabisa kwa kuwa wenzetu wamegundua vivutio na fursa zilizopo wanazichangamkia kwelikweli," alisema.