Tz tunakosea tu kwenye elimu ya msingi... masomo yote kuendeshwa kwa lugha ya kiswahili na mengine yote kwa kiingereza. Wangeongeza vipindi vya kiingereza ili wanafunzi wa elimu ya msingi zaidi ya kujua kiswahili pia kujua kiingereza. Hatuwezi kumfundisha sayansi ya kiswahili mwanafunzi wa msingi halafu sekondari tumfunze kwa kiingereza au historia kiswahili historia kiingereza itakuwa tunatwanga maji kwenye kinu.
Pia wanafunzi wetu wa msingi tuwajengee mfumo wa kujieleza kwa kujiamini. Tuwatengeee wasaa wa midahalo(debates) kati ya wanafunzi wenyewe wakiwa shule za msingi au shule kwa shule. Pia kucheza maigizo ya kwenye vitabu, story books, na simulizi za hapa na pale. Kuwepo na siku ya wazazi na watoto kutoa burudani.
Mi naamini kwa mifumo hii tutawatayarisha vema wanafunzi wetu kujiunga na sekondari.
Naikubali vema syllabus zetu za sekondari zetu na vyuo ni nzuri ila vinakosa kumfanya mwanafunzi kujieleza au kuwa mwajibikaji kwa elimu yake.