hii ndio hoja. Serikali imekuwa bigwa Wa kuanzisha mwendo na si kuumaliza. Waamini Wa biblia wanajua kuwa heri mwisho mzuri kwenye ushuhuda. Matangazo yote mikwala n.k kumbe ni laki na nusu. Gharama za matangazo yanayofanyika nadhani yanazidi pesa zilizotolewa. Ni hvi unit cost ya mtoto mmoja wa private ya kawaida wanaolipa ada ya million 1.8 ni sawa na shule yangu yenye watoto 400 ya serikali. Kiuchumi bora umfundishe watoto kumi wanaolipa vizuri kulikon watoto 400 wasiolipa maana kuwabeba ni Mzigo. Tunashauri serikali isitumie neno la elimu bure waseme tunachanga nikuchangie ili hata wazazi na wanafunzi waone thaman ya elimu wanayoipataHizo laki mbili zimetoka hazitatolewa tena mpaka mwakani 2017
anayetakiwa afafanue ni aliyeleta hoja kuwa haitoshi, sio mimi, ukileta hoja ni lazima uweze kuwa na strong arguments kutetea hoja yako sio kuniuliza tena mimi maswali wakati nategemea maelezoFafanua hizo bil.18 na point kwa shule ngapi za Tanzania ukatae hiyo laki 2 kwa kila shule?
kaka umeeleweka pesa kiukweli haitoshi ndiyo maana hata ukiangalia kwenye michango ya chakula na pesa za wapishi, kununa mafuta, kuni, majia, chumvi na vingine shule nyingi zimweongoze sana gharama hiyo ukilinganisha na miaka mingine hivy lengo wanataka kufidia kwakua pesa hyo haitoshiMbona mnakuwa wakali sana kila anayehoji haya mambo!!?
Lengo ni kujadiliana na pengine kuishauri serikali namna bora ya kutekeleza hii sera ambayo kwa vyovyote vile ni nzuri na hakuna anayeipinga.
Na tukunbuke pia kuwa utekelezaji wake ndo tu umeanza na ni kitu kilichokuwa nje ya utaratibu wa kibajeti. Kwa hiyo ni lazima tu kutakuwa na mapungufu ya hapa na pale ktk utekelezaji wake!!
Binafsi nimemuelewa mleta hoja na
wewe pia nimekuelewa.
Ni kwamba hizi 18.6bn ni kwa ajili ya
shule zote za msingi na sekondari kwa
mwezi desemba, 2015.
Kwa mujibu wa magawanyo wa fedha
hizo ni kwamba;
Kwa sekondari kidato cha I -IV kila mwanafunzi atalipiwa na serikali
Tshs. 45,000 kama fidia ya ada ambayo ilipaswa kulipwa na mzazi wa mwanafunzi.
Kwa shule za msingi kila mwanafunzi atalipiwa na serikali Tshs. 10,000= kwa mwaka.
Kwa utaratibu wa serikali ni kwamba hizo fedha zitakuwa zinatolewa kila mwezi kwa kutumwa moja kwa moja ktk shule husika, hazitalipwa kwa mkupuo mmoja!!
Sasa kwa mfano kama shule ya sekondari X ina wanafunzi 145 kidato cha I - IV (nyingi ya shule za vijijini zina idadi ya wanafunzi inayo range kati ya 90 - 350) maana yake shule hii shule ktk mgawa wa mwezi desemba imepata;
45,000 ÷ 12 × 145 = Tshs. 543,750/=
Maana yake haya ndiyo matumizi ya shule hii kwa mwezi January, 2016 mara shule zitakapofunguliwa!!
Hii ndiyo hoja nadhani nilivyomuelewa mleta mada. Swali lake ni kwamba, hizi pesa zinatosha kuendesha shule kwa mwezi??
Mimi binafsi sina jibu ktk swali hili kwa sababu kila shule ina mahitaji na bajeti yake ya mwezi, muhula na kwa mwaka mzima. Ninachoweza kusema ni kuwa inategemea na shule.
Kwa sababu kuna shule zina wafanyakazi (casual labours) ambao hawako ktk payroll la serikali na hulipwa na shule kama walinzi, wahudumu wa ofisi nk kulingana na vyanzo vya mapato ya shule husika iwe ni kutoka EK au michango ya wazazi kwa wakati ule kabla ya sera ya elimu bure kuanza. Pia kuna shule zingine vijijini hazina walimu wa kutosha especially wa sayansi na shule huajiri parttime teachers ambao hulipwa posho ya kati ya Tshs. 150,000 hadi 250,000 ili wanafunzi hawa wafundishwe
Hii kitu ni halisi wala si kuandika tu hapa. Mimi hapa naandika nikiwa Shinyanga na natembea sana vijijini. Kuna shule za sekondari ziko kwenye very remote areas na mazingira ni magumu sana to the extent kwamba walimu hupakimbia huko kila wanapopangiwa. Kuna shule moja iko wilaya ya Kishapu inaitwa Paji ina wanafunzi 123 wa kidato cha 1 - 4 na walimu 5 wote wa masomo ya Arts na language hasa Kiswahili ns History, Geography na Civics. Hakuna mwalimu wa Mathematics, physics, Biology na Chemistry.
Anachofanya mwalimu mkuu alikuwa anatafuta vijana wa walionaliza kidato cha sita na kusaidia kufundisha. Na huwezi amini kuwa kila mwaka mwalimu huyu hupeleka vijana wawili au watatu kidato cha tano (A'level). Sasa serikali ime consider hii kitu??
Na kuna shule zingine wala hazina watu wa namna hii kwa sababu kama ni walinzi au muhudumu wa ofisi ama mtunza bustani wote wanalipwa na serikali. Kwa hiyo ni wazi, shule kama hii pesa kama hii inaweza kutosha tu kwa mwezi japo kwa kubanana sana!
Kwa hiyo hii 18.6bn ni nyingi kwa kutamkwa kwa pamoja lakini zikishagawanywa mashuleni, picha halisi ya kitakachokwenda ktk kila shule ni kama nilivyoonesha hapo juu na kwa hakika kuna shule zinaweza kupata hata Tshs. 150,000 tu kwa mwezi!!!
Dah! Kuna watu wanakurupuka sana. Sijui huyu mleta mada kaandika wakati amepakatwa au ameinama! Yaani nawaza tu wadau.
Umezidi kwa umbeya. Kama una uhakika na unachokisema kwa nini haureveal hiyo shule ili tujue?
Magufuli kawafunga midomo UKAWA. Wamebaki kuandika umbea tu humu mitandaoni. Unamaikia John Mnyika siku hizi? Wapi amefia Salum Mwalimu? Wapi Tundu Lissu? Wapi Freeman Mbowe? Wote wameufyata kwa kasi ya Magufuli. Wakijaribu kusema wanabaki kuwa kituko. Yule mzee wa kujinyea nyea eti alilalamika kuwa wafanyabiashara waliomsaidia kwenye kampeni wanasakamwa na serikali. Alipotakiwa kuwataja ameufyata. Wengine wanasema eti Magufuli anatekeleza ilani ya UKAWA. kwikwikwikwiiiii
Siku zote wachawi ni adui wa maendeleo. Wachawi kama huyu mleta mada hawastahili hata kuishi. Ni wale ambao kwa mikoa ya wenzetu wanaangamizwa huku wanajiona
Kakuambia wewe kama nani? Pole sana
Unataka nije kwenye field gani ilhali kila siku nashinda field?
Bilion 18 sio kwa kila shule ni kwa shule zote jumla hiyo,katika hiyo bil 18 toa bil 3 za.ada za mitihani like NECTAmkuu hiyo hesabu yako umeipigaje, maana zimetolewa bilioni 18 na point, wewe hiyo laki mbili umegawanyaje hadi kuipata?
Mtu ana zungumza Fact wewe unaleta ngojela hii ni hatali sana tena sana.Dah! Kuna watu wanakurupuka sana. Sijui huyu mleta mada kaandika wakati amepakatwa au ameinama! Yaani nawaza tu wadau.
Changa nikuchangie mbona ilikua programu nzuri tu,ilianza enzi za Mwinyi ndo mdau huo hata michango ya madawat ilianza nami nikaamua kwenda na meza yangu shulehii ndio hoja. Serikali imekuwa bigwa Wa kuanzisha mwendo na si kuumaliza. Waamini Wa biblia wanajua kuwa heri mwisho mzuri kwenye ushuhuda. Matangazo yote mikwala n.k kumbe ni laki na nusu. Gharama za matangazo yanayofanyika nadhani yanazidi pesa zilizotolewa. Ni hvi unit cost ya mtoto mmoja wa private ya kawaida wanaolipa ada ya million 1.8 ni sawa na shule yangu yenye watoto 400 ya serikali. Kiuchumi bora umfundishe watoto kumi wanaolipa vizuri kulikon watoto 400 wasiolipa maana kuwabeba ni Mzigo. Tunashauri serikali isitumie neno la elimu bure waseme tunachanga nikuchangie ili hata wazazi na wanafunzi waone thaman ya elimu wanayoipata
bilion 18 sio kila shule nafahamu hilo, ila inatolewa bilioni 18.6 kila mwezi na hakuna necta kila mwezi, mimi siungi mkono kama inatosha au haitoshi na serikali inapochemsha ni vizuri kuikosoa kwa nguvu, point yangu ni kuwa unapokuja kupost mada jamiiforums post kitu ulichokifafanua vizuri kwa facts& figures, ili uonekane una point, sio kusema vitu nusunusu, au vitu ulivyovifanyia utafiti nusu alafu unajifanya unajua fullBilion 18 sio kwa kila shule ni kwa shule zote jumla hiyo,katika hiyo bil 18 toa bil 3 za.ada za mitihani like NECTA
Taja jina la hiyo shule na mahali ilipo ,kama ni kweli itafanyiwa kazi hatupo kwenye zama za Jk za usanii sanii unaotuletea wwHvi kweli shule inapewa laki mbili hata kama ni kwa mwezi hapo hapo toa hela ya mlinzi,maji,umeme hapo bado Hela za chaki shule zitaendeshwa vp hizi!!!
Hapo kwenye mil 1 ya sekondari,zaid ya nusu huishia form IV hawaendeleo,nao wanaachwa hakuna.mwongozo waoIdadi ya shule za Primary ni 15,816 na idadi ya wanafunzi ni 8,419,305
Idadi ya shule za Secondary ni 4,266 na idadi ya wanafunzi ni 1,638,695., ukichukua hizo takwimu utagundua kitu kingine cha kusikitisha kuwa watoto wengi wanaishia katika Elimu ya msingi kitu ambacho si afya kwa taifa..