Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,217
- 25,989
acha wivu wa kike kila mtangaza nia amezidisha idadi coz sheria inaruhusu! mwenye wachache ana 650!
Nimeongelea kuona mbali, sijui kama umefikiria mbali. Wewe unadhani kwa jinsi Lowassa anavyotumia hili suala la udhamini wa watu 870,000 kujinadi, linawaweka wapi wagombea wengine wa CCM? Unfair playing ground. Huwezi kutambia kitu ambacho hakipaswi wala hakikuwa sehemu ya makubaliano ya utaratibu wa kutafuta mgombea. Hata kama alipata 870,000 kwa kuwa hukukuwa na zuio juu ya idadi kubwa, na kwenda mikoa 31 badala ya 15, alipaswa kukaa kimya sio kuanza ku-jipromote kwa namna anayotaka kuielezea jamii kwamba yeye ni bora zaidi ya wagombea wengine wa CCM kwa sababu alipata wadhamini 870,000 na kwenda mikoa 31.
Pia fikiria uteuzi ujao wa wagombea uchaguzi wa 2025. Kama Lowassa akipita kuwa Mwenyekiti wa CCM na Raisi kipindi hiki, basi kutauwa na ushindani mkubwa kwa wagombea wa CCM nao kutaka idadi kubwa na kwenda mikoa yote ya Tanzania, wakijua kwamba hicho ni kigezo muhimu kwa Lowassa. Fedha nyingi itabidi zitumike kwenye kutafuta udhamini, ambapo tayari unabagua wagombea wa CCM ili wawe wale tu wenye uwezo wa kifedha. Lowassa atakuwa ameweka "precedent" na sasa itakuwa ni vurugu tupu suala dogo tu la kutafuta wadhamini.
Kwani CCM waliposema angalau mikoa 15 hawakujua Tanzania ina mikoa zaidi ya 30? na waliposema wadhamini 450 hawakujua CCM ina wanachama zaidi ya milioni 4? Kwa ujumla, alichofanya Lowassa kinaonyesha wazi hana uwezo wa kufikiria mambo kwa umakini kabla ya kutenda.
Ninakata shauri kwamba Lowassa ni aina ya watu ambao wanadhani mtu akiwa na pua kubwa basi atatoa kamasi nyingi!