acha apitishwe tu hakuna namna
na wewe ulipewa?120.,000 x 25,000=3,000,000,000.
mamvi mwenyewe ni fisadi atawezaje kukemea mafisadi wenzake
Mamvi anahangaika bure uraisi ataishia kuusikilizia kwenye radio
Heshima sana wanajamvi.
Katika harakati za kusaka wadhamini team Lowassa Ndossy iliandaa maandamano ya Piki piki kutoka uwanja wa ndege wa KIA hadi Arusha mjini.Duru za kiusalama zililazimika kuzuia piki piki zote maeneo ya KIA hadi King'ori ili kuepusha msongamano wa magari usiokuwa wa lazima.
Taarifa zaidi zinadai kila Boda boda ililipwa Tsh 60,000/=@ na mafuta lita 10 kwaajili ya kufanikisha zoezi hilo.
Waendesha boda boda tayari walishalipwa fedha zao ili kuepusha madai ambayo wakati mwingine yanasababisha kuichafua kambi ya Edward Lowassa Ndossy.
Tayari kambi hiyo wanajindaa kudai kiasi cha fedha kwakuwa kazi iliyokusudiwa haikufanyika hata kwa 5%.
Zoezi la utoaji taarifa lilifanyika katika uwanja wa Msikiti Mkuu wa Bondeni ambao pia ulitumika kuchangisha fedha kwaajili ya ujenzi wa nyumba za msikiti.
Waislam wengi walisikika wakilalamika kwasababu shughuli hiyo ilisababisha usumbufu wakati wa swala ya adhuhuri kwakuwa wahudhuriaji walikuwa wakipiga makelele na waandaaji wa shughuli walitumia vyombo vyenye sauti kubwa.
Nawasilisha.
Kwa wadhamini hao mbona Lema angepigwa chini asubuhi mapema.
tafta handaki la kujifichia kabla chaguo la Mungu halijakukuta
Mkuu nyie kama wanaccm mnamtaka nani awe rais??
Yaani wee Acha tu, kasomba Arusha yotee... Arusha town itahamia CCM bila shaka kabisa, kama mwendo ni huu, CDM watakiona cha mtema kuni..!!!
Lowassa ni Mwamba, na juu ya Mwamba huo Mungu kaamua kujenga nyumba yake...Hakika EL ni chaguo la watanzania wengi, chaguo la Mungu wa mbinguni...!!
Mkuu nyie kama wanaccm mnamtaka nani awe rais??
mwiba uliopo ingia ndipo utapotokea .Huyo emma ni CDM... anahangaika sana kumchafua EL, CDM kakosa wanaume, anakuja tafuta wanaume CCM, bahati mbaya CCM hatuli makombo...!!
Alafu wewe!! hivi kwa nini ni MJINGA sana??Wana CCM wengi wamerudi kwa Lowassa, baada ya kuwa na matumaini nae... so CC Arusha ingawa ni ngome ya CDM, ila wameapa, Urais ni EL tu... hawasikii, hawaoni, hawaelewi..hawaangalii chama, wanaangalia mtu...!!!
Arusha, siasa zimewaaingia haswa... wenyewe waangalia mtu, sio chama..!!!
Pesa ina nguvu za ajabu
Sasa mkuu tujuze wamesha mkata?