Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 21,179
- 37,475
Edward Lowassa Ngoyai Ndossy amepata wadhamini 120,338.Kanuni na taratibu za CCM ni wadhamini 450 tu ukiongeza wengine chama hakiwatambui.Kanuni hizo zina kwenda mbali zaidi kwamba mwanachama haruhusiwi kudhamini zaidi ya mtu mmoja.Kitendo cha Ndossy Lowassa kina kwenda kinyume na utaratibu wa chama kwakuwa ikitokezea wagombea watatu au wanne wakakiuka utaratibu wa chama kama Lowassa maana yake watia nia wengine watakosa wadhamini.Mkoa wa Arusha una wanachama hai wasiozidi elfu hamsini utashangaa idadi ya wadhamini waliomdhami Lowassa imetoka wapi kama si wanachama wa kununua kadi fast fasta.