Elimu Bure Vyuo Vikuu, Lowasa kalenga mbali

Elimu Bure Vyuo Vikuu, Lowasa kalenga mbali

Ni ahadi ngumu kutimiza lakini Mungu akijalia ikatimizwa basi umasikini utakua umepunguzwa kwa asilimia kubwa sana. Hali ya mzunguko wa fedha nchini ni mbaya sana jambo linaloathiri biashara zote na si kwamba watu hawana pesa ila kutokana na mwamko wa elimu kipaumbele cha kila mzazi ni kugharamia elimu ya mwanae. Endapo atabebewa mzigo huo basi angalau atamudu kula milo miwili, ataweza kujenga makazi bora, na hata kuweza kunywa soda wikendi kama si bia. Fedha zitarejea kwenye mzunguko na biashara nyingi zitapata uhai.

Elimu bure vyuo vikuu itawezekana kuanzia 2020 siyo kuanzia j3 tar 29 kama lowasa anavyoahidi. Huko ni kuongopea watu.
 
Kipindi hicho wanafunzi walikuwa wangapi? Tena miaka hiyo huenda walikuwa wanapikiwa msosi kama sekondari. Wanafunzi wote walikuwa wanapata accommodation vyuo, sasa hali ni tofauti. Nafikiri kuna assignment kubwa ya kufanya kabla hatujaifikia.

Mimi ni kati ya hao wanafunzi wa enzi ya kila kitu bure. Kipindi hicho Faculty iliyokuwa inachukua wanafunzi wengi ilikuwa engineering na jumla ya wanafunzi kwa mwaka wa kwanza tulipoanza sisi ilikuwa 180. faculty of law ilikuwa inachukuwa wanafunzi 20. na jumla ya wanafunzi wote kwa faculty nzima ilikuwa 60. Huo ni mfano tu.
 
Aiseee yaani billions zipatekane watu kugawana ila elimu haiwezekani.????
 
Kipindi hicho wanafunzi walikuwa wangapi? Tena miaka hiyo huenda walikuwa wanapikiwa msosi kama sekondari. Wanafunzi wote walikuwa wanapata accommodation vyuo, sasa hali ni tofauti. Nafikiri kuna assignment kubwa ya kufanya kabla hatujaifikia.

Elimu bure vyuo vikuu itawezekana kuanzia 2020 siyo kuanzia j3 tar 29 kama lowasa anavyoahidi. Huko ni kuongopea watu.

Hoja yako ni nini hasa!!!

Mbona unakuwa kama mlevi???
Embu kaa chini usome ukitafakari haya mabandiko mawili utajishtukia.
 
Mimi ni kati ya hao wanafunzi wa enzi ya kila kitu bure. Kipindi hicho Faculty iliyokuwa inachukua wanafunzi wengi ilikuwa engineering na jumla ya wanafunzi kwa mwaka wa kwanza tulipoanza sisi ilikuwa 180. faculty of law ilikuwa inachukuwa wanafunzi 20. na jumla ya wanafunzi wote kwa faculty nzima ilikuwa 60. Huo ni mfano tu.

mkuu, kumbuka hadi leo budget ya mishahara na ukarabati wa majengo inatoka serikalini hebu tuambie ada wanazolipa wanafunzi za kazi gani?

Wakati wenu law school ilikuwa na wanafunzi 20, leo kaone mwalimu mmoja anafundisha wanafunzi elfu moja hadi elfu tatu ukienda socialogy na bado ada wanalipa, sasa kwanini wasisome bure wakati mwalimu analipwa na serikali?
 
Huenda ni kwa kukosa uelewa kamili au ni kwa kukusudia ila atakuwa kalenga mbali na kukosa shabaha. Gharama za elimu ya chuo kikuu ni kama:-
1. Tuition fee
2. Meals and accommodation
3. Practical training/industrial practices nk
4. Special faculty requirements.
Je ikiwa bure ni kipi kitatolewa bure au vyote.
Je, loans board itafutwa?
Je, kama ikifutwa, mbona hatusikii kuwa wadaiwa wa loans board watafutiwa madeni yao, maana hakutakuwa na wakuyakusanya.
Hii ahadi imepakwa rangi ila ni sawa na kumpa mbu kazi ya kutibu malaria.

Ndugu hilo suala linawezekana, kwa sababu mpaka muda huu watu wanasoma na asilimia( 80%) ya wanaograduate wapo Mitaani hawajapata kazi ,wengine na miaka zaidi ya mitano mitaani hawajapata kazi. na hao waliyopata kazi ni asilimia 54% ndiyo wameanza kulipa hiyo mikopo ya loan board.

Na mpaka sasa Loan board hajawahi kusema kwamba imefilisika kwa kutolipwa madeni yao.


LOWASSA atakachokifanya ni KUibadilisha Higher Education Students'Loan Borard (HESLB) na kuwa Higher Education students' Financial Support(HESFS)
Hili linawezekana kulingana na Rasilimali tulizokuwa nazo.
 
hv unajua loan board ilianzishwa lini?...HESLB became operational in July 2005.kabla yahapo watu walikua wanasoma vyuoni kwa hela ya serikali kila gharama ilikua covered..
Hata mimi namshangaa sana huyu jamaa anadhana wasomi wote wamesomeshwa na mikopo daaa!!!tatizo wamegubikwa na blanket la ccm halafu kuna baadhi naona wanamsapoti utadhani kaongea pointi kumbe hakuna anachokijua.
 
Hajatuambia fedha za kutoa elimu ya bure anazipataje,hatukubaliani na mamvi,anatupotosha
 
Ni ahadi ngumu kutimiza lakini Mungu akijalia ikatimizwa basi umasikini utakua umepunguzwa kwa asilimia kubwa sana. Hali ya mzunguko wa fedha nchini ni mbaya sana jambo linaloathiri biashara zote na si kwamba watu hawana pesa ila kutokana na mwamko wa elimu kipaumbele cha kila mzazi ni kugharamia elimu ya mwanae. Endapo atabebewa mzigo huo basi angalau atamudu kula milo miwili, ataweza kujenga makazi bora, na hata kuweza kunywa soda wikendi kama si bia. Fedha zitarejea kwenye mzunguko na biashara nyingi zitapata uhai.

Una akili sana mkuu kama za Lowassa kuona mbali zaidi
 
Tatizo la CCM na wafuasi wake ni kuishiwa pumzi, hawana uwezo wa kupanda mlima tena.

Tunawashauri kubalini mpumzike, mpate pumzi labda mtaweza tena kuanza kukwea mlima!

Hakuna kitakachowekana kwenu kwa sababu mmengwa ktk mazoea hayo na imani ya "everything is impossible!"

Elimu ya watoto na vijana wetu itagharamiwa na serikali kuanzia chekechea hadi chuo kikuu. Andaeni watoto wenu wenye sifa ya kusoma, serikali yao ijayo chini ya CHADEMA/UKAWA ikiongozwa na Rais Edward N. Lowassa itawapa fursa hiyo bila kikwazo!!
 
Hivi kweli kuna wanaoamini hiyo ahadi inaweza kabisa kutimizwa katika zama hizi?

hivi mnadhani nchi hii haina hela???kwa taarifa yenu tanzania haina shida na pesa hata kidogo,tunatatizo la management tu.tukiweza kutatua tatizo hilo umaskini bai bai.
nchi hii ina maziwa na asali,uongozi tu ndo hatuna
 
hv unajua loan board ilianzishwa lini?...HESLB became operational in July 2005.kabla yahapo watu walikua wanasoma vyuoni kwa hela ya serikali kila gharama ilikua covered..

Nakumbuka tulikuwa tunaita boom'..maisha yalikuwa mazuri tu kwa siku tulikuwa tunapewa meal allowance sh.5000. Nakumbuka SUA kulikuwa pia na mabasi ya shule, mtrekta ya kujifunzia, na vitu vingi vingi vizuri. Na elimu ilikuwa bora ukilinganisha na sasa. elimu bure inawezekana hata vivuko kuwa bure inawezekana cha msingi kuwepo na 'political will' ambayo imekosekana CCM!
 
Hajatuambia fedha za kutoa elimu ya bure anazipataje,hatukubaliani na mamvi,anatupotosha

Atawafilisi wajomba wako walioiba hela za escrow,meremeta, iptl,epa,richmond, mabehewa, THC ...zote hizo ni hela. pia kumbuka hela 'za mboga' zinaweza lipia zaidi ya wanafunzi 10 wa chuo kikuu kwa muhula!
 
Lowassa keshasema punde akichukua nchi. Siku 100 za mwanzo,atakuwa dictator wa maendeleo,nchi itakuwa on a semi war footing,hakuna waziri kwenda likizo- ikiwezekana hata kuapishwa kwake kutakuwa low key sana-anatambua the gigantic task facing him katika kurekebisha the years of hurt inflicted on Tanzanians by CCM
 
Hoja yako ni nini hasa!!!

Mbona unakuwa kama mlevi???
Embu kaa chini usome ukitafakari haya mabandiko mawili utajishtukia.
Hayo mabandiko mawili hayapingani. Sera ya elimu ya mwaka 1995 ilitaja elimu ya msingi kuwa free and compulsory. Baada ya mafanikio ya MME na MES inaonesha kuwa kumbe tukisema secondary ndo iwe free and compulsory tunazo scientific bases. Hii mihemko ya kisema tuifanye elimu ya chuo kikuu ndo owe f&c ni kukurupuka.
 
Hayo mabandiko mawili hayapingani. Sera ya elimu ya mwaka 1995 ilitaja elimu ya msingi kuwa free and compulsory. Baada ya mafanikio ya MME na MES inaonesha kuwa kumbe tukisema secondary ndo iwe free and compulsory tunazo scientific bases. Hii mihemko ya kisema tuifanye elimu ya chuo kikuu ndo owe f&c ni kukurupuka.

Kwa maelezo yako bandiko la kwanza elimu bure iliwezekana sababu ilikuwa idadi ya wanafunzi husika.maana yake kwa sasa haiwezekani sababu wanafunzi wamekuwa wengi.

Wakati huo huo unasema labda miaka ya baadae huku ukisahahu kama ilishindikana mwaka huu kwa sababu ya uwingi Wa wanafunzi,basi miaka ya baadae haitawezekana hata elimu bure kwa shule za chekechea.

Kwa wizi wa escrow,iptl,Richmond,misamaha ya kodi,bajeti kubwa za safar za mh,mikataba mibovu ya madini,
Ni miujiza gani unahiyajika zaidi ya maamuzi kuwa kuanzia sasa elimu bure.

Najua ndani ya ccm haitawezekana miaka 10000,ndio serikali unayoizungumzia hapa??
 
Tatizo la CCM na wafuasi wake ni kuishiwa pumzi, hawana uwezo wa kupanda mlima tena.

Tunawashauri kubalini mpumzike, mpate pumzi labda mtaweza tena kuanza kukwea mlima!

Hakuna kitakachowekana kwenu kwa sababu mmengwa ktk mazoea hayo na imani ya "everything is impossible!"

Elimu ya watoto na vijana wetu itagharamiwa na serikali kuanzia chekechea hadi chuo kikuu. Andaeni watoto wenu wenye sifa ya kusoma, serikali yao ijayo chini ya CHADEMA/UKAWA ikiongozwa na Rais Edward N. Lowassa itawapa fursa hiyo bila kikwazo!!
Hakuna anayepinga watoto kusoma bure...! Tunachokataa ni kuongopewa kuwa hili ni jambo linaweza kutokea kwa ghafla bin vuu. Technically, unaposema elimu bure kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu una-include hata vyuo vya kati. Kwa mtu aliye sober atagundua kuwa it's too over ambitious.
 
Back
Top Bottom