Elimu bure iondolewe, watu waanze kulipa Ada

Elimu bure iondolewe, watu waanze kulipa Ada

Habar naomba kuchangia
Mimi ni mmoja wa wanufaika wa elimu bure. Japo ni kwa mwaka mmoja tu 2016 nilikua form four. Advance elimu sio bure kuna ada kama kawaida. Nililipa kwa sasa nipo chuo kikuu. Ada ni laki na hamsini mbaka laki na themanini (ukichukua ada plus additional cost)...

Mkuu hongera sana kwa mchango wako, pamoja na kunufaika na elimu bure, je unazijua athari za elimu bure hasa katika nchi masikini kama nchi yetu?
 
Yani Hata elimu hii hutaki watoto wa masikini wapate? Hii ni karibu na ushetani
 
Umesema vyema mkuu, lakini hujasikia wakisema elimu ni bure kwa sasa?
Nimeskia sana viongozi na watu mbalimbali kwa wingi wakidai ni elimu bure. Kiuhalisia na ufasaha ni elimu bila malipo au elimu pasi ya malipo maana kodi zinakokusanywa katika taifa huelekezwa katika elimu.

Iwekwe wazi na ifanyiwe sasisho jipya kwa tangazo maalum la serikali kwa kusema ni elimu bila malipo kama walivyowahi kupitisha zuio la kuita uwanja wa taifa - Dar es Salaam "Kwa Mchina".
 
Inategemea na eneo analo ishi kuna njia zipi za kupata kipato. Yawezekana ikashindikana

Hakuna mtu anayeshindwa kulipa hiyo 20,000 kama ada labda awe mgonjwa wa mwaka mzima

Unajua elfu ishirini kwa miezi 12 ni 1666.6
 
Hakuna elimu bure! Ni elimu bila malipo inayotokana na kodi yako unapouza fasihi mtandao kwa kununua DATA na yule mtoto anayenunua pipi dukani.

Hamna kiongozi yeyote mwenye pesa mfukoni ya kutoa elimu bure.
Kazi mnafanya wananchi wenyewe na sifa zinaenda kwa raisi. Mnalipa kodi. Hakuna bure. Kodi imeongezwa mishahara imepunguzwa.
 
Nimeskia sana viongozi na watu mbalimbali kwa wingi wakidai ni elimu bure. Kiuhalisia na ufasaha ni elimu bila malipo au elimu pasi ya malipo maana kodi zinakokusanywa katika taifa huelekezwa katika elimu.

Iwekwe wazi na ifanyiwe sasisho jipya kwa tangazo maalum la serikali kwa kusema ni elimu bila malipo kama walivyowahi kupitisha zuio la kuita uwanja wa taifa - Dar es Salaam "Kwa Mchina".

Kodi kukusanywa katika sekta nyingine alafu zikaachwa kwenye sekta ya elimu huoni inagharimu uendeshaji wa sekta ya elimu?
Kwa maana sekta ya elimu haizalishi chochote kwa serikali zaidi ya pesa za mitihani.

Hujasikia mpaka wasahishaji wa mitihani wakati mwingine wakilalamika kuwa malipo yamekuwa changamoto?

Elimu bila malipo katika nchi masikini ni kuwapa mzigo na kuzipa mzigo sekta zingine kugharamia sekta ya elimu ambayo ingeweza kujiendesha yenyewe kwa mapato yatokanayo na Ada
 
Hakuna mtu anayeshindwa kulipa hiyo 20,000 kama ada labda awe mgonjwa wa mwaka mzima

Unajua elfu ishirini kwa miezi 12 ni 1666.6
Sawa. Ila yanawezekana usione kwako ni pesa ndogo kwa wengine ni midhihani kupata Hata 200 kwa siku usidharau haya mabo yapo
 
Sawa. Ila yanawezekana usione kwako ni pesa ndogo kwa wengine ni midhihani kupata Hata 200 kwa siku usidharau haya mabo yapo

Sijaidharau mkuu ila nazungumzia uhalisia
Ndio maana humu ndani kuna watu wanasema Ada imeondolewa lakini michango ipo, kumbuka michango huwa zaidi ya ada.
 
Sishurutishi watu, bali nazungumza jambo lenye faida kwenye jamii.

Wewe mtu asome bure, unafikiri akili itaunda mtazamo gani kwenye maisha hasa katika jamii masikini?
Itaunda mtazamo chanya hasa kwenye matumizi sahihi ya kodi😁
 
Kodi kukusanywa katika sekta nyingine alafu zikaachwa kwenye sekta ya elimu huoni inagharimu uendeshaji wa sekta ya elimu?
Kwa maana sekta ya elimu haizalishi chochote kwa serikali zaidi ya pesa za mitihani...
Sioni ubaya wowote katika hili. Pesa zinazotokana na utalii zielekezwe kwenye elimu.
 
Mkuu usipolipa Ada kuna uwezekano wa kutafuta ajira, ukilipa ada ajira zipo tuu,aidha ujiajiri au uajiriwe.

Mtu akishazoea dezo/vya bure anataka mpaka kazi apewe kirahisi tuu
Kwani kazi ni dezo au wajibu wa serikali kutoa ajira. Kazi sio zawadi wala shindano la kusema mnamtafuta mshindi. Ni uzembe tu unafanyika ila hamna nchi ilioendelea ambapo inaona fahari kuhenyesha watu wake katika ajira
 
Sioni ubaya wowote katika hili. Pesa zinazotokana na utalii zielekezwe kwenye elimu.

Hili litafanyika kwa muda mchache kwani hujasikia kodi za utalii ni nyingi na kubwa mpaka kufanya watalii wanaokuja kushindwa kurudi kwa mara ya pili?

Mimi sio ubaya watu kuchangia kiasi kidogo cha pesa kama ada ili kuifanya sekta ya elimu isiwe mzigo kwa sekta zingine.
 
Back
Top Bottom