EFD: Mgomo wa wafanyabiashara Mwanza kuunga wa Dsm

EFD: Mgomo wa wafanyabiashara Mwanza kuunga wa Dsm

Niko Morogoro na huku maduka karibia yote yamefungwa nimezunguka nimeshindwa nunua kitu kabisa kila mahali yamefungwa

Leo asubuhi hapa jijini kuna mgomo wa kutofungua maduka yote hapa Mwanza na baadhi ya wafanya biashara wanadai kuwa watafunga kwa muda usio julikana.

Hili ni janga jingine kwa utawala huu wa Mafisadi , sasa kwa mtindo huu je uchumi wa Taifa unakuwa......?
 
Wafanyabiashara ningewaona wajanja kama wangekuwa wanaandamana ku ishinikiza serikali ili iwape hizo EFD bureee.Ila wao wanashinikizwa na wafanyabiashara wachache waliozoea kula hizi VAT ambazo wateja tunachajiwa badala ya kuzipeleka TRA.Ww mwananchi utakuwa mjinga ukimsupport mfanya biashara ambae anakuuzia bidhaa kwa bei ambayo ndani yake kuna VAT halafu ukilipia yy anazuia hela yote.EFD ndio dawa yao mm ni mmoja kati ya watu ambao huwa nazitaka sana hizi risiti za efd kwa sababu nimeshajiwekea kuliko nimuachie hiyo hela mfanyabiashara ni bora nikomalie risiti ili hela iende tuu serikalini.Wafanya biashara hawana lolote na wao ni mafisadi tuu ndio maana wanagomea hizi EFD ili waendelee kula kodi wanazotucharge kwenye bei za bidhaa zao badala ya kuzipeleka TRA.
 
Leo asubuhi hapa jijini kuna mgomo wa kutofungua maduka yote hapa Mwanza na baadhi ya wafanya biashara wanadai kuwa watafunga kwa muda usio julikana.

Hili ni janga jingine kwa utawala huu wa Mafisadi , sasa kwa mtindo huu je uchumi wa Taifa unakuwa......?

Siwezi kuwaunga mkono hawa wafanyibiashara wasiotaka kulipa kodi huku wakitegemea huduma nzuri kwa taifa lao.
 
Tatizo kubwa na la msing hapa ni zaidi ya Machine za EFD ni mfumo mzima wa kodi... Wafanyabiashara wana madai zaidi ya machine za EFD ambazo kwa sababu za makusudi serikali chini ya TRA ndio inachokishililia.. IKUMBUKWE Wafanyabiashara hawa ni walipa kodi wazuri wa kodi zao walizokuwa wanakadiliwa.

Madai ya wafanya biashara ni haya..

  1. Kwanza ni BEI ya machine ulikinganisha na BEI ya soko ya machine husika kwa soko la sehemu nyingine duniani.. kenya tu mashine zinapatikana kwa chininya TZS 350,000. ukienda china na kwingineko ni chini ya $80.
  2. Gharama kubwa na usumbufu unaotokana na machine hizo ukilinganisha na cash flow za mlengwa yaani mfanyabiashara anayeingiza 38,000 Kwa siku... Gharama za karatasi moja ni 6000 na gharama za maintenance ambazo ni zaidi ya laki 3 kwa mwaka na usumbufu wa kuripoti TRA NA KWA WAKALA kila machine inapoaharibika...
  3. Utaratibu wa faini kwa amabaye atashindwa kutumia machine hizo unatoa mwanya kwa wafanayakazi wasio waaminifu wa TRA( ambao ni wengi) na Askari waliozoea Rushwa kuleta taabu kwa wafanyabiashara.
  4. Machine za EFD hazionyeshi gharama za manunuzi na gharama za uwendeshaji ambapo hapo hasa ndio penye tatizo kubwa... Gharama nyingi za manaunuzi ama hazina risiti ama zina risiti ambazo hazilingani na gharama halisi... HILI LITAPELEKEA mfanyabiashara kutozwa kodi kubwa kuliko hanavyostahili kutokana na kukosekana na kumbukumbu za manunuzi.
  5. Mfumo mzima wa biashara ama zimetoka nje ya nchi ambazo ulipiwa kodi custom.. kodi ya import duty and VAT...Au zimenunuliwa kwa wakulima na wavuvi ama wafugaji ambao hawatoi risiti...Kwa zinazopita Customs ukadiliaji umekuwa shida kubwa... mzigo huo huo amabo haupishani hata miezi mitatu unaweza kuwa na kodi tofauti na tena yenye tofauti ya kutisha ... hii imeleta mianya ya rushwa kwa watumishi wa TRA na kupelekea wafanyabiashara kulipa malipo mengi yasiokuwa na risiti... amabayo yatakuja kumfanya alipe malipo mengi ya kodi ya mapato.
  6. Kodi zinazotozwa na TRA Customs hazinlingani na thamani halisi ya bidhaa zinazoingizwa na kushawishi wafanaya biashara kukubali kutoa rushwa ili angalau aweze kuuza bidhaa yake kwa gharama nafuu.
  7. kwa mazao yanaotka kwa wakulima mengi hayana risiti na kwa stahili hii mfanyabiashara atalazimaika kulipa zaidi kodi za mapato.
  8. Kwa ujumla mfumo mzima wa kodi unatakiwa kuangaliwa upwa ili uwe wazi na unaoshawishi wafanyabiashara kulipa kodi stahiki na kupunguza mianya ya Rushwa .... GHARAMA Nyingi za uendeshaji hazina risiti na hili ni tatizo la kuangalia ..
  9. Mfumo hauruhusu uingizaji wa mzigo wa pamoja ( sharing importation) ambapo kila mfanyabiashara aliyeshare container atalipa stahiki yake na mzigo wake kuwa na thamanai ya manaunuzi...
  10. kwa ujumla kufanya baishara Tanzania hasa kwa sekta zisizo rasmi zimekabiliwa na kodi nyingi zisizo na kichwa wa miguu... kodi za pango... kodi ya takataka.. kodi za fire... kodi za mabango... kodi za hamashauri... nk nk...

Tubadilike nchi ni yetu sote... sekta hii nayo ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa... iundwe tume maalumu ya kurekebisha mfumo mzima wa ulipaji kodi na kuwaka fair ness kwa pande zote.... na kusitisha zoezi la EFD

Muonamambo

A town
 
Back
Top Bottom