Raia ni wagumu sana kufanya maamuzi ya kumfurusha raisi kwasababu Huwa wanaliogopa jeshi ambalo linamiliki silaha na ambalo linaonekana kuwatii viongozi.
Ila kama raia wamebariki mapinduzi yanini Sasa ECOWAS kutaka kupeleka jeshi. Kitu kinachoonekana sio Cha busara sana ni jeshi la Niger kukataa mazungumzo ila pia huwenda wanaijua ECOWAS vizuri kuliko sisi na ndo maana hawataki mazungumzo nao.
Kama raia wamebariki jeshi kupindua utawala ambao ulikua unaonekana kama mti mkavu kwao basi Mungu AWABARIKI wafanye taratibu zao vizuri waweke utawala WA kiraia ambao unajua raia wanataka Nini na Jeshi lirudi mahala pake huku moyo wao ukiwa juu ya kuwalinda zaidi raia