Elimu ya uvaaji vibarakoa bado ni ndogo

Elimu ya uvaaji vibarakoa bado ni ndogo

Revolution

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2008
Posts
1,420
Reaction score
1,741
Habari za Asubuhi Watanzania wenzangu. Nipo Kigamboni na ninapanda sana daladala ninaona uvaaji wa barakoa (face mask) bado ni kwa kiasi kidogo sana! Uvaaji sio muhimu!?

Natoa rai wananchi wasisitizwe kuvaa barakoa. Nimeona MOI, baadhi ya hospitali na Mahakama za Tanzania wametangaza ili kupata huduma zao ni lazima kuvaa barakoa.

Kwa mtazamo wangu wananchi wengi wangeelimishwa tungeepusha maambukizi mengi. Wananchi bado wanachukulia poa sana! Tena ukivaa ukiingia kwenye daladala ni kama wanakushangaa hivi!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukipita mjini umevaa watu wanakuona kama umevaa kinyago unaonekana waajabu watu wazidi kupewa elimu wasiisha kwa mazoea
 
Ukipita mjini umevaa watu wanakuona kama umevaa kinyago unaonekana waajabu watu wazidi kupewa elimu wasiisha kwa mazoea

Ila hao wanaokucheka Wakifa kwa CORONA watakukumbuka sana wakiwa Mavumbini.
 
Ila hao wanaokucheka Wakifa kwa CORONA watakukumbuka sana wakiwa Mavumbini.
muhimu sana kuchukua hatua unazoona zitakusaidia wewe na familia yako tatizo watu wanachulia mzaha bado watu wanapeana tano mtaani
 
muhimu sana kuchukua hatua unazoona zitakusaidia wewe na familia yako tatizo watu wanachulia mzaha bado watu wanapeana tano mtaani

Nini kupeana Tano hizo Ndugu Mimi nimeshuhudia Juzi tu Watu wakisalimiana kwa Kupeana Mikono yao kisha baadae Wakabusiana vile vile.
 
Ninafurahi Mkuu wa Mkoa wa Dar Mh. Makonda ameliona hili la barakoa na ametoa maagizo. Nashauri iwe ni kwa Nchi zima na sio kwa Dar pekee.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom