Elimu yetu na jeneza lake

Elimu yetu na jeneza lake

Joined
Aug 20, 2016
Posts
24
Reaction score
15
Kwa sasa naomba nikiri kuwa ELIMU yetu iko ICU inaelekea kwenye jeneza ama kaburi ifukiwe NA kupotea kabisa. Kuna mambo tutabishana lakini kwa hili naomba mnielewe.

Nilikuwa najaribu kuongeza ELIMU ya computer out na kwa bahati tunapata wasaa wakufundishwa na walimu wa out. Kuna mkurugenzi hapa out hajui hesabu za form four.

Kidogo niko vizuri kwenye hesabu. Huyu mkurugenzi ana PhD na anawaingiza chaka wanafunzi mbaya kabisa. Sasa najiuliza hao wanafunzi wa secondary inakuwaje?

Kama tujuavyo wanafunzi wanaofeli ndio wanaokimbilia nafasi za ualimu na tuna miaka zaidi ya 30 tunachukua wanafunzi wanaofeli na kuwafanya walimu. Kwa maana hiyo tuna walimu wengi sana waliofeli, na si ajabu ukakuta kuna shule ina walimu wote waliopita kwa division four mbaya kabisa.

Sasa najiuliza kama bado tunapigana na walimu kufaulisha wanafunzi na tunaacha kupigana NA kuondoa walimu vilaza mashuleni basi kwa sasa tuko ICU na hiki kizazi kitakapo mpata mwendawazimu atakitumbukiza kaburini mazima.

Inawezekana tunaiangalia elimu kwa jicho la kawaida. Wandugu mnaofanya maamuzi upande wa elimu na serikalini kwa ujumla.

Chonde chonde tafakarini upya jinsi ya kuinusuru ELIMU yeti
 
Kama tujuavyo wanafunzi wanaofeli ndio wanaokimbilia nafasi za ualimu na tuna miaka zaidi ya 30 tunachukua wanafunzi wanaofeli na kuwafanya walimu. Kwa maana hiyo tuna walimu wengi sana waliofeli, na si ajabu ukakuta kuna shule ina walimu wote waliopita kwa division four mbaya kabisa.
Kwa F4 sasa unatakiwa uwe na Div 1-3 kwenda teaching. Ukija wa BA, BSc na BED-inategemea chuo kwa mfano UDSM,DUCE na MUCE kama huna ufaulu mzuri chances ni kubwa hutapata. Hawa nimeona performance ya selected students kwa miaka kama 3 iliyopita-hivyo si kweli tena kwa zama hizi, ingawa sina data ya vyuo vingine vinachukua wakina nani.
 
mie naona tusihangaike na walimu wa juu…

huku chini watu wafundishwe independent learning,

culture ya kukariri ibadilishwe taratiibu,kwa kufundisha vidudu na primary kujisomea vitabu…

mtoto akiwa anasoma vitabu,knowledge yake inaongezeka kila anavyokua,

akifika form six ni mtu anauejielewa haswaa…

akienda chuo anakua expert!

na hata asipoenda chou,still ana knowledge ya kutosha..
 
Kwa F4 sasa unatakiwa uwe na Div 1-3 kwenda teaching. Ukija wa BA, BSc na BED-inategemea chuo kwa mfano UDSM,DUCE na MUCE kama huna ufaulu mzuri chances ni kubwa hutapata. Hawa nimeona performance ya selected students kwa miaka kama 3 iliyopita-hivyo si kweli tena kwa zama hizi, ingawa sina data ya vyuo vingine vinachukua wakina nani.
Inapendeza kama tumebadilika. Ndama secondary iko wilayani sehemu nzuri ambayo kila mwalimu angependa kufundisha. Ina miaka 14 hakuna mwanafunzi ameshawahi pata japo B tu ya hesabu kweli hapa unaniambia tuna walimu kweli?
 
Kwa F4 sasa unatakiwa uwe na Div 1-3 kwenda teaching. Ukija wa BA, BSc na BED-inategemea chuo kwa mfano UDSM,DUCE na MUCE kama huna ufaulu mzuri chances ni kubwa hutapata. Hawa nimeona performance ya selected students kwa miaka kama 3 iliyopita-hivyo si kweli tena kwa zama hizi, ingawa sina data ya vyuo vingine vinachukua wakina nani.
mie naona tusihangaike na walimu wa juu…

huku chini watu wafundishwe independent learning,

culture ya kukariri ibadilishwe taratiibu,kwa kufundisha vidudu na primary kujisomea vitabu…

mtoto akiwa anasoma vitabu,knowledge yake inaongezeka kila anavyokua,

akifika form six ni mtu anauejielewa haswaa…

akienda chuo anakua expert!

na hata asipoenda chou,still ana knowledge ya kutosha..
Rebeca uko vizuri ni wakati sasa wakuanza kuijenga misingi ya watoto mapema sana thanks
 
Inapendeza kama tumebadilika. Ndama secondary iko wilayani sehemu nzuri ambayo kila mwalimu angependa kufundisha. Ina miaka 14 hakuna mwanafunzi ameshawahi pata japo B tu ya hesabu kweli hapa unaniambia tuna walimu kweli?
Kufaulu au kutokufaulu kuna mambo mengi, na mchango wa walimu ni mkubwa sana issue ni motivation-kuna shule za mjini zina walimu wengi lakini performance ndiyo hivyo. Tumesikia ya Jangwani na hata hiyo unayo itaja. Bado tuna safari ndefu pamoja na jinsi tunavyo watayarisha hao walimu etc. Issue ya msingi ilikuwa quality ya wanaokwenda ualimu, sasa pia kuna quality ya wanaofaulu ualimu, etc.
 
Back
Top Bottom