TzPride
JF-Expert Member
- Nov 2, 2006
- 2,616
- 1,167
Ndugu zangu wanajambo ninafuraha sana maana sasa watanzania wanaweka msimamo mzuri. Mijadala ya EAF sasa wabongo wengi wana kataa "fast tracking". Kweli wengi tunashindwa kuelewa nini hasa sababu ya fast tracking...ni kama unahamu na mtoto na kwa kuwa mkeo ni mjamzito basi unaharakisha afanyiwe operesheni kabla ya mda wa kuzaa hujafika ili wewe upate mtoto..je, hapo utapata mtoto au unataka mkosa?
Wabunge walijadili vizuri sana jambo hili mbele ya kamati ya Wangwe, wengi walitaka waambiwe kwa nini tuharakishe?
Cha kusikitisha ni kwamba leo nimeona taarifa kwenye chombo kimoja cha habari kuhusu serikali ikijibu maoni ya wabunge kwa kusema hayo maoni ni yao tu sio ya watu wanaowawakilisha. Siamini serikali yetu inataka tutumbukiza kwa nguvu EAF. Kama ni hivyo basi awamu hii ndo itakuwa awamu mbovu kuliko zote na historia itaihukumu.
Sitaki kupoteza Utanzania kwani hata Utanganyika uliniponyoka bila ridhaa yangu.
Wabunge walijadili vizuri sana jambo hili mbele ya kamati ya Wangwe, wengi walitaka waambiwe kwa nini tuharakishe?
Cha kusikitisha ni kwamba leo nimeona taarifa kwenye chombo kimoja cha habari kuhusu serikali ikijibu maoni ya wabunge kwa kusema hayo maoni ni yao tu sio ya watu wanaowawakilisha. Siamini serikali yetu inataka tutumbukiza kwa nguvu EAF. Kama ni hivyo basi awamu hii ndo itakuwa awamu mbovu kuliko zote na historia itaihukumu.
Sitaki kupoteza Utanzania kwani hata Utanganyika uliniponyoka bila ridhaa yangu.