The Economic Freedom Fighters Tanzania. (EFF)
Tunaendelea kuhusu vuguvugu la kiasiasa la Mapinduzi ya kiuchumi.
Vuguvugu hili limeanzishwa rasmi tarehe 24 May 2023, ni vuguvugu la kisiasa lenye mtazamo wa kimataifa ( International Outlook). Vuguvugu hili ni sauti ya watu maskini na fukara, wanyonge ambao wako tayari kusimamia rasilimali zao kwa maslahi yao wenyewe na vizazi vyao.
Vuguvugu hili la kisiasa linafuata siasa kali ya Mlengo wa shoto, falsafa na itikadi yake ni nyenzo ya jamii yenyewe kujikomboa kiuchumi na hasa jamii ambayo imekuwa chini ya matabaka ya kinyonyaji.
ITIKADI
Vuguvugu hili la kisiasa linaamini katika Ujamaa na kwa Umoja wetu tunasema "Ujamaa ni Imani" Jamii nyingi ya Watanzania (Afrika) imeendelea kuishi misingi ya Ujamaa licha ya msukumo mkubwa sana wa kiuchumi kutoka nje ya Tanzania ( Afrika) katika mazingira ya kuamuliwa namna ya kuishi na kuzalisha mali kwa Jamii yetu. Kwa mtazamo wetu Ujamaa bado ni nyenzo na itikadi imara ya kupambana na umaskini, matabaka au kiwango kikubwa cha umaskini kwa watu wetu. Hatuna budi kuunganisha jamii yetu ili kwa pamoja ishiriki katika maendeleo yake yenyewe bila kupangiwa na mifumo ya kinyonyaji ya wageni. Ujamaa ni Alama ya Ukombozi wa kiuchumi kuwatoa watu kwenye ufakara kwa kutumia rasilimali zao wenyewe, kusimamia mambo yao ya kiuchumi, kisiasa na Kitamaduni ikiwa Pamoja na sayansi na teknolojia iliyobuniwa na jamii yenye Uhuru kamili wa kiuchumi .
FALSAFA
Nguvu na Kazi. Falsafa hii ni muhimu ili kuumba kizazi chenye kutumia nguvu ya ziada ili kujikomboa kiuchumi kutoka mikononi mwa wanyonyaji na wote wasiyotaka tujikomboe kiuchumi. Kizazi kinachofanya kazi kwa bidii, kuzalisha mali kwa bidii kwa ushiriki wenyewe katika kukuza uchumi wao na kusimamia rasilimali zao wenyewe ili ziwanufaishe. Jamii isiyo fanya kazi kwa bidii utawaliwa na wageni na ambao uleta mitaji na faida ya mitaji hiyo upelekwa kwa wageni wakati huo Jamii inayomiliki rasilimali ubakia maskini na fukara kwa kwakukabidhi urithi wao kwa vizazi vya wageni.
Imani yetu ni madhubuti katika kukoleza moto na hamu ya Ukombozi wa kiuchumi, kubuni njia mbadala za kupambana na wanyonyaji na mifumo Kandamizi dhidi ya jamii yetu yenye kutumwa na kuamuliwa namna ya kutumia rasilimali zake. Uwezo wetu ni kusimamia rasilimali zetu kutumika kwa ajili ya jamii yetu inayoishi chini ya mstari wa umaskini.
Je tupo tayari kwa ajili ya Vuguvugu hili la Ukombozi wa Kiuchumi?
Ujamaa ni Imani.
View attachment 2716069