Elimu yetu: Kuuza miili UDOM ni matokeo...

Elimu yetu: Kuuza miili UDOM ni matokeo...

My take:
Loan board ni wazembe, lunch masaa mawili. Imagine, wa kuhamishiwa mikopo toka mwezi wa tisa hadi sasa bado. Wanachuo wanaishije? Lampard mpaka basi! Ubaya mawaziri wa elimu hawajakaa kwenye huo mfumo
 
hawa dada zetu waache kujiendekeza, ufuska ni tabia ya mtu wanatakiwa pindi wapatapo mikopo itumike vizuri sio kwenda kufanya shopping za kushindana kimavazi na kununua simu kali siku mbili tatu pesa imeisha wanaaanza umalaya! Pia wapatapo likizo watafute part time job na kipato kiwasaidie walkati wanasubiria mikopo!na wazazi na ndugu wengine waangalie pia namna ya kusaidia maana hii bodi ya mikopo ipo jina tu!


part time job gani zaidi ya hiyo waliyoigundua?
 
Hizi taarifa zinahitaji kufanyiwa utafiti zaidi ili kujua ukubwa wa tatizo. Offcourse katika mkusanyiko mkubwa kama ilivyo katika vyuo vingine huwezi kukosa watu wenye tabia hizo.

Kuna kasumba ya wadada poa kujipaisha ili kuvutia wateja. Kinachofanyika ni hawa dada poa wa Dom kuwa hadaa wateja wao kuwa ni wanafunzi wa udom. Wateja wao nao bila kufanya kutafakari hujikuta wakiamini hivyo na habari kuendelea kusambaa. Wabongo kwa kuamini umbeya:

Offcourse you have a point hapo lakini wewe siku za wikiend kipindi Bunge linapokuwa na vipindi vyake, nenda CSSH ukaangalie prado zinazoingia na kutoka college hapo haswa mida ya saa kumi na moja mpaka saa mbili je hao nao ni wanafunzi ndo wanamiliki hayo ma-prado!
Pia mwaka kuna dada mmoja amehitimu pale mwaka 2010/11 huyu alikuwa anafahamika sana kwa kuwauza wenzake kwa waheshimiwa kiasi kwamba akaanza kumiliki gari aina ya nadia (japo sina uhakika kama ni hiyo kazi ndio ilimpatia), kipindi hicho kulikuwa na kada mmoja wa ccm ambaye pia alikuwa anawauza wadada saaana tu kwa wabunge! huyo alikuwa anafahamika na kila mtu aliyekuwepo UDOM kipindi hicho
 
wadau mi sasa naamini wanafunzi wa kiume wa UDOM ni vibaka, majambazi na matapeli. Wao wanawezaje kumudu maisha bila kujiuza?
 
Tatizo Halipo DOM pekee tembelea Vyuo vikuu vyote TZ na utajua ukubwa wa tatizo.

Maisha magumu yamewapeleka dada zetu hapo walipo plus kutaka urahisi kupitia migongo ya wenye nazo.

Pia tatizo la Ushoga kwa vijana wakiume nalo huchangiwa na hali hii ambayo akina dada wameangukia, huanza kama mchezo kwa kugawa 0713 na baadae huharibika kabisa na kushindwa kujinasua toka kwenye tatizo hili.
 
Ni kweli kuna tatizo la mikopo.Ama mikopo haitoshi ama inachelewa kutolewa, lakini si wote wanatumia karama hii ya biashara ya ngono. Hii ni hulka ya mtu ama upeo wake wa kufikiria biashara gani atumie kutatua matatizo haya, akaona biashara rahisi ni ngono. Si watu wote hutumia njia moja kutatua tatizo la aina ileile. Tatizo la mikopo liko vyuo vyote vya Tanzania, lakini tatizo la biashara ya ngono inasemekana kuwa kubwa UDOM. Nadhani iko haja ya kufikiri zaidi ya mikopo na Bodi ya mikopo.
Nasisitiza kuwa hii ni hulka ya mtu. Wapo watu wametumia mbinu hii kujineemesha maisha hata bila ya tatizo la mikopo. Wapo wanafunzi wamefaulu kozi zao kwa kupatiwa misaada na wakufunzi kwa mtaji huu huu, wapo waliojengewa nyumba nzuri kuliko baadhi yanyumba za watumishi, wapo waliopandishwa vyeo kwa mtaji huu huu. Kuna watu familia zao zimeyumba sababu ya biashara hii. Tusilione tatizo hili kwa juu juu. Hawa watu wazima waliofanikisha mambo ya kwa njia hii walianza wakiwa umri sawa na wa waliovyuoni sasa. Mbinu iliyomsaidia mtu kufikia mafanikio fulani hataicha maishani. Jamii corrupt huzaa watoto corrupt. Yawezekana wanafunzi wanaojiuza wanatoka katika familia ambazo ama mama anajiuza, ama amepora mume wa mtu ama mama kapata cheo kwa njia ya upendeleo ama baba anahangaika na changu doa ametelekeza familia yake. Fanyeni utafiti zaidi ya kufikiria mikopo na bodi ya mikopo.
nakubaliana na wewe hasa inapokuwa 'out of will' kwa kuchagua, ndiyo kila mmoja anatumia chake lakini kwa hawa hapana:waliamua kutumia akili lakini serikali na bodi ya mikopo zinawafanya watumie 'uchi' bila kupenda. Lazima tuichukie CCM kwavitendo na tuikatae hata kwa kura 2015.
 
kama wanafanya kwa hamu kama wewe unavyodhani mkuu sidhani kama ni tatizo kubwa kama unavyofikiri,WANAJIUZA ili wapate chochote kitu,sasa sijui mtu anaweza kujiuza kwa ajili ya erection tu.

Wataalamu wa maisha ya kiroho au wamezoeleka kwa jina la mababu wa kiroho waliangalisha karne kadhaa zilizopita kwamba "uvivu ni adui wa roho." Mwili unahitaji kutumikishwa na ukichoka unahitaji kujipumzisha.

Hawa vijana kwa kukaa darasani tu hawautumikishi mwili na maungo yake, bali ni ubongo ndio unaofanya kazi. Baada ya darasa mwili unadai haki zake. Moja ya udhaifu ambao binadamu huupata ni nguvu za uzazi kupata erection kutokana na mwili kutofanyiziwa mazoezi ya kutosha. Lakini mwili ukichoka, viungo vya uzazi havina nguvu sana kama mtu mvivu asiyeutumisha mwili wake ndiyo maana ya uvivu ni adui wa roho.

Nilipokuwa nasoma shule tulikuwa na utaratibu wa michezo shuleni na vyuoni, mpira wa miguu, riadha, muziki, nk. Baada ya mazoezi hayo kinachokuja akilini ni kumaliza haraka assignments na kwenda kulala, mwili umeshoka. Niamkapo asubuhi ni mchakamchaka wa kufa mtu kuwahi shuleni au chuoni na haitoshi baada ya line up kinachofuata ni mchakamchaka wa km kadhaa kabla ya kuingia madarasani wakati kipindi cha awali ni hesabu au kiingereza mtu unakuwa umeshachangamka. Leo ukiwaona wanafunzi na kuwaamrisha
"stand at easy! attention!", Endeleas mbele, left right left right, right turn!" utaona wanakutazama usoni na kuchekacheka.

Baada ya mapumziko ya mchana kunakuwa na gwaride ambalo marching yake inasaidia kutuweka fiti na well organized. Unaingia ungwe ya lalasalama baada ya gwaride lenye kuongozwa na
brass band. Watoto walivutika kutamani shule sababu ya vivutia hivyo, niambie nini kinaendelea?

Tulikuwa na elimu ya kujitegemea mashuleni, kulima mashamba ya kahawa, bustani ya mboga mbalimbali, mashamba ya mahindi nk. Hayo yalitusaidia kupata chakula cha mchana tulipokuwa shule ya msingi na pale upungufu unapotokea, bodi ya shule iliomba wazazi kuchangia debe moja la mahindi kwa kila familia yenye wanafunfi shuleni. Tulikuwa tunafurahia shule.

Tazama wanafunsi siku hizi shule za msingi ni tepetepe na legelege. Hakuna program za kuwasaidia kuwa wakakamavu, matokeo yake wangali wadogo wanafanya mambo ya kikibwa ambayo ni aibu hata kuyaanika hapa, ni ni wavuta bangi ile mbaya. Hao ndio wanaohitimu shule ya msingi kwa ufaulu wa karatasini lakini hawajui kusoma na kuandika. Hawa ndio wanaotegemewa kuwa wanachuo katika vyuo vyetu vikuu nchini.

Mfumo wa elimu wa kikoloni tuliouharibu ndio unaotutesa sasa. Wenzetu Kenya na Uganda waliudumisha unaona kiwango chao cha elimu hakina utata kama hapa kwetu Tanzania nakupenda kwa moyo wote.
 
Ni kweli kuna tatizo la mikopo.Ama mikopo haitoshi ama inachelewa kutolewa, lakini si wote wanatumia karama hii ya biashara ya ngono. Hii ni hulka ya mtu ama upeo wake wa kufikiria biashara gani atumie kutatua matatizo haya, akaona biashara rahisi ni ngono. Si watu wote hutumia njia moja kutatua tatizo la aina ileile. Tatizo la mikopo liko vyuo vyote vya Tanzania, lakini tatizo la biashara ya ngono inasemekana kuwa kubwa UDOM. Nadhani iko haja ya kufikiri zaidi ya mikopo na Bodi ya mikopo.
Nasisitiza kuwa hii ni hulka ya mtu. Wapo watu wametumia mbinu hii kujineemesha maisha hata bila ya tatizo la mikopo. Wapo wanafunzi wamefaulu kozi zao kwa kupatiwa misaada na wakufunzi kwa mtaji huu huu, wapo waliojengewa nyumba nzuri kuliko baadhi yanyumba za watumishi, wapo waliopandishwa vyeo kwa mtaji huu huu. Kuna watu familia zao zimeyumba sababu ya biashara hii. Tusilione tatizo hili kwa juu juu. Hawa watu wazima waliofanikisha mambo ya kwa njia hii walianza wakiwa umri sawa na wa waliovyuoni sasa. Mbinu iliyomsaidia mtu kufikia mafanikio fulani hataicha maishani. Jamii corrupt huzaa watoto corrupt. Yawezekana wanafunzi wanaojiuza wanatoka katika familia ambazo ama mama anajiuza, ama amepora mume wa mtu ama mama kapata cheo kwa njia ya upendeleo ama baba anahangaika na changu doa ametelekeza familia yake. Fanyeni utafiti zaidi ya kufikiria mikopo na bodi ya mikopo.

Jambo la kujiuliza kwa nini biashara hiyo imeshamiri zaidi Dodowa ambako wabunge na waheshimiwa mbalimbali wa serikali hukutana? Je, uwopo wao unachangia? Mara kadhaa imeelezwa magari ya waheshimiwa humimimika huko kuwachukua wanafunzi baada ya muda wa masomo na weekend. Ieleweke wote wachukuliwao ni ndugu au wengine ni kwa ajili ya kuwabinafsi waheshimiwa baada ya uchovu na kuzinzia bungeni?
 
Tatizo dada zetu Hawakosi sababu wakiwa wanalipwa mapema watasema sababu nyingine,wakati mtu anakinyima haki yako insteady ya wewe kugombania haki yako unahamua kufanya mambo ya hatari Kama prostitution nikama vile ujitia kitanzi, Kama unaweza kufanya hivyo kwanini usiandamane au ukagoma mpaka ulipwe haki yako Kwani ukimaliza chuo Itabidi elipe huo mkopo.Tatizo wanafunzi bongo Hawapo makini ya nini future Yao, ni mpaka pale kutakuwa na system ya kuwakamata wanachuo wanaofanya ukahaba na wawe kwenye record ya polisi ambayo baadaye wajiri watakuwa na access nayo nakufanya wakose kazi in future. It's shame kwani wanafunzi wa vyuo vote duniani wanaparty hard sio kujiuza.
 
Serikali yetu imeweka elimu yetu rehani,natafakari jinsi mdogo wangu alivyosoma kwa tabu utafikiri ni mkimbizi ktk hii nchi.
 
by Alex Nicholaus Thomas Mushi .

Kwa dhati ya moyo wangu nimesikitishwa sana na taarifa zilizozagaa kwenye vyombo vya habari kuhusu kujiuza kwa dada zetu wa UDOM. Wasomi ambao wana Dodoma na watanzania kwa ujumla walitegemea kujifunza kutoka kwao. Taarifa hizi zimenichochea kukaa chini na kuandika waraka huu huku nikizingatia ukweli kwamba UDOM ndipo nilikosomea masomo yangu ya shahada ya kwanza; mbali na matatizo yote yaliyonikumba katika safari hiyo ya kukamilisha shahada hiyo lakini nalazimika kusema kitu kwa faida yetu wote.

Ikumbukwa moja ya mategemeo ya jamii ya wana Dodoma kutoka kwenye chuo cha UDOM kilipo anzishwa mwaka 2007 ilikuwa ni kujionea jamii staarabu iliyoelimika na yenye kila sifa ya kuigwa, na pia jamii ya Dodoma ilitegemea watoto wao wangejionea namna wasomi hawa wanavyoishi kwa kusadifu kwa vitendo elimu, maadili na mila za nchi yao. Zaidi waliamini mambo hayo yangekuwa chachu ya kuwachochea vijana wao kuzingatia masomo ili na wao siku moja wafikie elimu hiyo ya Chuo lakini hali imekuwa tofauti kabisa. Leo jamii hii ya wana Dodoma wanashuhudia wasomi wanaoshinda mitaani wakiranda randa na nguo za kuogelea na za kulalia kana kwamba walikotoka hakuna wazazi, wanashuhudia wasomi wanaojiuza kama njugu.

Kiukweli siwezi hata siku moja kuruhusu kulea au kuipamba tabia hizo hata kama kuna sababu za msingi ambazo zinaweza zikawa zimesababisha tatizo hili kutokea. Kinachofanywa na dada zetu hawa ni kitendo ambacho kila mungwana anapaswa kukikemea kwa nguvu, na zaidi ya yote ni wajibu wetu wote kama vijana kurudia maadili yetu kama watanzania na kulaani kwa nguvu haya. Kama tutaruhusu tabia hii ikaota mizizi tutaandaa wasomi wasio waadilifu na wasio jiamini, tutandaa wasomi wenye shahada za kwenye chupi (nisamehewe kwa hiyo lugha lakini nimekosa neon linalokidhi ninachomaanisha),tutandaa wasomi walioathirika hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa, tutaandaa taifa la wavivu na wasifikiri kwa ufanisi.

Tukumbuke kuruhusu tabia hii kubobea ni kuruhusu kuporomoka kwa elimu ambayo ni msingi wa taifa lolote duniani. Na sidhani kama ni busara kuangalia umauti wa taifa letu kwa kuruhusu tabia hii kuota mizizi, kwani dhambi hiyo haitaishia chuoni tu, itaingia makazini na hapatakuwa na kazi zaidi ya uzinzi tu, baada ya hapo dhambi hii itasambaaa hadi kwa watoto na wajukuu wetu na hatimaye itakuwa ndio mfumo wetu wa maisha. Lakini mbali na yote niliyoeleza hapo juu ninayo yangu kwa serikali yangu, vijana hawa wa UDOM ni watoto wenu na wengine wameingia pale wakiwa hawana hata elimu ya kimaisha au ya kujitegemea, wengine wanakutana na kila aina ya tabia pale.

Mimi nilisha kuwa kiongozi wa mikopo UDOM-HSS kwa karibu miaka yote ya masomo yangu ya shahada ya kwanza, naelewa kiasi sababu na wakati dada zetu hawa wanapojiuza. Kipindi ambacho dada zetu hawa hujiuza huwa ni pale Bodi ya mikopo inapochelewesha mikopo ya wanafunzi, hali huwa mbaya kiasi dada zetu hawa ufika mahali wanalazimika kujidhalilisha ilimradi wapate chochote cha kujikimu. Na ukizingatia majumbani kwao hawa msaada wowote wanaoupata.

Mfano mzuri wa ucheleweshaji wa mikopo kwa wanafunzi wa kozi ya Uhusiano wa Kimataifa (BA IR) hawajapewa mikopo yao mpaka leo, na wanatakiwa kula, kunywa, kuwasiliana na kununua vitini vya masomo ili hali familia walizotoka ni masikini wa kutupwa. Haya yote ni mazingira hatarishi kwa dada zetu hawa. Serikali kama mzazi nakuomba mliangalie kwa umakini sana suala hili ili tuwaepushie wale wanajihusisha na tabia hii ya kuuza miili yao kutokana na kuishiwa au kukosa fedha za kujikimu Muda mwingine unaweza kusema serikali inafanya makusudi kuwacheleweshea mikopo yao wa sababu wanaonufaika sana na tabia hiyo ya dada zetu kujiuza ni wabunge wanapokuja kwenye vikao vyao vya bunge.

Kujiuza kwa dada zetu hawa ni dhahiri ni matokeo ya mambo kadhaa ambayo serikali haina budi kuyafuatilia kwa kina na hatimaye kutatua kwa ustawi wa tafa letu la Tanzania. Hatupaswi kufurahia tabia hii hata kidogo kwan kufanya hivyo kunaweza liathiri taifa letu kwa ujumla wake siku za usoni.

……………“ukiona panafuka moshi ujue kuna moto”…………

Na wavulana wakicheleweshewa mikopo wanajikimu vipi?
 
Hili ni Tatizo kwa vyuo vyote...Tulianza na Mabibo Hostel (UDSM) sasa UDOM lakini pia uliza SUA na Mzumbe nao wanajikongoja...watoto wetu wanapenda vitu vya bei kali na pesa hawana na hapo wanaingia ktk tatizo la ufusika na hasa Mikopo inapochelewa
 
bodi ya mikopo ifanye wajibu wake kwa muda. kama mtu atajiingiza kwenye hayo madudu na iwe kwaujinga wake mwenyewe. wengine hata hivo wamejaa tamaa na kuiga. ushauri utawafaa sana hao vijana
 
by Alex Nicholaus Thomas Mushi .

Kwa dhati ya moyo wangu nimesikitishwa sana na taarifa zilizozagaa kwenye vyombo vya habari kuhusu kujiuza kwa dada zetu wa UDOM. Wasomi ambao wana Dodoma na watanzania kwa ujumla walitegemea kujifunza kutoka kwao. Taarifa hizi zimenichochea kukaa chini na kuandika waraka huu huku nikizingatia ukweli kwamba UDOM ndipo nilikosomea masomo yangu ya shahada ya kwanza; mbali na matatizo yote yaliyonikumba katika safari hiyo ya kukamilisha shahada hiyo lakini nalazimika kusema kitu kwa faida yetu wote.

Ikumbukwa moja ya mategemeo ya jamii ya wana Dodoma kutoka kwenye chuo cha UDOM kilipo anzishwa mwaka 2007 ilikuwa ni kujionea jamii staarabu iliyoelimika na yenye kila sifa ya kuigwa, na pia jamii ya Dodoma ilitegemea watoto wao wangejionea namna wasomi hawa wanavyoishi kwa kusadifu kwa vitendo elimu, maadili na mila za nchi yao. Zaidi waliamini mambo hayo yangekuwa chachu ya kuwachochea vijana wao kuzingatia masomo ili na wao siku moja wafikie elimu hiyo ya Chuo lakini hali imekuwa tofauti kabisa. Leo jamii hii ya wana Dodoma wanashuhudia wasomi wanaoshinda mitaani wakiranda randa na nguo za kuogelea na za kulalia kana kwamba walikotoka hakuna wazazi, wanashuhudia wasomi wanaojiuza kama njugu.

Kiukweli siwezi hata siku moja kuruhusu kulea au kuipamba tabia hizo hata kama kuna sababu za msingi ambazo zinaweza zikawa zimesababisha tatizo hili kutokea. Kinachofanywa na dada zetu hawa ni kitendo ambacho kila mungwana anapaswa kukikemea kwa nguvu, na zaidi ya yote ni wajibu wetu wote kama vijana kurudia maadili yetu kama watanzania na kulaani kwa nguvu haya. Kama tutaruhusu tabia hii ikaota mizizi tutaandaa wasomi wasio waadilifu na wasio jiamini, tutandaa wasomi wenye shahada za kwenye chupi (nisamehewe kwa hiyo lugha lakini nimekosa neon linalokidhi ninachomaanisha),tutandaa wasomi walioathirika hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa, tutaandaa taifa la wavivu na wasifikiri kwa ufanisi.

Tukumbuke kuruhusu tabia hii kubobea ni kuruhusu kuporomoka kwa elimu ambayo ni msingi wa taifa lolote duniani. Na sidhani kama ni busara kuangalia umauti wa taifa letu kwa kuruhusu tabia hii kuota mizizi, kwani dhambi hiyo haitaishia chuoni tu, itaingia makazini na hapatakuwa na kazi zaidi ya uzinzi tu, baada ya hapo dhambi hii itasambaaa hadi kwa watoto na wajukuu wetu na hatimaye itakuwa ndio mfumo wetu wa maisha. Lakini mbali na yote niliyoeleza hapo juu ninayo yangu kwa serikali yangu, vijana hawa wa UDOM ni watoto wenu na wengine wameingia pale wakiwa hawana hata elimu ya kimaisha au ya kujitegemea, wengine wanakutana na kila aina ya tabia pale.

Mimi nilisha kuwa kiongozi wa mikopo UDOM-HSS kwa karibu miaka yote ya masomo yangu ya shahada ya kwanza, naelewa kiasi sababu na wakati dada zetu hawa wanapojiuza. Kipindi ambacho dada zetu hawa hujiuza huwa ni pale Bodi ya mikopo inapochelewesha mikopo ya wanafunzi, hali huwa mbaya kiasi dada zetu hawa ufika mahali wanalazimika kujidhalilisha ilimradi wapate chochote cha kujikimu. Na ukizingatia majumbani kwao hawa msaada wowote wanaoupata.

Mfano mzuri wa ucheleweshaji wa mikopo kwa wanafunzi wa kozi ya Uhusiano wa Kimataifa (BA IR) hawajapewa mikopo yao mpaka leo, na wanatakiwa kula, kunywa, kuwasiliana na kununua vitini vya masomo ili hali familia walizotoka ni masikini wa kutupwa. Haya yote ni mazingira hatarishi kwa dada zetu hawa. Serikali kama mzazi nakuomba mliangalie kwa umakini sana suala hili ili tuwaepushie wale wanajihusisha na tabia hii ya kuuza miili yao kutokana na kuishiwa au kukosa fedha za kujikimu Muda mwingine unaweza kusema serikali inafanya makusudi kuwacheleweshea mikopo yao wa sababu wanaonufaika sana na tabia hiyo ya dada zetu kujiuza ni wabunge wanapokuja kwenye vikao vyao vya bunge.

Kujiuza kwa dada zetu hawa ni dhahiri ni matokeo ya mambo kadhaa ambayo serikali haina budi kuyafuatilia kwa kina na hatimaye kutatua kwa ustawi wa tafa letu la Tanzania. Hatupaswi kufurahia tabia hii hata kidogo kwan kufanya hivyo kunaweza liathiri taifa letu kwa ujumla wake siku za usoni.

……………“ukiona panafuka moshi ujue kuna moto”…………

Mada ni nzuri ila haina utafiti wa kutosha juu ya kuuza miili kama ni Udom peke yao au hata vyuo vingine. Na kwa sababu hizo mi sioni kama ni fair kuwatupia lawama bodi ya mikopo au wanachuo wa Udom. Nahisi vyuo vyote kuna watu wanaopenda ngono na namna ya kufanya wanaona kwa upande wa 'wa kike' ni kupata vyote kwa pamoja starehe na uchumi bila kujali kama wameishiwa au la! Lakini pia tuangalie jamii yetu tusije tukadhani ni hao tu, maana karibu kila mji siku hizi una 'Ohio' yake na zinaongezeka toka Ohio hadi Hananasifu achilia mbali maeneo ya uwanja wa fisi n.k Ukifika Mwanza utasikia habari za mtaa wa makoroboi na hata miji midogo midogo kama Kgm fika Zanzibar Logde usiku hakuna tofauti na Ohio ya Dar taabu ni kukosa kwa Moven Peak jirani kama ilivyo Dar. Kwa hiyo mjadala mkubwa kimantiki kwangu ungekuwa ni kwanini kizazi chetu kinashabikia 'ngono' sana kana kwamba hakuna starehe nyingine? Halafu hata kama si uchumi, kwani neno Buzi lilitokana na wanavyuo? Mi naona kuna misconception hapa kwa kuwa upande wa 'ke' pamoja na wao kupenda starehe hiyo wameona ni starehe ambayo 'me' lazima waigharimie na hivyo inafanya wakimbizane kuchuna. Tembelea ma-bar mengi na kumbi nyingi za music wanaolipwa pesa au kuruhusiwa kuingia bure ni 'ke' kwa kuwa wanapaswa kulipiwa na 'me' katika starehe iendanayo na 'ngono'! Hapa naona ndo kisa na mkasa katika mambo haya. Kwa hivyo ndugu zanguni si Udom wala vyuo tu ni tabia yetu tunapenda ngono ila tunataka wakiume waigharimie hata kama sisi tunahitaji kupendwa kuliko kutumiwa kama vyombo vya starehe kwa akina 'me'. Ni mawazo yangu!!!!!
 
Kuna Mh. Mmoja alikuwa na tabia hiyo ya kuja kuchukua wadada pale Mabibo 2006-2007 kabla hajaoa..ni dhahiri ufuska na umalaya wa viongozi hasa wabunge, mawaziri, wakurugenzi na makada wa CCM wengi wakiwa wafanyabiashara (wakwepa Kodi kama yule wa Mwanza CGM) nd wanaharibu wadada wetu. Tamaa nazo zinawatawala hawa wadada. Swali la kujiuliza: je, ni wote wanajiuza? Nakubaliana na mchangiaji aliyesema tabia hii inamzizi fulani si haba. Tatizo wanafunzi wa leo kujifanya hawajui shida alhali wengi familia zao shida ni utamaduni. Wakifika University wanashoboka na maisha..Ukimwi zawadi kwao. Hayo ni ya UDOM,, je, ISW (wanajiuza Posta, Ambiance-Africa Sana etc pamoja na wadada wa UDSM), IFM na CBE ndo usiombe!! Ni tamaa tu na ulimbukeni wa kutaka maisha ya ghafla yenye raha alhali tutokako shida ni sisi na sisi ndiyo shida. Ni tabia tu na inaweza kuepukwa,,, BOOM kisingiziooo. Mbona kuna Malaya wenye fesha nyingi ambao kwao wanahitaji Sexual satisfaction na si pesa!! Wadada waache ulimbukeni (MY TAKE).
 
Mwenye e mail ya lukuvi aweke hapa ili aeleze kama haya yalioelezwa yapo kwenye mafanikio ya serikali ya awamu ya nne kama alivyokuwa anabwabwaja itv asubuhi.
 
Kila binadamu anatumia kiungo kimojawapo cha mwili wake ili kujipatia kipato chake ili aweze kuishi. Wapo wanaotumia akili zao kuuza katika soko na kujiapatia mahitaji yao.

Mfano wahasibu, wahandisi, wanasheria,madaktari orodha ni ndefu. Akili ni kiungo cha mwili kama kiungo kingine chochote. Waliojaliwa akili hawakujaliwa ukahaba. Lakini wapo waliojaliwa vipawa zaidi ya kimoja kama vile wenye jinsia mbili, huamua kutumia kimojawapo. Wapo wanaotumia miguu kucheza mpira au kukimbia au hata kuruka.

Hawa nao wanajipatia ujira utokanao na matumizi ya viungo vya miili yao kama atumiavyo kahaba kiungo chake. Wapo pia wanaotumia sauti zao kuimba na kuburudisha jamii kwa ujira wa kuuza kazi zao za sauti zao. Wapo wapiga mieleka, ngumi nk. Wote hawa tunasema wanatumia vipawa vyao kujiendeleza kwa faida yao.

Katika uchumi wa kiliberali chochote kinauzika na kunulika.Hawa dada zetu makahaba wanatumia viungo vya miili yao kama wanavyotumia watu wengine kuuza na kujipatia ujira. Katika soko kuna kuuza vitu (products)na huduma(service) Huduma ni kama benki, bima, hoteli ngono nk.

Uhuru tulipata mwaka 1961, wacha watu wawe huru kufanya walitakalo maadamu hawavunji sheria. Tabia ya mtu hutembea nayo popote anapoenda. Kama mtu ana tabia ya ukahaba (mjasiriamali wa ukahaba) hawezi kuiacha kwa sababu tu anasoma Chuo kikuu. Ni kama mtu mwingine yeyote anayeweza kuzungukwa na rasilimali nyingi lakini anashindwa kuzibadilisha kuwa vitega uchumi.

An Enterprenuer is the one who sees the opportunity that others don't see

Asungwilemwaifunga; uko sahihi kwa mtazamo wako. Tena umefanya analysis nzuri sana. Ila umesahau kuangalia kama sheria za nchi yetu ukahaba unanafasi gani! Pia kuna taratibu za jamii ambazo sio lazima ziwe katika sheria mara nyingi huwa zinaongozwa na mila na desturi za jamii, ukahaba katika jamii yetu unapewa nafasi gani!. Haya na mengine kama haya ungeyajadili huenda yangesaidia ku-shape discussion yako.
 
Back
Top Bottom