Emmanuel Martin ni Douglas Costa wa Afrika.

demigod

JF-Expert Member
Jan 2, 2015
8,250
15,116
Najua mnajua kuwa kila mtu anamjua Douglas Costa de Souza ni nani? Kama humjui basi unashauriwa usimalizie kusoma huu uzi, ufungue YouTube ukiwa unatafuta video za huyu Kijana.

Leo nimeamua kumzungumzia Emmanuel Martin. Uwezo wa huyu kijana ulinipa shaka sana katika kuamini kama ni mchezaji wa kuhimidiwa.

Nikajipa zoezi la kumfuatilia huyu Kijana kwenye hizi mechi 2 alizocheza mpaka sasa. Si tu kwenye mechi, bali pia nilipata nafasi ya kupitia Mazoezi (Uhuru) nilipokuwa natoka kazini. Hakika Ubora wa huyu Kijana hauna tofauti na winga matata wa kibrazil anaye tafuta Ugali wake pale katika klabu ya Bavarians. (Bayern Munchen).

Douglas Costa (Pacha wake na Emmanuel Martin)
87a145baa740ffad4f99e0f8d37004b3.jpg


Uwezo wake wa
1.kupunguza adui katika mazingira magumu, 2.Kumiliki mpira mguuni pale akosapo nafasi ya kutoa pasi,
3.Kukokota Mpira kuelekea lango la Adui,
4.Uwezo wa kutoa pasi ndefu zenye macho.

Umenifanya bila shaka kuamini kuwa Huyu kijana Emmanuel Martin ni hazina ya Taifa. Ukizingatiza timu ya Taifa yaniTaifa Stars imekuwa ikikosa mshambulizi wa kushoto ambaye mwenye kuweza kuleta sekeseke langoni mwa mpinzani

"Emmanuel Martin katika picha dhidi ya NDANDA FC" jezi namba 18.

0126caafd4a0d8a2f7c66608fec82d24.jpg
07bc346ac669b9d8c9453b5fa5edf5f3.jpg
734b299c7f9a68337f6d3cec5ab857fd.jpg
 
Hili ndicho kilichotokea kwa mmoja wa shabiki wa Mikia FC baada ya kuona performance ya Emmanuel Martin zikiwa zimebaki mechi kadhaa kabla Emmanuel Martin hajakutana Uso-Kwa-Uso na Bokungu.

16a2d2d97216da6ee9b51640d23fbaec.jpg
 
Kijana yupo vizuri sana.
Lwandamina alimwona mara moja akajua ni kifaa cha ukweli
Kaseke asahau nafasi imekwenda hiyo.
Ni kweli aisee! Yaani tofauti na Kaseke. Dogo akiwa na mpira Mguuni ni kama Adrew Pirlow.... Huwezi kumpoka kirahisi mpaka umechezee rafu..
 
Huyo kijana wako ni noma sanaaaa!! Ni zaidi ya Messi and Ronald put together!!!!!! Haijawahi kutokea huku duniani kama yeye!!!
 
Pa
Huyo kijana wako ni noma sanaaaa!! Ni zaidi ya Messi and Ronald put together!!!!!! Haijawahi kutokea huku duniani kama yeye!!!
Pamoja na hayo kijana anajua si utani. Akiendelea hivi bila kubweteka TP mazembe inamhusu.
 
Pa
Huyo kijana wako ni noma sanaaaa!! Ni zaidi ya Messi and Ronald put together!!!!!! Haijawahi kutokea huku duniani kama yeye!!!
Pamoja na hayo kijana anajua si utani. Akiendelea hivi bila kubweteka TP mazembe inamhusu.
 
Pa

Pamoja na hayo kijana anajua si utani. Akiendelea hivi bila kubweteka TP mazembe inamhusu.
Ingekuwa vema ungewaza dogo anaweza kwenda kucheza soka ulaya kwenye team ndogo za huko kuliko kufikiria kila mchezaji wa bongo apite alipopita Samata. anyway tunamuombea dogo afike mbali
 
Pa

Pamoja na hayo kijana anajua si utani. Akiendelea hivi bila kubweteka TP mazembe inamhusu.
Mkuu kwa hadhi ya Klabu kama Yanga SC hivi sasa. Sioni wachezaji wakikimbilia pale TP MAZEMBE.

La sivyo hivyo vilabu viwe vinamwaga mpunga wa kutosha sana kuwashawishi wachezaji wa Yanga SC kuondoka.

Ona watu kama Al Ahly walivyo lilia saini ya Ngoma...... Kwenye dau la usajili ndipo likakwamia.

Labda waende simba pale. Wao kuuza wachezaji nje ndio mafanikio. Masuala ya Kubeba ndoo ndio mafanikio yetu sisi Yanga SC.
 
Mkuu kwa hadhi ya Klabu kama Yanga SC hivi sasa. Sioni wachezaji wakikimbilia pale TP MAZEMBE.

La sivyo hivyo vilabu viwe vinamwaga mpunga wa kutosha sana kuwashawishi wachezaji wa Yanga SC kuondoka.

Ona watu kama Al Ahly walivyo lilia saini ya Ngoma...... Kwenye dau la usajili ndipo likakwamia.

Labda waende simba pale. Wao kuuza wachezaji nje ndio mafanikio. Masuala ya Kubeba ndoo ndio mafanikio yetu sisi Yanga SC.
Yanga siyo kama TP Mazembe, yanga wana uwanja wao, wana ndege yao!! Halafu Mazembe wachezaji wao mishahara inachelewa hadi wagome kufanya mazoezi!! Ama kweli yanga ni noma!!!!!!
 
Dogo yupo vizuri.
Tatizo hawezi kupata mafanikio kwakuwa yupo Yanga.
Mchezaji aliyepitia Yanga na kutupiwa virago na akapambana kivyake ni Nonda Shabani tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom