Edward Lowassa special thread

Edward Lowassa special thread

Unajua mie hadi sasa sijaelewa kama CCM walitoa maagizo ya wagombea kukusanya wadhamini wengi kadiri iwezekanavyo. Lowassa amekuwa akilitumia sana hili, na kuliweka mbele sana magazetini nk. Lakini najiuliza, ina mana wagombea wengine walishindwa kuonyesha wingi wa wadhamini wao au walichukua tu idadi inayotakiwa ya wadhamini kila mkoa, kulingana na maagizo ya CCM?

Nakumbuka Muhongo alipeleka DVD akaambiwa hazitakiwi kwenye kurudisha form za ugombea, sasa vipi Lowassa na hii 870,000?

Mie nadhani kwa jinsi Lowassa alivyotumia hili suala la wadhamini ni sababu mojawapo tosha ya kumwambia ana silka ya kukiuka utaratibu, na kwamba alikuwa akifanya kampeni badala ya kutafita wadhamini. Mwache akaangwe kwa mafuta yake mwenyewe. Maana kufanya kampeni kwa kutumia mgongo wa kutafuta wadhamini ni kutowatendea haki wagombea wengine wa CCM, has ukiangalia kwamba sasa anajinadi kwamba alipata wadhamini 870,000 tofauti na wagombea wengine wa CCM. Kwani CCM iliweka ushindani wa kuwa na idadi kubwa ya wadhamini kwa wagombea?

Huyu jamaa kweli mara nyingine haoni mbali juu ya athari za mambo anayofanya. Amekuwa so blinded na kutaka kuwa raisi kiasi kwamba yuko tayari kufanya lolote ili aupate. Kwani Ikulu kuna nini kwa mtu kama Lowassa?

Mtu mwenye obsession ya Ikulu namna hii ni wa kutilia shaka sana.

acha wivu wa kike kila mtangaza nia amezidisha idadi coz sheria inaruhusu! mwenye wachache ana 650!
 
Akipewa nchi atataka awe ncheo cha Ayaaa twalaaaah the supreme, ataandika katiba yake ili afanye anavyotaka
 
Mbwembwe zote wadhamini kiduchu hivyo, hama kweli hakika huyu atakiwi, kutumia bil 200 kuambulia wadhamini 870,000!!!

chadema 2010 ilipata kura million mbili na lowasa kapata wadhamini laki nane!! so wadhamini pekee anawazidi chadema nguvu

acheni wivu wa kike
 
Mbwembwe zote wadhamini kiduchu hivyo, hama kweli hakika huyu atakiwi, kutumia bil 200 kuambulia wadhamini 870,000!!!

mara oooh lowasa mwizi,mara ooo katumia 200b, kwa akili ya kawaida n mwendawazimu tu, halafu mtu anaeshindwa kujua wanachaa 870000 ni zaidi ya ailimia kumi ya wanachama wote,unategemea nini akiteulwa si atakomb a zote 100%
 
"chaguo la Mungu", ngoja nitafute namba ya Mzee Kilaini nimuulize. Labda kama wanaongelea 'mungu' mwingine lakini kama ni yule yule tuliyeambiwa na father, tafadhali tuwiane radhi!
 
"Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu"


Mmh, Susan, ni kweli hayo usemayo lakini? Kumbuka kuna suala la njia nyembamba na pana, na unajua ni ipi ina wengi zaidi - njia pana ya waliopotea. Pia kumbuka ni wengi waliotaka Barnabas aachiliwe badala ya Yesu. Sasa sijui unataka kutuambia nini Wakristo. Nadhani Lowassa ni Mkristo pia, anapaswa kukumbuka hilo. Siku zote njia yenye watu wengi ni ile ya waliopotea, masikini vipofu wasiojua wanakopelekwa lakini wakiwaamini wanaowaongoza bila kujua ni vipofu kama wao.
 
Hili ndio neno zito kweli ?????????????????????????????????.Siku ukisikia neno zito ualiitaje !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!.
 
acheni kukulupuka kama.chafya
kwan kowassa kupata wadhamini wote haoo na pia kumaliza mikoa yote sauti ya wengi ni sauti ya mungu na ambaliki mtu huyuu aende magogoni
 
Kama ameshindwa kuelewa maelekezo ya chama je katiba ya nchi itakuwaje, je siataendesha nchi kibabe

Apson kamaliza kazi baada ya kusaidia kumpoteza jamaa huyu kuogelea kwenye tope bila ya yeye kushtukia na sahivi anapeleka mafairi panahusika
 
Ukimtazama na kumsikiliza Edward Ngoyai Lowassa unaweza kunibishia. Ukimtazama na kumsikiliza tena Lowassa utaniamini. Ukimtazama na kumsikiliza Lowassa kwa mara ya tatu, hutatamani kumtazama na hata kumsikiliza mara nyingine. Ni msanii kwelikweli. Lowassa anajipambanua kama dawa ya umaskini wa Tanzania. Ameshindwa vibaya kuuondoa umaskini wa Monduli tu aliyoiongoza kwa miaka 25 kama Mbunge.
 
Unajua mie hadi sasa sijaelewa kama CCM walitoa maagizo ya wagombea kukusanya wadhamini wengi kadiri iwezekanavyo. Lowassa amekuwa akilitumia sana hili, na kuliweka mbele sana magazetini nk. Lakini najiuliza, ina mana wagombea wengine walishindwa kuonyesha wingi wa wadhamini wao au walichukua tu idadi inayotakiwa ya wadhamini kila mkoa, kulingana na maagizo ya CCM?

Nakumbuka Muhongo alipeleka DVD akaambiwa hazitakiwi kwenye kurudisha form za ugombea, sasa vipi Lowassa na hii 870,000?

Mie nadhani kwa jinsi Lowassa alivyotumia hili suala la wadhamini ni sababu mojawapo tosha ya kumwambia ana silka ya kukiuka utaratibu, na kwamba alikuwa akifanya kampeni badala ya kutafita wadhamini. Mwache akaangwe kwa mafuta yake mwenyewe. Maana kufanya kampeni kwa kutumia mgongo wa kutafuta wadhamini ni kutowatendea haki wagombea wengine wa CCM, has ukiangalia kwamba sasa anajinadi kwamba alipata wadhamini 870,000 tofauti na wagombea wengine wa CCM. Kwani CCM iliweka ushindani wa kuwa na idadi kubwa ya wadhamini kwa wagombea?

Huyu jamaa kweli mara nyingine haoni mbali juu ya athari za mambo anayofanya. Amekuwa so blinded na kutaka kuwa raisi kiasi kwamba yuko tayari kufanya lolote ili aupate. Kwani Ikulu kuna nini kwa mtu kama Lowassa?

Mtu mwenye obsession ya Ikulu namna hii ni wa kutilia shaka sana.
Siyo wa kumtilia shaka tu, bali ni wa kumwogopa kama Ukoma!
By Mwalimu Nyerere.
 
chadema 2010 ilipata kura million mbili na lowasa kapata wadhamini laki nane!! so wadhamini pekee anawazidi chadema nguvu

acheni wivu wa kike

Mkilala, mkiamka mnaiota Chadema tu. Sasa hapa Chadema inahusiana nini na hizo Sanaa za wadhamini? Mtasema yote mwaka huu.
 
Watanzania hatupo makini na ndio maana viongozi wanasaini mikataba yenye madudu,caption ya picha ina makosa,timu nzima imepitisha!!!
 
Back
Top Bottom