Kweli nimeamini ukimsifia mgema lazima tembo alitie maji, EFM sasa wamekuwa ni watu wa kutangaza singeri na jogingi kwa kuvipatia air time kubwa kuliko habari za michezo, sifa ni kitu kibaya sana.
Mojawapo ya vitu vilivyoifanya EFM iwe maarufu ni kuutangaza na kuupromote muziki wa Singeli...
Kusema kwamba EFM wanatangaza singeli na jogging muda wote unadanganya...
Kinachofanyika saaa hivi ni muendelezo wa ile misimu ya kutoa burudani na zawadi kwa wasikilizaji wao...
EFM wanayo matamasha kwa misimu tofauti....Kuna SHIKA NDINGA....KAPU LA EFM na sasa ni msimu wa MUZIKI MNENE ambao ulianzia Boko na wiki hii wapo Temeke....Vipindi kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa ni vilevile MAWIO..JOTO LA ASUBUHI...SPORTS HQ...UHONDO...LADHA 3600...UBAONI...E SPORTS....GENGE (hiki ndicho kipindi maalum kwa muziki wa singeli)...LULLABY na MPAKA KUCHEE...
Pia weekend wana vipindi kama E GOSPEL...LADHA TAMU...FUNGA MTAA(Muziki wa singeli)...AFRO POWER...BUSTANI YA WATOTO...MUDA WETU...MIX SUNDAY...OLD SKUL HIT...OLDS 80s...RDJ MIX na NGOMA REGGAE...
Kusema kwamba muda wote wanatangaza singeli na jogging sio kweli...
Katika huu msimu wa MUZIKI MNENE kila Jumatano wanakuwa na matangazo ya nje live (Kipindi cha Uhondo)..Alhamisi ni matangazo ya nje live (kipindi cha Sports Hq)...Ijumaa ni matangazo ya nje live(Joto la Asubuhi)...
Junamosi ni EFM jogging club...pia kunakuwa na bonanza(mechi za mpira wa miguu) ...Matukio ya kijamii(kufanya usafi Temeke Hosputal) na usiku ni mwendo wa burudani live kutoka kwa RDJs wa EFM na wasanii ambapo wikiend hii ni Temekeeeee...Pia kuna Singeli michano(mashindano ya kutafuta wasanii chipukizi wa Singeli)..Usiku mambo yote yatakuwa Buliaga Bar - Temeke..Dullah Makabila na Ruby watatoa burudani ya live..
Matangazo haya na burudani za bure za live za singeli zinaifanya EFM ipendwe sana...
Muziki unaongea....Amsha popo...
[HASHTAG]#TUNASEPANAKIJIJI[/HASHTAG]....