Bad c&pKile chama cha MALEMA kimeanzisha tawi lake Bongo.
Bad c&pKile chama cha MALEMA kimeanzisha tawi lake Bongo.
Hili ni jambo jema sana. Hata hivyo, hili lilipaswa kuwa kwenye jukwaa la "Biashara, Uchumi na Ujasiriamali.The Economic Freedom Fighters Tanzania.
Leo tunaangalia maana ya Nembo ya Vuguvugu la The Economic Freedom Fighters Tanzania. (EFF)
Na maana ya Rangi kuu nne na moja ya ziada inayopampa bendera yetu.
Kumbuka vuguvugu hili ni la kisiasa linaloegemea siasa za Mlengo mkali wa shoto na kufuata Itikadi ya Ujamaa, falsafa ya Nguvu na kazi na sera za Kiuchumi zinalenga Ukombozi wa kiuchumi zinazoegemea kwenye itikadi ya Kijamaa (Modern Socialism Economic policies) halifungamani na upande wowote wa kisiasa na aliegemei popote lakini msingi wake wa kiitikadi ni wa Kijamaa bila kuathili utamaduni wa Tanzania na Sheria zinaiongoza.
Kuasisiwa kwa vuguvugu hili ni uthubutu wetu kuakikisha Ukombozi kamili wa Tanzania kiuchumi kutoka kwa wanyonyaji na vibaraka wao hapa Tanzania, malengo ya kimataifa yametajwa katika mada za juu na malengo ya Kitaifa ambayo yanatuleta pamoja kama wanamapinduzi wa kiuchumi yatakujia kwa kadri ya maitaji na muda wa kuwafikia nyie nyote.
Vuguvugu hili limeasisiwa kwa misingi ya Nidhamu, tunaamini kuwa wanamapinduzi sharti wawe na Nidhamu ili kufikia itaji letu la kuwakilisha watu wa aina zote, tunaamini pia siasa bila ukombozi kamili wa kiuchumi ni batili na Uongozi ni huduma kwa Wananchi na hivyo kujinufaisha kama kiongozi ni batili pia.
Maana ya Nembo yetu.
Mosi, Nyota za dhahabu 54 zinazoizunguka Ramani ya Afrika zinamaanisha Mataifa 54 ya Afrika ambayo yanaitaji kuungana na kuunda Taifa moja kubwa kiuchumi, Kitamaduni, Kijeshi, Kitaasisi, kisayansi na Kitechnolojia (THE UNITED REPUBLICS OF AFRICA) Hii siyo ndoto yetu peke yetu kama The Economic Freedom Fighters Tanzania (EFF) ni hitaji letu sote tangu kuasisiwa kwa Uhuru wa Kisiasa wa Afrika na kizazi chetu kina jukumu la kuasisi Mapinduzi ya kiuchumi na kuyaleta pamoja Mataifa yote 54, bila kusahau Mataifa mawili kama Somaliland na Sahara Magharibi ambayo tunayatambua kama Mataifa huru.
Nyota za dhahabu 54 pia inawakilisha mshikamano wa kimataifa na maendeleo endelevu ya Afrika katika Mapinduzi na Ukombozi kamili wa Afrika kiuchumi na watu wote waliyo chini ya mifumo hodhi kiuchumi ambayo inawaacha wengi kwenye umaskini na ufakara Duniani kote.
Pili, Nembo yetu ina Ramani ya Afrika inayowakilisha nguvu na Uthubutu wa watu wake, Rasilimali na UTU, Ramani imekolezwa kwa rangi ya kijani ikimaanisha Ardhi yake inayotakiwa kutumika kwa ufanisi ili kuwatajirisha watu wenyewe.
Tatu, Ndani ya Ramani kuna mwenge unaowakilisha Umoja na Uhuru kamili wa kiuchumi kwa Watanzania (Afrika) na hasa wale wote waliyoachwa katika mfumo wa kiuchumi kandamizi na wa kinyonyaji. Mwenge huu unamlika kila aina ya maovu, kama Rushwa na ufisadi, Matumizi mabaya ya rasilimali na kuwamlika viongozi wababaifu wa kisiasa. Kwetu Mwenge huu ni gao madhubuti ya maendeleo endelevu ya Tanzania (Afrika).
Rangi kuu nne za Bendera yetu ni Kijani, Nyekundu, Njano na nyeusi.
Kijani, Nyekundu na Njano ni rangi za Umajumuhi wa Afrika ( Pan African color's)
Na Nyeusi, inatuwakilisha sisi wenyewe watu weusi Duniani kote.
Nyeupe, pia ni miongoni mwa rangi zisizoonekana kwenye Nembo yetu nayo inawakilisha makundi maalumu na kutumika pale itakapolazimika kutumika.
"Ujamaa ni Imani"View attachment 2722799
Economic Freedom Fighters Tanzania (EFF)
MALENGO MAKUU YA VUGUVUGU LA (EFF)
1. Kuuanganisha Watu weusi Duniani kote katika harakati za kujikomboa kiuchumi. (International Outlook)
Kujikomboa kiuchumi ni nyenzo muhimu ya kulinda UTU wa watu weusi ambao tumefanywa daraja la tatu tangu kuumbwa kwa Dunia, pamoja na nguvu ya watu weusi (Black Supremacy) lakini tumeshindwa kutumia nguvu hii kushinda ubepari na Ubeberu mamboleo.
Afrika ni bara changa na Tanzania ni Nchi changa kiuchumi, lakini tajiri kwa rasilimali zake na utamaduni, namna pekee ya kuitumia nguvu hii ni kujikomboa kiuchumi na The Economic Freedom Fighters Tanzania (EFF), tuko tayari kuungana na yeyote anayeifikiria Tanzania miaka 100 mpaka 200 ijayo. Uthubutu wetu ni kuandaa kizazi cha mapinduzi ya Kiuchumi hapa Tanzania na kutumia rasilimali zetu kwa maslahi ya Watanzania wenyewe.
2. Kuunda na kuweka misingi ya Umoja wa Mataifa ya Afrika (THE UNITED REPUBLICS OF AFRICA).
Ili tuwe na nguvu ya kiuchumi na kujikomboa kiuchumi lazima tuungane kama Afrika na kuwa Taifa moja lenye Jeshi moja, Rais mmoja, Bank kuu Moja, Sarafu moja na dhamira thabiti ya kuunda THE UNITED REPUBLICS OF AFRICA.
Wazo la Muungano wa Mataifa ya Afrika (THE UNITED REPUBLICS OF AFRICA) limekuwepo tangu kuasisiwa kwa Ukombozi wa kisiasa na viongozi wetu kama Mwalimu Julias Nyerere na Kwame Nkrumah.
Haya ni malengo makuu ya The Economic Freedom Fighters Tanzania (EFF) kwa maana ya mtazamo wa kimataifa na mtazamo wa Kitaifa ni dhabiti ya taasisi hii kukuwajulisha Wananchi kadri ya uwezo wetu wa kuwafikia
Vuguvugu hili ni sehemu ya sauti ya wananchi wanyonge na maskini wa Tanzania na Afrika, sauti hii haipo kwa ajili ya Mabepari na Mabeberu, kama tulivyosema vuguvugu hili linafuata Itikadi ya Ujamaa inayooegemea Mlengo mkali wa kushoto.
Tupo tayari kwa gharama kwa ajili ya Mapinduzi ya Ukombozi wa Kiuchumi Tanzania.
"Ujamaa ni Imani"View attachment 2720077
Ujamaa ni umasikiniSalaam,
Huu utakuwa ukurasa rasmi wa Vuguvugu la Kimapinduzi la Ukombozi wa Kiuchumi Tanzania, amboa utakuhabarisha kuhusu Itikadi, falsafa, sera, utangamano, dira ya Economic Freedom Fighters Tanzania, maoni, mtazamo na mambo mengi ya kisiasa, Kiuchumi, kijamii, Sayansi na teknolojia na Uhuru kamili wa kiuchumi wa Afrika.
Vuguvugu (movement) alichangamani na upande wowote wa kisiasa, bali linalenga kuhamasisha nguvu ya mtu mweusi na wote wasiyo na sauti Duniani kote kujikomboa kiuchumi.
Vuguvugu hili linapinga ubaguzi wa aina yoyote ile ikiwa ni pamoja na makundi maalumu ya kijamii ndani na nje ya Nchi.
Karibu sana Watanzania wote.
Economic Freedom Fighters Tanzania,
Ujamaa ni Imani.View attachment 2695905
Halina usajili ni kama Pan-African kwa sasa. Tunaomba maoni yako ushauri wako.Limesajiliwa ? Au ni kama PAN AFRICA ?
Woooow, Eff karibuni Tanzania , sikujua Kama mko TanzaniaEconomic Freedom Fighters Tanzania
(EFF)
Toa maoni na ushauri wako juu ya Vuguvugu hili la kisiasa ambalo halina Mlengo wa chama chochote wala hakihusiana na serikali.
Hili ni vuguvugu la Kimapinduzi la Ukombozi kamili wa kiuchumi Tanzania, Afrika na kwa wale wote wanaoonewa kiuchumi Duniani kote.
Tupe ushauri wako na maoni yako wazi ua kwa siri DM.
KUMBUKA HIKI SIYO CHAMA CHA SIASA.
The Economic Freedom Fighters Tanzania (EFF)Woooow, Eff karibuni Tanzania , sikujua Kama mko Tanzania
Ahsante sana, tunaomba maoni yako na ushauri wako.Karibu Tanzania , EFF
Naelewa hii Wing yenu naifahamu nadhani Mara ya Mwisho alikuwa anaiongoza Goodrich GardeeThe Economic Freedom Fighters Tanzania (EFF)
Ipo hapa Tanzania, kumbuka siyo chama cha siasa.
Karibu sana na tunashukuru sana.EFF Mimi ni Supporter wenu mkubwa nafatilia kila Jambo Ila Ile ya kuunga mkono ushoga hapana na mtapoteza Sana vijana wa Afrika
Shida ni nchi zetu za Afrika kutunga Sheria za kutugawa, tulitakiwa tuwe na sheria inayomuhusu vijana wa Africa kujumuika pamoja kiitikadi. EFF fit to serve as a machinery that could put African Youth together with common interests and Common AgendaHalina usajili ni kama Pan-African kwa sasa. Tunaomba maoni yako ushauri wako.
It's non governmental and non profit Organization.
Maoni yangu yanafungwa na mipaka ya kisheria ya kila nchi Ila mtafiti sheria gani za Kimataifa zinaweza kutumika kufanya tujumuike pamoja kwa Uhuru, for me I wish Eff iwe Tz Kama ilivyo SA.Ahsante sana, tunaomba maoni yako na ushauri wako.
Hili ni vuguvugu la Kimapinduzi la Ukombozi wa Kiuchumi.
The official Platform for The Economic Freedom Fighters to champion radical Economic policies in Tanzania. It's for fearless Fighters only. View attachment 2781667