Fake Lowassa
New Member
- Jun 5, 2011
- 3
- 13
Ndugu zangu,
Sikutaka kabisa kushiriki katika hii mitandao ya kijamii ambayo mimi niliiona kama ni ya kihuni, lakini nimegundua kwamba kuna vitu vya msingi sana ambavyo huwa vinajadiliwa humu na hii imenifanya niamue kushirikii.
Nimesoma michango yenu mingi sana humu, kimsingi michango mingi imejaa chuki dhidi yangu na wenzangu, huwa nashindwa kuelewa sababu hasa ya kunichukia kiasi hiki. Sitaki Malumbano na yeyote, lakini sipendi pia muendelee kuendesha propaganda za kunichafua.
Kuna watu ambao watahakikisha napotea kisiasa, sijui ni kwa maslahi ya nani, najua sababu ni kwamba na wala sijisifu, mimi ni kati ya watu ambao pamoja na matatizo ya kibinadamu niliyonayo, nina uwezo mkubwa wa kuliongoza taifa hili na hii inanifanya nionekane tishio kwa wale wote ambao wanataka kuliongoza hili taifa. Mimi sina nia ya kuwa rais wa Tanzania kwa vyovyote vile lakini ningependa kuwaongoza watanzania iwapo wananchi wangependa iwe hivyo.
Kuhusu hizi shutuma ninazopewa, nadhani ni uonevu tu kwa kuwa hakuna hata mmoja wa wale wanaonishutumu ambaye ana ushahidi wa moja kwa moja kwamba mimi nilishiriki katika kuihujumu nchi, na kwa uzalendo wangu niliamua kuuacha uwaziri mkuu, sijui watanzania wanataka nifanye nini. Najua kama binadamu nina mapungufu yangu na kila mtu anayo lakini hiki kisiwe kigezo cha kuyaacha mazuri yote niliyoifanyia nchi hii na kunisakama, kunitushi na kunidhalilisha kwa kila njia.
Naomba watanzania mnielewe kuhusu Richmond nilifanya kwa nia njema lakini bahati mbaya na kwa makosa ya kibinadamu kampuni ile ikawa feki, ni nilikubali kubeba lawama kwa kujiuzulu. Watanzania kosa langu ni nini hasa? Nihukumuni kwa haki tafadhali sio kwa propaganda.
Ya CCM na dhana ya kuendelea kuchafuana ya magamba nitaileza siku nyingine. Naomba leo niishie hapa, nitaendelea kueleza ukweli wangu popote nitakapopata fursa ikiwa ni pamoja na kupitia mitandao hii ya kijamii.
Sikutaka kabisa kushiriki katika hii mitandao ya kijamii ambayo mimi niliiona kama ni ya kihuni, lakini nimegundua kwamba kuna vitu vya msingi sana ambavyo huwa vinajadiliwa humu na hii imenifanya niamue kushirikii.
Nimesoma michango yenu mingi sana humu, kimsingi michango mingi imejaa chuki dhidi yangu na wenzangu, huwa nashindwa kuelewa sababu hasa ya kunichukia kiasi hiki. Sitaki Malumbano na yeyote, lakini sipendi pia muendelee kuendesha propaganda za kunichafua.
Kuna watu ambao watahakikisha napotea kisiasa, sijui ni kwa maslahi ya nani, najua sababu ni kwamba na wala sijisifu, mimi ni kati ya watu ambao pamoja na matatizo ya kibinadamu niliyonayo, nina uwezo mkubwa wa kuliongoza taifa hili na hii inanifanya nionekane tishio kwa wale wote ambao wanataka kuliongoza hili taifa. Mimi sina nia ya kuwa rais wa Tanzania kwa vyovyote vile lakini ningependa kuwaongoza watanzania iwapo wananchi wangependa iwe hivyo.
Kuhusu hizi shutuma ninazopewa, nadhani ni uonevu tu kwa kuwa hakuna hata mmoja wa wale wanaonishutumu ambaye ana ushahidi wa moja kwa moja kwamba mimi nilishiriki katika kuihujumu nchi, na kwa uzalendo wangu niliamua kuuacha uwaziri mkuu, sijui watanzania wanataka nifanye nini. Najua kama binadamu nina mapungufu yangu na kila mtu anayo lakini hiki kisiwe kigezo cha kuyaacha mazuri yote niliyoifanyia nchi hii na kunisakama, kunitushi na kunidhalilisha kwa kila njia.
Naomba watanzania mnielewe kuhusu Richmond nilifanya kwa nia njema lakini bahati mbaya na kwa makosa ya kibinadamu kampuni ile ikawa feki, ni nilikubali kubeba lawama kwa kujiuzulu. Watanzania kosa langu ni nini hasa? Nihukumuni kwa haki tafadhali sio kwa propaganda.
Ya CCM na dhana ya kuendelea kuchafuana ya magamba nitaileza siku nyingine. Naomba leo niishie hapa, nitaendelea kueleza ukweli wangu popote nitakapopata fursa ikiwa ni pamoja na kupitia mitandao hii ya kijamii.