kindikwili
JF-Expert Member
- Oct 5, 2016
- 1,862
- 2,871
Amani iwe kwenu!
Kwa mfumo wetu wa sasa wa elimu mwanafunzi anaanza darasa la kwanza akiwa na miaka 7, anasoma elimu ya msingi kwa miaka 7, akifaulu anaenda sekondari kwa miaka 4, akifaulu anasoma sekondari ya juu miaka 2 na akifaulu anaenda chuo miaka 3 (au zaidi kwa baadhi ya fani). Kwa mtindo huu mtu anamaliza chuo akiwa na miaka isiyopungua 23 yaani 7+7+4+2+3. Umri huu ni mkubwa sana na ingefaa mtu huyu awe tayari anajitegemea kama mfumo wa elimu mbadala ungetumika.
Mimi napendekeza mfumo wa elimu ungekuwa hivi, mwanafunzi aanze shule akiwa na miaka 6 (hii inawezekana maana imeshazoeleka hasa mijini) sasa iwe ni sera ya nchi bila kujali jinsi ya mtoto. Halafu elimu ya msingi iwe miaka 6 tu hapa itabidi darasa la sita lasasa livunjwe masomo yanayofundishwa darasa la tano, sita na saba yaanzie darasa la nne, tano na kufika mwaka wa sita yawe yamefundishwa yote.
Wanafunzi wanafaulu elimu ya msingi kwa walau wastani Wa C waende sekondari ambako watasoma kwa miaka 3 (kama QT wanasoma elimu ya sekondary katika mazingira ya nyumbani kwa miaka 2 na wanafaulu basi wanafunzi wa shule wanaweza kufaulu vizuri tu wakisoma sekondary kwa miaka 3 tena bila shida).
Wanafunzi wanaofeli darasa la saba yaani waliopata chini ya daraja la C wapewe nafasi ya kukariri shule (ukweli wa mambo ni kwamba viongozi wetu wengi na watunga sera wetu wa sasa wengi wao walirudia shule hadi mara 4 ndiyo wakafaulu, sasa kwanini waone ni nongwa kwa mwanafunzi wa sasa kurudia shule?). Kurudia shule kwa mwanafunzi anayetaka ikubalike kisera kabisa tena bila usumbufu kwa jina lake lile lile, ila wale ambao hawataki kurudia wapelekwe VETA.
Sera ya elimu ya VETA iwe huria kwa mwanafunzi au mtu yeyote anayetaka kujifunza elimu ya ufundi bila kujali umri ilimradi huyo mtu kahitimu elimu ya msingi na anataka kujiunga kwa hiari yake. KWA WANAOFELI DARASA LA SABA IWE NI LAZIMA KWENDA VETA KAMA HATATAKA KURUDIA SHULE. Hii itazuia kuolewa kwa umri mdogo na kupunguza raia wasio na ujuzi na kazi kwa siku za baadaye
Wanaofaulu elimu ya form four kwa daraja la kwanza na la pili wapelekwe form five na six kwa miaka 2, watakaopta daraja la tatu wapelekwe vyuo vya kati (cerificates baadaye diploma) pamoja na VETA kwa anayechagua lakini kwa wenye division 4 na zero wapewe nafasi ya kwenda VETA au kurudia kama private candidates kama ilivyo kwa sasa. Kwa vile elimu ya ufundi ni ya vitendo basi hata mwenye div zero anaweza kuisoma vizuri tu hivyo akiomba kusoma VETA apewe nafasi bila kujali kama ana ufaulu wowote wa elimu ya sekondari.
Kwenda chuo kikuu iwe ni kwa wanafunzi wanaopata daraja la kwanza na la pili tu baada ya kufaulu form six lakini wale wanaopata division THREE wapelekwe kusoma diploma ya anachokihitaji na kwenye ile ada yao serikali iwape mkopo kwa asilimia zisizopungua 70% ya ada maana wengi wao watakuwa ni watoto wa wale wanaoitwa wanyonge simaanishi kuwa watoto wa wanyonge ndiyo wanapata div 3 ila wanaweza kuwa wengi kuliko watoto wa wenye ahueni.
Mwanafunzi anayepata chini ya div 3 anaweza kwenda kusoma VETA kwa level yake au kurudia shule kwa mfumo wa elimu huria. Mwnafunzi wa chuo kikuu apewe mkopo si chini ya 70% pia.
FAIDA YA MFUMO HUU.
1. Kwa mfumo huu pendekezwa mwanafunzi atamaliza chuo kikuu akiwa na miaka 20 kwa watakaosoma chuo kikuu miaka 3.
2. Nchi itazalisha watendaji wengi sana (technicians) yaani watu wa level ya certificates na diploma kuliko ilivyosasa kila mtu ni graduate
3. Elimu ya ufundi itapewa wigo mpana kuliko ilivyo sasa hii itapunguza tatizo la ajira kwani watakaotoka VETA watakuwa na uwezo wa kutengeneza ajira wenyewe kuliko ilivyosasa ambapo graduates wengi hawawezi kujiajiri wenyewe hata baada ya kukaa miaka karibia 16 darasani
4. Uwekezaji kwenye vyuo vikuu utakuwa kidogo umepunguzwa maana watakaodahiliwa huko ni wachache hivyo serikali na wadau kufanya uwekezaji zaidi kwenye VYUO VYA UFUNDI PAMOJA NA VYUO VYA KATI.
5. Ndoa za utotoni zitapungua kwani wanaofeli darasa la saba watatakiwa kuendelea na VETA au kurudia shule (hii ikiratibiwa vizuri hawa bado watakuwa chini ya uangalizi wa serikali -hapa uratibu wa karibu utatakiwa kuanzia local government hadi juu kabisa)
6. Hakutakuwa na mtanzania ambaye hatakuwa na elimu au ujuzi lakini pia muda wa kukaa shule utapungua kutoka walau miaka 23 yasasa hadi 20
NB: Ni vizuri serikali iweke utaratibu wa ofisi ya mwenyekiti na mtendaji wa kijiji au mtaa kuwa na majina ya wanafunzi wote wanaotarajiwa kufanya mtihani wa darasa la saba na baada ya matokeo wajue ni wangapi wamechaguliwa kwenda sekondari na kuhakikisha kwamba wale ambao hawajachaguliwa mzazi anaitwa kuamua kama mwanaye ataenda VETA au atarudia shule.
Serikali ya kijiji ihakikishe moja kati ya hayo yanafanyika kinyume chake wazazi au walezi wawajibishwe kikamilifu.
Unakaribishwa kutoa maoni yako, unaweza kuboresha ila si vizuri kukosoa bila kutoa walau maoni bora zaidi yenye kujenga.
Kwa mfumo wetu wa sasa wa elimu mwanafunzi anaanza darasa la kwanza akiwa na miaka 7, anasoma elimu ya msingi kwa miaka 7, akifaulu anaenda sekondari kwa miaka 4, akifaulu anasoma sekondari ya juu miaka 2 na akifaulu anaenda chuo miaka 3 (au zaidi kwa baadhi ya fani). Kwa mtindo huu mtu anamaliza chuo akiwa na miaka isiyopungua 23 yaani 7+7+4+2+3. Umri huu ni mkubwa sana na ingefaa mtu huyu awe tayari anajitegemea kama mfumo wa elimu mbadala ungetumika.
Mimi napendekeza mfumo wa elimu ungekuwa hivi, mwanafunzi aanze shule akiwa na miaka 6 (hii inawezekana maana imeshazoeleka hasa mijini) sasa iwe ni sera ya nchi bila kujali jinsi ya mtoto. Halafu elimu ya msingi iwe miaka 6 tu hapa itabidi darasa la sita lasasa livunjwe masomo yanayofundishwa darasa la tano, sita na saba yaanzie darasa la nne, tano na kufika mwaka wa sita yawe yamefundishwa yote.
Wanafunzi wanafaulu elimu ya msingi kwa walau wastani Wa C waende sekondari ambako watasoma kwa miaka 3 (kama QT wanasoma elimu ya sekondary katika mazingira ya nyumbani kwa miaka 2 na wanafaulu basi wanafunzi wa shule wanaweza kufaulu vizuri tu wakisoma sekondary kwa miaka 3 tena bila shida).
Wanafunzi wanaofeli darasa la saba yaani waliopata chini ya daraja la C wapewe nafasi ya kukariri shule (ukweli wa mambo ni kwamba viongozi wetu wengi na watunga sera wetu wa sasa wengi wao walirudia shule hadi mara 4 ndiyo wakafaulu, sasa kwanini waone ni nongwa kwa mwanafunzi wa sasa kurudia shule?). Kurudia shule kwa mwanafunzi anayetaka ikubalike kisera kabisa tena bila usumbufu kwa jina lake lile lile, ila wale ambao hawataki kurudia wapelekwe VETA.
Sera ya elimu ya VETA iwe huria kwa mwanafunzi au mtu yeyote anayetaka kujifunza elimu ya ufundi bila kujali umri ilimradi huyo mtu kahitimu elimu ya msingi na anataka kujiunga kwa hiari yake. KWA WANAOFELI DARASA LA SABA IWE NI LAZIMA KWENDA VETA KAMA HATATAKA KURUDIA SHULE. Hii itazuia kuolewa kwa umri mdogo na kupunguza raia wasio na ujuzi na kazi kwa siku za baadaye
Wanaofaulu elimu ya form four kwa daraja la kwanza na la pili wapelekwe form five na six kwa miaka 2, watakaopta daraja la tatu wapelekwe vyuo vya kati (cerificates baadaye diploma) pamoja na VETA kwa anayechagua lakini kwa wenye division 4 na zero wapewe nafasi ya kwenda VETA au kurudia kama private candidates kama ilivyo kwa sasa. Kwa vile elimu ya ufundi ni ya vitendo basi hata mwenye div zero anaweza kuisoma vizuri tu hivyo akiomba kusoma VETA apewe nafasi bila kujali kama ana ufaulu wowote wa elimu ya sekondari.
Kwenda chuo kikuu iwe ni kwa wanafunzi wanaopata daraja la kwanza na la pili tu baada ya kufaulu form six lakini wale wanaopata division THREE wapelekwe kusoma diploma ya anachokihitaji na kwenye ile ada yao serikali iwape mkopo kwa asilimia zisizopungua 70% ya ada maana wengi wao watakuwa ni watoto wa wale wanaoitwa wanyonge simaanishi kuwa watoto wa wanyonge ndiyo wanapata div 3 ila wanaweza kuwa wengi kuliko watoto wa wenye ahueni.
Mwanafunzi anayepata chini ya div 3 anaweza kwenda kusoma VETA kwa level yake au kurudia shule kwa mfumo wa elimu huria. Mwnafunzi wa chuo kikuu apewe mkopo si chini ya 70% pia.
FAIDA YA MFUMO HUU.
1. Kwa mfumo huu pendekezwa mwanafunzi atamaliza chuo kikuu akiwa na miaka 20 kwa watakaosoma chuo kikuu miaka 3.
2. Nchi itazalisha watendaji wengi sana (technicians) yaani watu wa level ya certificates na diploma kuliko ilivyosasa kila mtu ni graduate
3. Elimu ya ufundi itapewa wigo mpana kuliko ilivyo sasa hii itapunguza tatizo la ajira kwani watakaotoka VETA watakuwa na uwezo wa kutengeneza ajira wenyewe kuliko ilivyosasa ambapo graduates wengi hawawezi kujiajiri wenyewe hata baada ya kukaa miaka karibia 16 darasani
4. Uwekezaji kwenye vyuo vikuu utakuwa kidogo umepunguzwa maana watakaodahiliwa huko ni wachache hivyo serikali na wadau kufanya uwekezaji zaidi kwenye VYUO VYA UFUNDI PAMOJA NA VYUO VYA KATI.
5. Ndoa za utotoni zitapungua kwani wanaofeli darasa la saba watatakiwa kuendelea na VETA au kurudia shule (hii ikiratibiwa vizuri hawa bado watakuwa chini ya uangalizi wa serikali -hapa uratibu wa karibu utatakiwa kuanzia local government hadi juu kabisa)
6. Hakutakuwa na mtanzania ambaye hatakuwa na elimu au ujuzi lakini pia muda wa kukaa shule utapungua kutoka walau miaka 23 yasasa hadi 20
NB: Ni vizuri serikali iweke utaratibu wa ofisi ya mwenyekiti na mtendaji wa kijiji au mtaa kuwa na majina ya wanafunzi wote wanaotarajiwa kufanya mtihani wa darasa la saba na baada ya matokeo wajue ni wangapi wamechaguliwa kwenda sekondari na kuhakikisha kwamba wale ambao hawajachaguliwa mzazi anaitwa kuamua kama mwanaye ataenda VETA au atarudia shule.
Serikali ya kijiji ihakikishe moja kati ya hayo yanafanyika kinyume chake wazazi au walezi wawajibishwe kikamilifu.
Unakaribishwa kutoa maoni yako, unaweza kuboresha ila si vizuri kukosoa bila kutoa walau maoni bora zaidi yenye kujenga.