Elimu ya Bure ya Lowassa ni Kiini Macho

Elimu ya Bure ya Lowassa ni Kiini Macho

kama serikali sikivu imeshuhudia madini ya trillion 36yakiuzwa na yenyewe ikiambulia hela za maandazi sh trillion 1.8 ,inashindikana nini kwa serikali makini kuchukua zaidi ya 50%ya hizo pesa kwa sababu madini ni yetu atashindwa nini kulipa 1.2trilion kwa sababu ya vijana wetu.
 
Ukweli wa elimu bure ya Lowassa huu hapa.


Mgombea urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Mh. Edward Lowassa.
Ahadi aliyoitoa mgombea urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), ya kutoa elimu ya Chuo Kikuu bure inaweza kugharimu Taifa kiasi cha Sh. trilioni 1.35($675millioni) kwa mwaka, Nipashe limebaini.

Lowassa katika uzinduzi wake wa kampeni alitoa ahadi ya kutoa elimu bure kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu iwapo atachaguliwa kuwa rais wa awamu ya tano-hali iliyozua ubishi kutoka kwa Chama Cha Mapinduzi.

Baadhi ya vigogo wa CCM wanadai ni ndoto kutoa elimu bure kwa kuzingatia hali ya uchumi wa nchi, huku kambi ya Lowassa ikisisitiza kwamba jambo hilo linawezekana endapo raslimali za taifa zitatumika ipasavyo.

Gazeti hili limefanya uchambuzi kwa kutumia takwimu mbalimbali zikiwamo zile za serikali ili kuweza kubaini gharama za elimu bure, lakini kwa kuzingatia elimu ya chuo kikuu tu.

Kwa mujibu wa uchambuzi huo, kwa mwaka 2016 pekee, endapo mathalan kutakuwa na wanafunzi 300,000 katika vyuo vikuu vya umma na binafsi, gharama zinaweza kuwa Sh. trilioni 1.35 kwa mwaka.

Gharama hizi kwa mwaka ni sawa na asilimia 6 ya bajeti ya Serikali kwa kuzingatia bajeti ya mwaka 2015/16 ambayo ni Sh. 22.495 trillion kama ilivyowasilishwa na kupitishwa na bunge Juni mwaka huu mjini Dodoma.

Gazeti hili limetumia wastani wa Sh. milioni 4.5 kwa kila mwanafunzi wa chuo kikuu kwa mwaka kwa ajili ya ada na matumizi mengineyo.

Hata hivyo, zipo baadhi ya shahada kama uhandisi na udaktari ambazo wanafunzi hupewa wastani wa milioni 6 kwa mwaka kama gharama ya masomo na matumizi mengineyo.

Kwa maana nyingine, gharama yote ya kuwasomesha wanafunzi bure katika vyuo vikuu Tanzania kwa mwaka kama alivyoahidi Lowassa ni sawa na thamani ya kununua mashangingi (Toyota Land Cruiser VX-V8) 3,375.

Ghari jipya aina ya Land Cruiser VX-V8 maarufu kama shangingi hugharimu kiasi cha dola za Marekani 200,000(Sh. milion 440) kulingana na takwimu ambazo Nipashe imezikusanya toka vyanzo mbali mbali.

Kwa lugha rahisi kwa mujibu wa uchambuzi wa Nipashe, Shangingi moja huweza kugharimia masomo kwa wanafunzi 97 kwa mwaka kusoma shahada ya kwanza chuo kikuu.

Gharama hizi pia ni sawa na asilimia 11 ya makusanyo yote yaliyofanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/14.

Kwa mujibu wa uchambuzi wa Nipashe, gharama hizi ni sawa na asilimia 75 ya misamaha yote ya kodi iliyotolewa nchini katika mwaka wa fedha wa 2013/14.

Kwa mwaka kulingana na ripoti ya kamati ya Bajeti ya Bunge misamaha ya kodi nchini ilifikia kiwango cha juu cha Sh. trillion 1.8 kwa mwaka wa fedha wa 2013/14, sawa na asilimia 4.3 ya pato la taifa—zaidi ya kiwango kinachokubalika kitaalamu cha asilimia moja tu.

Ingawa Nipashe haikuweza kuipata idadi kamili ya magari ya shangingi yanayomilikiwa na serikali, uzoefu unaonyesha kuwa aina hiyo ya magari inatumiwa na watumishi wakubwa wa serikali.
Watumishi hawa ni wa kuanzia hadhi ya wakurugenzi, makamishina, makatibu wakuu, naibu mawaziri, mawaziri, majaji na wakurugenzi wote wa mashirika ya umma.

Pia magari hayo yanatumika na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, kama vile jeshini, Polisi, Magereza, Takukuru na hata kwenye idara za serikali zinazojitegemea.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipoingia madarakani alitangaza kuchukua hatua madhubuti za kupunguza matumizi ya magari hayo serikalini, lakini juhudi zake hazikuzaa matunda.

Matumizi ya magari hayo yanatajwa kuwa ni moja ya eneo ambalo serikali inatumia fedha nyingi za walipa kodi, huku mahitaji mengine ya msingi ya wananchi kama elimu, afya na maji yakikosa fedha za kuleta matokeo makubwa chanya kila mwaka wa fedha.

Share na wenzako
 
Ndugu wana JF leo gazeti la Nipashe limetoa mchanganuo wa gharama za Elimu ambazo Lowassa anasema anaweza kuzikabili na hatimaye watanzania wakasoma bure hadi chuo kikuu . Ingawa naipenda Ukawa lakini dosari hizi za wazi katika kuchanganua mambo hazipaswi ziachwe bila kutolewa tahadhari ili mgombea wetu wa Ukawa apate kuaminiwa kwa kile anachokisema.

Kiukweli upembuzi ule umeacha maswali mengi bila majibu huku nikihoji uwezo wa serikali ya Ukawa kutoa Elimu hiyo bure kwa ngazi zote za Elimu kuanzia chekechea. Gharama za Elimu ya juu pekee ni 6% ya budget ya 2014/2015. Na ukweli hizo ni fedha za kujikimu za wanafunzi 300,000 tu kwa mwanafunzi mmoja kupewa TZS 4.5m. Hapo hatujazingatia mishahara ya waalimu, tuition fees na vifaa vya kufundishia. Katika hali hii ni dhahira serikali itaelemewa na kutoa bora elimu kuliko elimu bora. Mzigo huo wa gharama ya elimu ukijumlishwa na shule za sekondari, msingi na chekechekea ni dhahiri elimu itachukua zaidi ya asilimia 20 ya budget ya nchi. Kama hii itakuwa hivyo ni dhahiri sekta nyingi muhimu zitaathirika na kupunguz a ufanisi wa serikali.

Tunahitaji majibu kutoka kwa ukawa kama kweli hii sera inaweza kutelezeka na kwa namna gani. Tusifanye masihara na hili. Lakini lazima watueleze kuhusu Tertiary Education nayo itakuwa buree au vipi?


Mbona Nyerere aliweza Na zilikua zama za Giza?
 
Elimu ya bure ya lowassa inawezekana sana tena sana...nyerere aliwezaje bila tanzinite gesi etc...muulize mtu wa zamani hadi nauli za kurudi makwenu zilikuwa zinapewa mashuleni

Huwezi kufananisha enzi za nyerere na sasa.

Kwa miaka hii idadi ya watu ni kubwa na muamko wa elimu uko juu kuliko ilivyokuwa zamani kwa hiyo wananfunzi ni wengi.

Enzi za mwalimu kijiji kizima wanaweza wakafaulu watu 10 tu kwenda sekondari ndio maana ilikuwa rahisi kusomesha watu bure.
 
Hapo kwenye READ umeanza angalau kuwa na kujitambua kidogo, kwa hiyo unakubali kwamba lowasa sio kweli kwamba atatoa elimu bure kwa maana kila kitu bure??

Unaongea kitu usichojua. Mimi nakuambia kitu ambacho nimefanya. Au labda mtu anaposema ''elimu bure'' wewe unaelewaje? Kwasababu tunaweza kuwa tunabishana na mtu anayefikiri elimu bure ina maana ya kila kitu bure
 
Lowassa angesema habari ya kupunguza ada ningemwelewa kabisa.. ila kusema eti bure aaa hapa ni uongo.
si kwamba elimu bure haiwezekani, inawezekana ila ni mpaka matumizi ya pesa yapunguzwe mfano kupunguza mishahara ya wabunge mawaziri na rais angalau kwa asilimia 50 hiyo tu inaweza kutimiza ndoto ya elimu bure... sasa mbu ge gani atakubali kulipwa 6mi..??
 
We piga kura ili EL aingie ikulu, kama ulaghai si utaona. Hii nchi watu wameiba fedha hadi mhe. Rais akawabembeleza warudishe tushindwe somesha vijana wetu bure.
 
Kwa hapa tulipofika tunahitaji kuweka nguvu kubwa kwenye elimu ili tutoke hapa. Hakuna lisilowezekana kama tukita.
 
Ndugu wana JF leo gazeti la Nipashe limetoa mchanganuo wa gharama za Elimu ambazo Lowassa anasema anaweza kuzikabili na hatimaye watanzania wakasoma bure hadi chuo kikuu . Ingawa naipenda Ukawa lakini dosari hizi za wazi katika kuchanganua mambo hazipaswi ziachwe bila kutolewa tahadhari ili mgombea wetu wa Ukawa apate kuaminiwa kwa kile anachokisema.

Kiukweli upembuzi ule umeacha maswali mengi bila majibu huku nikihoji uwezo wa serikali ya Ukawa kutoa Elimu hiyo bure kwa ngazi zote za Elimu kuanzia chekechea. Gharama za Elimu ya juu pekee ni 6% ya budget ya 2014/2015. Na ukweli hizo ni fedha za kujikimu za wanafunzi 300,000 tu kwa mwanafunzi mmoja kupewa TZS 4.5m. Hapo hatujazingatia mishahara ya waalimu, tuition fees na vifaa vya kufundishia. Katika hali hii ni dhahira serikali itaelemewa na kutoa bora elimu kuliko elimu bora. Mzigo huo wa gharama ya elimu ukijumlishwa na shule za sekondari, msingi na chekechekea ni dhahiri elimu itachukua zaidi ya asilimia 20 ya budget ya nchi. Kama hii itakuwa hivyo ni dhahiri sekta nyingi muhimu zitaathirika na kupunguz a ufanisi wa serikali.

Tunahitaji majibu kutoka kwa ukawa kama kweli hii sera inaweza kutelezeka na kwa namna gani. Tusifanye masihara na hili. Lakini lazima watueleze kuhusu Tertiary Education nayo itakuwa buree au vipi?

Shangingi 1 = ada ya wanafunzi wa vyuo 97.

Tanzania kuna mashangingi mangapi?
 
Ndugu wana JF leo gazeti la Nipashe limetoa mchanganuo wa gharama za Elimu ambazo Lowassa anasema anaweza kuzikabili na hatimaye watanzania wakasoma bure hadi chuo kikuu . Ingawa naipenda Ukawa lakini dosari hizi za wazi katika kuchanganua mambo hazipaswi ziachwe bila kutolewa tahadhari ili mgombea wetu wa Ukawa apate kuaminiwa kwa kile anachokisema.

Kiukweli upembuzi ule umeacha maswali mengi bila majibu huku nikihoji uwezo wa serikali ya Ukawa kutoa Elimu hiyo bure kwa ngazi zote za Elimu kuanzia chekechea. Gharama za Elimu ya juu pekee ni 6% ya budget ya 2014/2015. Na ukweli hizo ni fedha za kujikimu za wanafunzi 300,000 tu kwa mwanafunzi mmoja kupewa TZS 4.5m. Hapo hatujazingatia mishahara ya waalimu, tuition fees na vifaa vya kufundishia. Katika hali hii ni dhahira serikali itaelemewa na kutoa bora elimu kuliko elimu bora. Mzigo huo wa gharama ya elimu ukijumlishwa na shule za sekondari, msingi na chekechekea ni dhahiri elimu itachukua zaidi ya asilimia 20 ya budget ya nchi. Kama hii itakuwa hivyo ni dhahiri sekta nyingi muhimu zitaathirika na kupunguz a ufanisi wa serikali.

Tunahitaji majibu kutoka kwa ukawa kama kweli hii sera inaweza kutelezeka na kwa namna gani. Tusifanye masihara na hili. Lakini lazima watueleze kuhusu Tertiary Education nayo itakuwa buree au vipi?

Kikao kimoja pale bandalini kilitumia Tsh. billion 9, vipi kuhusu ziara za Kikwete nje ya nchi katumia sh. Ngapi? Madini tunalipwa 3% tena mrahaba Lowasa amesema itakuwa 30%. Ni vema ukatafakari kwa kina kama Libya ya Gaddafi aliweza kutoa elimu, Afya, Maji, na pembejeo za kilimo bure tena kwa kutumia hazina ya mafuta inakuwaje sie tushindwe?
 
Shangingi 1 = ada ya wanafunzi wa vyuo 97.

Tanzania kuna mashangingi mangapi?

hahaa huo uwiano wa shangingi moja kwa wanafunzi 97 ni uongo uliopitiliza. hao waliopiga hizo hesabu hawana data kabisa za kutosha
 
hahaa huo uwiano wa shangingi moja kwa wanafunzi 97 ni uongo uliopitiliza. hao waliopiga hizo hesabu hawana data kabisa za kutosha

Mkuu Hebu lete hizo takwimu sahihi shindanisha na zao ili isaidie kwenye kufanya maamuzi

Swali kubwa ni je unajua bei ya hizo shangingi kuitungua mpya?? (Achana na zile USED za Beforward)

Kwa makadirio kulingana na specifications zinacheza kwenye 60,000$ to 65,000$ (ukiipiga kwenye madafu ni zaidi ya 130Millioni....Je hujalipa ada za watoto kibao???

Pia unajua unywaji wake wa mafuta?
 
Kuongeza mikoa,wilaya,wizara nyingi hiyo budget yake ipo.Unajua gharama yake.kuanzia madereva wa wakuu wa mikoa,wilaya,wafanya kazi ofisi ya mkuu wa mkoa,wa wilaya.hata nisiende mbali.mwenye upeo anajua tukibana mianya hiyo basi .tosha kabisa
 
Huna akili ndugu. Unadhani ipi itawajibika kutoa elimu, kati ya serikali ya ukawa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tz?

Huna fikra na hujitambui
 
Elimu bure inawezekana. Ila hauwezekanivkwa mwenendo wa sasa waserikali katuka utendaju kazi na udhibiticwa wizi na matumizi makubwa. Lazima yafanyike mabadiliko makubwa. Vuongozi wetu wakubali kuacha kuishickm miungu watu! Viingozi wanatuambia nchi maskini lakini wao wanaishi km wapo peponi. Haiwezekani. Lazima huo umaskini uonekane pia kwa viongozi wetu kubana matumizi
 
Mkuu Hebu lete hizo takwimu sahihi shindanisha na zao ili isaidie kwenye kufanya maamuzi

Swali kubwa ni je unajua bei ya hizo shangingi kuitungua mpya?? (Achana na zile USED za Beforward)

Kwa makadirio kulingana na specifications zinacheza kwenye 60,000$ to 65,000$ (ukiipiga kwenye madafu ni zaidi ya 130Millioni....Je hujalipa ada za watoto kibao???

Pia unajua unywaji wake wa mafuta?

takwimu hapo zinaonesha kila mwanachuo kwa mwaka anahitaji 4.5mil, hiyo kwa wanafunzi 97 ni zaidi ya 430mil, sasa si umeona kuwa hiyo 130mil ya vx mpya haitoshi kwa wanafunzi 97..!!
 
Ndugu wana JF leo gazeti la Nipashe limetoa mchanganuo wa gharama za Elimu ambazo Lowassa anasema anaweza kuzikabili na hatimaye watanzania wakasoma bure hadi chuo kikuu . Ingawa naipenda Ukawa lakini dosari hizi za wazi katika kuchanganua mambo hazipaswi ziachwe bila kutolewa tahadhari ili mgombea wetu wa Ukawa apate kuaminiwa kwa kile anachokisema.

Kiukweli upembuzi ule umeacha maswali mengi bila majibu huku nikihoji uwezo wa serikali ya Ukawa kutoa Elimu hiyo bure kwa ngazi zote za Elimu kuanzia chekechea. Gharama za Elimu ya juu pekee ni 6% ya budget ya 2014/2015. Na ukweli hizo ni fedha za kujikimu za wanafunzi 300,000 tu kwa mwanafunzi mmoja kupewa TZS 4.5m. Hapo hatujazingatia mishahara ya waalimu, tuition fees na vifaa vya kufundishia. Katika hali hii ni dhahira serikali itaelemewa na kutoa bora elimu kuliko elimu bora. Mzigo huo wa gharama ya elimu ukijumlishwa na shule za sekondari, msingi na chekechekea ni dhahiri elimu itachukua zaidi ya asilimia 20 ya budget ya nchi. Kama hii itakuwa hivyo ni dhahiri sekta nyingi muhimu zitaathirika na kupunguz a ufanisi wa serikali.

Tunahitaji majibu kutoka kwa ukawa kama kweli hii sera inaweza kutelezeka na kwa namna gani. Tusifanye masihara na hili. Lakini lazima watueleze kuhusu Tertiary Education nayo itakuwa buree au vipi?
Vipi na elimu bure ya Magufuli? Nayo ina mashiko?
 
Back
Top Bottom