Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 183,582
- 1,105,402
Lengo la elimu katika jamii ni nini? Miafrika kweli ndivyo tulivyo! Hatujui elimu hii tuliyoletewa na wazungu ina lengo gani. Mbona waliotuletea wenyewe wanaitumia vizuri?
Kama lengo lako la kwenda shule ni kutajirika basi unapoteza muda. Acha hata leo anza ujasiriamali. Lakini kama lengo lako kwenda shule ni kujipatia maarifa anuai kuhusu mambo mbalimbali hapa duniani na kukufanya uishi vizuri (hata kama siyo tajiri) basi nenda shule.
Wenzetu Ulaya kule siyo ajabu kumwona msomi profesa akienda kazini kwa baiskeli. Na ukiulizia utaambiwa profesa huyo pengine ndiye aligundua nadharia hii au ile. Kwa wenzetu usomi ni kurithisha mawazo yao kwa kizazi kipya na kuchangia knowledge kwa kizazi kijacho na ubinadamu kwa ujumla. Sisi ni kutajirika. Na tofauti hii ndiyo inayoitafuna Afrika kiasi kwamba hata wasomi wetu tunaona hawana faida kwa sababu wako bize wanatafuta utajiri. Watafanya utafiti lini? Wataandika mawazo yao lini? Watagundua vitu vipya lini? Watatoa mchango wao katika kuendekeza ujuzi wa binadamu lini? Afrika - bara la giza!!!
Kama lengo lako la kwenda shule ni kutajirika basi unapoteza muda. Acha hata leo anza ujasiriamali. Lakini kama lengo lako kwenda shule ni kujipatia maarifa anuai kuhusu mambo mbalimbali hapa duniani na kukufanya uishi vizuri (hata kama siyo tajiri) basi nenda shule.
Wenzetu Ulaya kule siyo ajabu kumwona msomi profesa akienda kazini kwa baiskeli. Na ukiulizia utaambiwa profesa huyo pengine ndiye aligundua nadharia hii au ile. Kwa wenzetu usomi ni kurithisha mawazo yao kwa kizazi kipya na kuchangia knowledge kwa kizazi kijacho na ubinadamu kwa ujumla. Sisi ni kutajirika. Na tofauti hii ndiyo inayoitafuna Afrika kiasi kwamba hata wasomi wetu tunaona hawana faida kwa sababu wako bize wanatafuta utajiri. Watafanya utafiti lini? Wataandika mawazo yao lini? Watagundua vitu vipya lini? Watatoa mchango wao katika kuendekeza ujuzi wa binadamu lini? Afrika - bara la giza!!!