Elimu ya juu huleta umasikini


Umeanza vizuri ila hapo kwenye bold umechemka. ..
Kwanza tupe scale ya utajiri.
Pili kwa taarifa yako wako madaktari matajiri, walimu maskari n.k
Kuhusu elimu ya Tanzania ... kasoro kubwa iliyopo ni kwamba ile inayoitwa elimu ya msingi siyo kabisa. Haimpi msingi mwanafunzi huyo.
Wataalam wa elimu wangeifumua na kuweka somo la Umahili wa kazi somo ambalo lingemfanya kila mtu awe makini kwa lolote analofanya.
Mi nawafahamu mafundi wa kushona ambao ni matajiri kabisa na wamefikia hatua ha kuajiri.
Namfahamu mwalimu mmoja mfugaji wa kuku wa kienyeji aliamua kuhachana na ajira na kuendelea na ufugaji,,, ni tajiri mkubwa tu.
Kuhusu maaskari ao sitaki kuwaongelea kwa sababu kila mtu anajua utajiri wao umeegemea wapi.
Nasisitiza UMAHILI WA KAZI ... hili ndilo somo ambalo kimsingi lingemkomboa mtanzania.
 
Mama Kairuki sasa aachie ajira hali imekuwa ngumu!
 
Reactions: SDG
Tukumbuke kusoma sana sio kuelimika ila kuwa na busara ni zaidi ya elimu ya darasani
Kitu cha kujiuliza ni je! yale unayoyaelewa yanakusaidia kwenye maisha? kama jibu ni ndiyo shukuru Mungu, kama jibu ni hapana ujue we ni maskini kama maskini wengine.

Kuna vijana wanajua kunyoa tu nywele wana maisha mazuri sana ...

na

Kuna vijana wame graduate fani mbali mbali wanaishi maisha ya shida.

KATI YA HAO WAWILI NANI AMEELIMIKA?
 
Alie na uhakika wa kula ndo ameelimika
 
Habari ndo hiyo ... unalikuta limtu linakutajia vyuo lilivyosoma ... linaishi nyumba ya kupanga isiyokuwa na umeme ... elimu gani hiyo!
Tatizo hawa wanao jiita wasomi wengi wanadharau sana ndo maana hata ukipata fursa hatuwezi kuwaita
 
Hapa ndio unafiki wa watanzania unapojidhihirisha! Sasa mnatajaje? Mtu asiposoma mnamwita kilaza/bashite wanaosoma, mnawaambia wanapoteza muda! Sasa mnataka nini?
 
Unajua bro mi huwa namshangaa mtu anayemdharau mwenye kiduka kidogo wakati yeye ndo mteja wa hapo; na hana duka kubwa.
Mkuu usishangae ni ulimbukeni na ujuaji pasipo kujua kazi ya hawa wasomi ni kuishi kwa hisia kama watumia ngada
 
Hapa ndio unafiki wa watanzania unapojidhihirisha! Sasa mnatajaje? Mtu asiposoma mnamwita kilaza/bashite wanaosoma, mnawaambia wanapoteza muda! Sasa mnataka nini?
Sio unafiki, ukiwa hujasoma lakini ukaendesha mambo yako kadri inavyotakiwa (bila uongo) nani atakusema.
Huyu kijana wa Arbert, Kihiyo na wengine wanasemwa kwa kuwa walidanganya umma kuwa wamesoma kumbe hakuna.
 
MTU mwenye Mali huilinda Mali yake
MTU mwenye elimu .elimu yake humlinda
MTU mwenye Mali kadiri anavyoitumia hupungua
MTU mwenye elimu kadiri anavyoitumia huongezeka MTU mwenye Mali huwa na maadui wengi
MTU mwenye elimu huwa na marafiki wengi
 
Lakini naomba kuuliza wasomi wengi wenye elimu kuanzia masters na kuendelea si wanazichukua nje ya Tanzania? Je usomi wao nje ya nchi umeleta utofauti na wale walio soma ndani ya nchi? Majibu pls
 
Lakini naomba kuuliza wasomi wengi wenye elimu kuanzia masters na kuendelea si wanazichukua nje ya Tanzania? Je usomi wao nje ya nchi umeleta utofauti na wale walio soma ndani ya nchi? Majibu pls
Nimeishaliongea hilo ... MSINGI
 
Soma kitabu kinaitwa Rich CASHFLOW Quadrants kifanyie kazi kitabu baada ya miaka mitano niletee zawadi ya subaru ni moja ya vitabu vimebadilisha maisha yangu.
Watanzania wengi tunasoma ili tu professional employer instead to be professional investors.
Wakati mwingine kama huna hoja ya maana kuleta jF bora ukae kimya.
 
Soma kitabu kinaitwa Rich CASHFLOW Quadrants kifanyie kazi kitabu baada ya miaka mitano niletee zawadi ya subaru ni moja ya vitabu vimebadilisha maisha yangu.
Watanzania wengi tunasoma ili tu professional employer instead to be professional investors.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…