martyr2012
JF-Expert Member
- Jul 18, 2012
- 603
- 245
Ndugu wana JF leo gazeti la Nipashe limetoa mchanganuo wa gharama za Elimu ambazo Lowassa anasema anaweza kuzikabili na hatimaye watanzania wakasoma bure hadi chuo kikuu . Ingawa naipenda Ukawa lakini dosari hizi za wazi katika kuchanganua mambo hazipaswi ziachwe bila kutolewa tahadhari ili mgombea wetu wa Ukawa apate kuaminiwa kwa kile anachokisema.
Kiukweli upembuzi ule umeacha maswali mengi bila majibu huku nikihoji uwezo wa serikali ya Ukawa kutoa Elimu hiyo bure kwa ngazi zote za Elimu kuanzia chekechea. Gharama za Elimu ya juu pekee ni 6% ya budget ya 2014/2015. Na ukweli hizo ni fedha za kujikimu za wanafunzi 300,000 tu kwa mwanafunzi mmoja kupewa TZS 4.5m. Hapo hatujazingatia mishahara ya waalimu, tuition fees na vifaa vya kufundishia. Katika hali hii ni dhahira serikali itaelemewa na kutoa bora elimu kuliko elimu bora. Mzigo huo wa gharama ya elimu ukijumlishwa na shule za sekondari, msingi na chekechekea ni dhahiri elimu itachukua zaidi ya asilimia 20 ya budget ya nchi. Kama hii itakuwa hivyo ni dhahiri sekta nyingi muhimu zitaathirika na kupunguz a ufanisi wa serikali.
Tunahitaji majibu kutoka kwa ukawa kama kweli hii sera inaweza kutelezeka na kwa namna gani. Tusifanye masihara na hili. Lakini lazima watueleze kuhusu Tertiary Education nayo itakuwa buree au vipi?
Kiukweli upembuzi ule umeacha maswali mengi bila majibu huku nikihoji uwezo wa serikali ya Ukawa kutoa Elimu hiyo bure kwa ngazi zote za Elimu kuanzia chekechea. Gharama za Elimu ya juu pekee ni 6% ya budget ya 2014/2015. Na ukweli hizo ni fedha za kujikimu za wanafunzi 300,000 tu kwa mwanafunzi mmoja kupewa TZS 4.5m. Hapo hatujazingatia mishahara ya waalimu, tuition fees na vifaa vya kufundishia. Katika hali hii ni dhahira serikali itaelemewa na kutoa bora elimu kuliko elimu bora. Mzigo huo wa gharama ya elimu ukijumlishwa na shule za sekondari, msingi na chekechekea ni dhahiri elimu itachukua zaidi ya asilimia 20 ya budget ya nchi. Kama hii itakuwa hivyo ni dhahiri sekta nyingi muhimu zitaathirika na kupunguz a ufanisi wa serikali.
Tunahitaji majibu kutoka kwa ukawa kama kweli hii sera inaweza kutelezeka na kwa namna gani. Tusifanye masihara na hili. Lakini lazima watueleze kuhusu Tertiary Education nayo itakuwa buree au vipi?