EA ecosystems law hits snag

Binafsi yangu kutokana na experience niloiona ktk nchi hizi sidhani kama Jumuiya ya EA inaweza kutusaidia badala ya kutuongezea matatizo pande zote. Tazama jinsi Jokakuu na Wakenya wanavyopelekana na hhata kutuhumiana ktk maswala na misimamo tofauti ya nchi hizi. Tazama migogoro tulonayo na Zanzibar badala ya kwenda mbele miaka yote tumekuwa na uhasama fulani ndani wakati wanaofaidika na Muungano huu ni Wazanzibar zaidi ya bara. Rwanda na Burundi wao wanataka ardhi zaidi maana nchi zao ndogo na umoja huu una faida kubwa kwao.

Kenya wamejijenga ktk viwanda na mteja wao mkubwa ni Tanzania na wakiweza kuongeza wigo la ku supply nchi nyingine tano zaidi watajiboresha zaidi kiuchumi. Binafsi yangu naamini kabisa Uchumi wa nchi kama Ureno, Spain na Greece umekufa kwa sababu walikuwa tegemezi wa nchi kama Uingereza, France na Germany ambao wali ongeza wigo la soko la mali zao. Na kifo cha nchi hizi kiucxhumi inaondoa soko lao pia hivyo wako tayari kutumia kiasi chochote cha fedha kuhakikisha uchumi za ya nchi hizi una boreka kwa lengo la kuhifadhi soko lao wakati nchi hizi zinaendelea kuwa wahitaji wa mali za nchi za Germany, Uingereza na Ufaransa, sasa wanasogea zaidi kwa nchi zilizokuwa ktk Russian federation.

Swala la kujiuliza sisi na hii EAC tutafaidika vipi na jumuiya hii iwe kuuza mazao yetu, usafiri au communication au chochote na tunachukua nguvu gani kuimarisha miradi hiyo maana vitu vyote hivi sisi tuko nyuma sana na bado ni wahitaji na sii wazalishaji. Na je Wabunge wetu wanaelewa fika wanatakiwa kusimamia mambo gani ambayo ndio nguzo ya tanzania kujiunga na EAC kama hatuna isipokuwa kufuata mkumbo kwa sababu ya mahitaji yetu wenzetu wakiwa supplier basi tumekwisha. Utaweza vipi kujenga kiwanda cha maziwa ikiwa Kenya wanaweza ku supply kwa bei nafuu na kutosheleza! - Ndio tutalijenga Taifa tegemezi hivyo.

Mkandara,

..hii jumuiya imegeuka kuwa kama utapeli vile.

..wananchi waliambiwa tunaungana ili tuweze kukabili ushindani wa kiuchumi na kibiashara dhidi ya mataifa ya nje.

..kinachotokea on the ground ni nchi wanachama wa EAC kukanyagana, kuhujumiana, na kushindana wenyewe kwa wenyewe.

..nakubaliana na wewe kwamba Tanzania tumekuwa soko la bidhaa za Kenya kwa muda mrefu sasa. Tunachotakiwa kujiuliza ni hali hiyo itaendelea kwa muda gani? What r we doing ili na sisi tuweze kuuza bidhaa za viwandani Kenya, Uganda, na kwingineko?

..wa-Tanzania hawataki UTUMWA na UKOLONI ndani ya East African community. Wako wenzetu ambao wanadhani wao wana haki juu ya wengine ndani ya jumuiya hii.




..
 
Safi Mkandara........Nitatafuta hoja za Uhispania Ureno na Italia halafu nitarudi
 
Safi Mkandara........Nitatafuta hoja za Uhispania Ureno na Italia halafu nitarudi
Karibu sana nakuomba tu zisome kutoka kwa wataalam na wenyeji wa nchi hizo na sii IMF au world bank wanavyosema maana nimekupa reality on the ground.
 
Mkandara,

..hii jumuiya imegeuka kuwa kama utapeli vile.

..wananchi waliambiwa tunaungana ili tuweze kukabili ushindani wa kiuchumi na kibiashara dhidi ya mataifa ya nje.

..kinachotokea on the ground ni nchi wanachama wa EAC kukanyagana, kuhujumiana, na kushindana wenyewe kwa wenyewe.

..nakubaliana na wewe kwamba Tanzania tumekuwa soko la bidhaa za Kenya kwa muda mrefu sasa. Tunachotakiwa kujiuliza ni hali hiyo itaendelea kwa muda gani? What r we doing ili na sisi tuweze kuuza bidhaa za viwandani Kenya, Uganda, na kwingineko?

..wa-Tanzania hawataki UTUMWA na UKOLONI ndani ya East African community. Wako wenzetu ambao wanadhani wao wana haki juu ya wengine ndani ya jumuiya hii.




..

Kususia EAC ina maana kuwa TZ haiko tayari kushirikiana na mataifa mengine katika ngazi za juu za uongozi. Kiuchumi/biashara kati ya nchi hizi tatu za EAC imeongezeka sana baada soko la euro kupata pigo. Na hii ni ishara tosha kuwa lazima soko zipanuke EA.. Lazima intra-border trade EAC iweze kutiliwa maanani na si mzaha tena...Uchumi za Euro zimekufa na haziwezi faidi EAC.

Hatuwezi tegemea Ulaya tena kwa hizi factors nilizozungumzia hapa juu. Je ni nini munafanya hasa EAC kuhakikisha viwanda vinanawiri...sio ndani ya kenya pekee yake hata Sudan Kusini, kule Uganda, kule Rwanda...EAC sio tu kuhusu kenya..Kuna mataifa kama manne.
 
Kususia EAC ina maana kuwa TZ haiko tayari kushirikiana na mataifa mengine katika ngazi za juu za uongozi. Kiuchumi/biashara kati ya nchi hizi tatu za EAC imeongezeka sana baada soko la euro kupata pigo. Na hii ni ishara tosha kuwa lazima soko zipanuke EA.. Lazima intra-border trade EAC iweze kutiliwa maanani na si mzaha tena...Uchumi za Euro zimekufa na haziwezi faidi EAC.

Hatuwezi tegemea Ulaya tena kwa hizi factors nilizozungumzia hapa juu. Je ni nini munafanya hasa EAC kuhakikisha viwanda vinanawiri...sio ndani ya kenya pekee yake hata Sudan Kusini, kule Uganda, kule Rwanda...EAC sio tu kuhusu kenya..Kuna mataifa kama manne.

Kabaridi,

..tatizo ni kwamba Kenya mmeigeuza Tanzania kuwa ndiyo East Africa. Tanzania isipokubali jambo lolote lile basi mnaanza negative attacks and things come to a grind. Mfano ni suala la ardhi na free movement of labor. Kwanini Kenya,Somalia,Ethiopia,Uganda. etc msiendelee na masuala hayo na kama Tanzania itavutiwa in the future itaomba kujiunga?? Kwanini spend all this time attacking Tanzania? We are a free country bwana, na EAC is not gonna overule our constitution.

..suala lingine Tanzania tuna better option zaidi ya EAC. Sisi ni wanachama wa SADC ambayo ina combined population of 257 million kulinganisha na East Africa ambayo ina population ya 150 million.

..Tanzania haisusii wala haitasusia mashirikiano ya kiuchumi na kibiashara na nchi yoyote ile. Ila masuala ya ARDHI wananchi wamesema over and over kwamba hawataki kuingiliwa. Suala la mkataba wa ulinzi tumesema hatutasaini mkataba wa kiujanja-ujanja. Ushiriki wetu[tanzania] kwenye EAC utaendelea kuwa on our terms not on any other country's terms.
 
Safi sana Bukyanagandi...... kwanza uhuru wa kujadiliana si sawa na ya kutaniana. Na post hii ni ya kufanya uchanganuzi hasa nini kinachozuia maendeleo ya kasi barani na haswa Afrika mashariki. Tunataka pia kueleza au kujibu maswali magumu kuhusu kama ni mwendo wa kasi wa maendeleo ulioiboronga Euro-zone na kufanya yakawa watumwa wa mikopo. Tunataka pia tujikumbushe na tufahamu kama shughuli ya mungano wa Euro na kutia saini kwa nchi kumi na mbili za Ulaya katika mkataba wa "Maastricht Treaty" ulikuwa na ulbuniwa kwa lengo zuri au baya? Tunaeza jiuliza pia kama tunezipa mgongo suala hadharani la kuzorota kwa njia za ubunifu an utekelazaji sera ndani ya safu za uongozi EU.

Mkuu wala husipoteze muda kujadiliana nao maswala ambayo yako obvious, si rahisi kubadirisha mind set za baadhi yao. Mkuu, baadhi ya hawa jamaa wana malengo fulani katika forum hii na wako well organized, wanafikili wakisema sema Tanzania basi hilo tu litatufanya tubadirishe misimamo yetu thabiti kuhusu certain issues ambazo wanaona tulisha washtukia siku nyingi na siku hizi tumewazidi kete, wanatuona kero kweli kweli. Kuikasikilia TANZANIA kunatokana na msimamo wetu huo wa kukataa shotgun wedding ya Federation vile vile na kutokubali ku-sign an open ended clauses zilizo wekwa kimaksudi kula kwetu.

Leteni mambo ya kujenga kwenye FORUM hii na sio ridiculous rhetoric ambazo hazisadii chochote Tanzania, Kenya au wana JF, mimi binafsi sipendi mambo ya kutuniana misuri kama wendawazimu.
Mkandara, nikirudi katika mada, swali ni Kasi ya maendeleo ni nzuri kwa mataifa ya Afrika au una ubaya wake? Kuna mifumo aina nyingi ya serikali lakini zote matokeo haziridhishi. Hivi niliambiwa na Mkandara nielezee nini kiini cha Uispania, Italia, na Ureno kupata pigo katika uchumi.

Historia ya Demokrasia nchini Spain, Portugal, na Greece:


Nchi hizi ndizo the most affected katika Eurozone na demokrasia hizi zilianza mwaka wa 70. Hali inayodhihirishwa na "ustawi wa demokrasia" hizi ni ya kutatanisha. Kuna sababu nyingi kando na ubadhirifu wa fedha Uhispania zinazochangia kuanguka kwa uchumi (ambao huendeshwa na mapato zinazotokana na biashara ya "real-estate"). Matumizi ya fedha ya kitaifa katika miradi ya kawi katika bajeti iliongezeka, huku ikiongeza deni la kitaifa/national debt kuwa kubwa.

Uhispania:
Msimu huu Uhispania imefikia katika "njia-panda" katika matumizi ya fedha ya kitaifa/government spending. Je! Uhispania itazuia/katiza matumizi mengi ya fedha ya kitaifa kupunguza deni, au itasalia/kuzidi kukopa mikopo kutoka IMF na Banki ya dunia (ambapo credit-rating itashuka hadi "junk-levels"). Yafaa itiliwe maanani kuwa ni vigumu wigo wa uchumi kupanuka na kuzaa mapato pasipo na matumizi ya fedha. Ndiposa, ninaposikiza malalamishi ya wtz wengi kuhusu muungano wa sarafu, ninakubali hali ilivyo hapo na huwa sipingi. Hakika, sera hizi za serikali za kisocialisti zimewekwa/au zitawekwa katika katiba na afadhali Tz isalie hapo SADC kuliko EAC...(NB..mataifa mengine yanapopigania kuingia EAC, inaonekana jambo ls kutafuta ufadhili wa ardhi, fedha, au CHAKULA).

Taswira tunayoipata kati ya SADC na EAC ni ukubwa wa populations katika SADC ambao ukitizama ni rasilimali ambao hujatiliwa maanani. Umaskini katika bloc hii ni ya kusikitisha mno, licha ya mataifa mengine kutangaza kuboreka kwa uchumi kutokana na uvumbuzi wa madini/rasilimali kama gesi, makaa-ya-mawe, na uchimbaji mafuta. Nusu ya watu wanaishi chini ya dola-kwa-siku. Poor population intergration katika mataifa SADC pia inatisha/XENOPHOBIA(jambo halizungumziwi lakini ni wazi/hadharani). Tena picha halisi ya HIV/AIDS, inadidimiza sehemu ya tija ya populations.

Ureno:
Taswira ya Ureno ni kinyume na ya Uhispania bila kusahau pia Ireland ni mojawepo ya mataifa ina hili tatizo. Si mara ya kwanza Ugiriki kupata mkopo/bail-out kutoka EU, na mikopo hii imezidisha kusambaratisha uchumi. Hivi sasa IRELAND na GREECE zimesalia "financial-basket-case". PORTUGAL imesalia katika biashara kuuza sehemu ya hisa za kitaifa/government shares/bonds kuhifadhi Uchumi na kuvutia wawekezaji kutoka nje. Uchumi ureno unaoendeshwa sana na ukulima, hutegemea sana ununuzi wa bidhaa za mafuta kutoka mataifa mengine kukithi mahitaji ya kawi na uzalishaji wa viwanda. Hili ni jambo huchangia pakubwa katika utumizi mkubwa wa fedha ya kitaifa na kuongezea mapungufu katika bajeti.

Italia:
Kinyume na taswira za nchi zingine, kuna tofauti kubwa ukijaribu kulinganisha uchumi wa ITALY na mengine Eurozone. Sekta nyingi/asilimia kubwa ya biashara huendeshwa na watu/familia binafsi/makundi ya wafanya biashara mashuhuri ambao ni wamiliki viwanda. Kimaendeleo, taifa hili linaorodheshwa kama ishirini na tatu (technologia, na mawasliano). Tukizingatia mambo haya, ni rahisi kwa nchi hii kupata mafanikio katika panda-shuka yake ya kuimarisha/kuhifadhi uchumi maana deni sio la taifa, ila ni watu binafsi ambao wana jukumu la kulipa deni kwenye Banki kuu/European Central Bank. Uchumi wao unaweza kufananishwa kimsingi na ya Uchina.

..........Uchumi/Italy ni mara mbili zaidi katika ukubwa ukishikanisha ule wa Greece na Ireland.

Yaonekana uchumi wa taifa hili halijarudi hatua nyingi nyuma sababu kuu ikiwa umeegemea kwenye sekta ya ununuzi na uuzaji hisa/sovereign bonds kati yake na European central bank. Yaonekana kama likizo la afueni, lakini swali ni lini/njia ipi itatumika kulipa deni?

Taswira halisi ya URUSI/mtazamo wa uchumi na hadhi yake:

Sekta ya ununuzi na uuzaji wa bidhaa ndani ya Russian Federation mathalan ya mataifa mengine Europa yaliyostawi (Germany, France, na Britain) na uchimbaji madini/almasi, ndio vipengee ambavyo vimekuwa msingi wa upanuzi wa wigo wa uchumi na huchangia pakubwa katika uendeshaji wake. Uzalishaji wa kawi na uuzaji wa mafuta huchangia kwa asilimia ndogo katika kuimarisha uchumi. Pia, tofauti nyingine na inayodhihirika wazi ni sifa yake katika umilikaji wa hazina kubwa ya fedha. Licha ya sifa hiyo, sekta ya ununuzi wa bidhaa unagharimu serikali kiasi kikubwa kutoka kwa hazina ya taifa/Russian Federation huku sekta yake ya uuzaji inayoendeshwa na ukulima/ukuzaji wa mimea ikipata pigo kutokana na janga ya kitaifa kama ukame na kupanda kwa ghafla katika bei za bidhaa muhimu kama vyakula.

Kuna taswira pia mataifa mengi yanaambatanisha uchumi zao na Russian federation katika kufadhiliwa/subsidies mfano nchi za Ukraine na Georgia. Tofauti ya maendeleo/mwanya ulioko kati ya nchi za Russia na jirani zake ni kubwa mno, ambalo kwa muda mrefu imefanya nchi hizi kutegemea nchi za Magharibi, Asia, na Europa kwa ununuzi wa bidhaa na tena kama njia ya kuepuka ubepari unaodhihirishwa na Russian Federation. Bidhaa za kutengenezwa kutokwa kwa uzalishaji ya kawi hujumuisha asilimia 20% tu ikilinganisha na 65% zinazotoka kwenye viwanda.

Hatuwezi lenga kushughulika kuleta mambo ya kujenga wakati kuna sekta zingine zimeorodheshwa duni. Ni heri EAC kama muungano uvunjwe maana licha ya kujaribu kuondoa vikodi, haileti manufaa maana kila nchi ina sera zake. Ninavoona katika siku za baadaye, EAC itabaki tawi unganishi la SADC. Manake tukitarajia kuingilia intergration na kuruhusu uhuru wa uhamiaji, mataifa yote EAC yatakubali lakini, isiwe moja ya mataifa inakataa huku ikitumia ardhi kama sababu. Hali hii haifai kuwa ngumu kama wadau wengine wanjaribu kuonyesha. Mradi tu kuna viwanda na biashara inaoendelea, labor-force ya Afrika mshariki itakuwa rasimali yenye maana.
 
Kabaridi,
Mku8u wangu umeeleza mambo madogo sana ambayo ni sura ya uchumi wa nchi hizi na sii sababu kubwa ya kuathirika kwa uchumi wa nchi hizo. Greece, Ureno na Spain zote zinaathirika kiuchumi kutokana na kuingia EU kichwa kichwa wakati kiujumlay hawakuwa na kitu cha kuuza ktk nchi nyinginezo zaidi ya wao wenyewe kuwa Wahitaji..Hivyo, ukitazama kwa undani kwa nini nchi hizi madeni yamewaelemea ni kwa sababu wakopo zaidi ya uwezo wao kuuza. Unapouza unakuwa unajenga faida na kupitia faida ilopatikana ndipo unalipa madeni na kubakia na ziada.

Swala la Matumizi ya serikali linaweza kuwa na uzito mkubwa ktk kuchangia lakini wakati huo huo mchango huo unatokana na uzalishaji maana Uingereza, Germany na France wana matumizi makubwa ya serikali kuliko Ureno, Greece na Spain lakini maadam wao wanauza, wamewekeza ktk vitu vinavyolipa na kuhitajika, wana mishahara mizuri na kadhalika wanaweza kuyamudu matumizi yao kutokana na faida inayopatikana.

Ni mfano rahisi sana wa matumizi hata yetu sisi, kama wewe una biashara inayolipa tuseme kwa kila siku unaingiza 1 millioni faida na ukitumia 500,000 (50%) kila siku kwa matumizi yako mwenyewe haitaonekana unafuja fedha kuliko Mkandara ambaye anaingiza 100,000 kama faida kwa siku na akatumia 80,000 kwa siku (80%). Huyu ni rahisi kumyooshea kidole lakini Kiuchumi kabla ya kulaumu ni lazima pia tutazame mfumko wa bei za bidhaa ili kuhalalisha ama kutohalalisha matumizi ya hizo Tsh 80,000 kwa siku na sio tu kuchukua asilimia 80 ya pato lake Mkandara hujirusha ndio maana anakwenda chini. Sasa ukija punguza matumizi haya unakuta kumbe unapunguza hata nauli ya mtoto kwenda shule, Kupungua safari na matumizi ya gari hata kwenda kazini, mke kusuka na kutengneza kucha (unaharibu ndoa), nyama choma (unafukuza marafiki) na kadhalika ambayo kumbe ni muhimu sana ktk ujenzi wa familia yangu...

Haya ndio yanayotokea Greece, Ureno na Spain mkuu wangu nchi hizi hazina cha kuuza EU zaidi ya wao kuwa tegemezi na ktk maswala wanayoambiwa wakate matumizi ambayo ndio muhimu zaidi kwa wananchi wake. Na ukitazama kiuchumi kama huna uwezo huna budi kuachia baadhi ya lakini Germany, UK na France wao wanendelea kujirusha kwa sababu biashara zao kubwa kubwa bado zina soko kubwa ktk soko la Ulaya na dunia tofauti na hawa wangineo. Kama kweli Germany, UK na France wanataka umoja wa nchi za Ulaya basi wafanye wawe na mfuko mmoja wa Ktaifa ktk kukusanya mapato ya EU, kisha wagawane uone kama hayo mataifa makubwa watakubali... Nchi maskini zote zitapenda hivyo lakini Germany, France na UK watapinga vikali na pengine hata kuondoka ktk ushirikiano huu huu kulinda maslahi yao. Siasa za kiuchumi na Ubepari zina mfumo wa CHANGU CHANGU, CHAKO CHANGU hasa ukiwa mhitaji..

Maadam sisi Tanzania ni Wahitaji hatuna sababu wala haraka ya kujiunga na EAC maana hatuna kitu cha kuuza huko isipokuwa siasa za ujanja ujanja. Nyie nambieni tukiweka sarafu moja itatusaidia nini kiuchumi?..Kujiunga kwetu EAC inatusaidia nini kiuchumi ikiwa bandari zetu mbovu kuliko Kenya, reli yetu mbovu, usafiri wa anga mbaya, Utalii Kenya wamejiweka vizuri zaidi, mazao ya chakula - Kilimo kwanza kime fail, hatuna viwanda isipokuwa tuna soko kubwa la mahitaji toka sindano hadi vifaa vya ujenzi na huduma za jamii kama simu, shule, Hospitali, vyakula, mavazi, na kadhalika ambavyo mashirika yote ofisi mama ziko Kenya au nje.

Naomba sana nambieni sisi tunafaidika vipi na EAC haswa!...
 
The has been many issued raised in the EAC National asembly regarding intergration but if one look at each issue raised by out neighbour you will find that their main interest is Tanzanian' Land!!! Shame on them!!! Even the cuurent bill as introduced by our fellow its’ enforcement is now being challenged by Tanzania, on the grounds that it would interfere with land issues which are not part of the broader EAC Treaty.
I would like again to request our representatives in the East African Assembly and our President Jakaya Kikwete not to sign the Bill. It’s against the EAC Treaty,” This Bill originated from a private motion
I will never never ever accept the land issue to be put in the East African Matters never ever
 
Ni ruhusu tu niseme, tofauti ya matumizi ya fedha kati ya Spain na Germany ni kubwa. Tatizo ni Ugerumani walipoboresha sekta yao ya uuzaji na ununuzi wa bidhaa uhuispania wangalijaribu kufuata mfano huo. Hivi Uhispania walijaribu kubishana na ndovu (Ugerumani) kunia na ndio jambo likawatumbukiza kwenye shimo la deni. Serikali nchini Ujerumani ni ya kisocilaisti kama Uhispania na mengine EU. Na hili ndilo tatizo pia na Ureno na Ireland.. Italia wanaweza samehewa lakini si kwa muda mrefu.

Kusema tanzania ni wahitaji wa msaada ni wazo tu lako mwenyewe ambao umejiwekea. Kuna kwa mfano Wingi wa populations/labor-force. Mutafaidika ikiwa kutakuwa na uwazi katika kutaka kushirikiana katika uongozi na mandeleo na kuhakikisha uchumi Afrika mashariki imesawazishwa.

Kabaridi,
Mku8u wangu umeeleza mambo madogo sana ambayo ni sura ya uchumi wa nchi hizi na sii sababu kubwa ya kuathirika kwa uchumi wa nchi hizo. Greece, Ureno na Spain zote zinaathirika kiuchumi kutokana na kuingia EU kichwa kichwa wakati kiujumlay hawakuwa na kitu cha kuuza ktk nchi nyinginezo zaidi ya wao wenyewe kuwa Wahitaji..Hivyo, ukitazama kwa undani kwa nini nchi hizi madeni yamewaelemea ni kwa sababu wakopo zaidi ya uwezo wao kuuza. Unapouza unakuwa unajenga faida na kupitia faida ilopatikana ndipo unalipa madeni na kubakia na ziada.

Swala la Matumizi ya serikali linaweza kuwa na uzito mkubwa ktk kuchangia lakini wakati huo huo mchango huo unatokana na uzalishaji maana Uingereza, Germany na France wana matumizi makubwa ya serikali kuliko Ureno, Greece na Spain lakini maadam wao wanauza, wamewekeza ktk vitu vinavyolipa na kuhitajika, wana mishahara mizuri na kadhalika wanaweza kuyamudu matumizi yao kutokana na faida inayopatikana.

Ni mfano rahisi sana wa matumizi hata yetu sisi, kama wewe una biashara inayolipa tuseme kwa kila siku unaingiza 1 millioni faida na ukitumia 500,000 (50%) kila siku kwa matumizi yako mwenyewe haitaonekana unafuja fedha kuliko Mkandara ambaye anaingiza 100,000 kama faida kwa siku na akatumia 80,000 kwa siku (80%). Huyu ni rahisi kumyooshea kidole lakini Kiuchumi kabla ya kulaumu ni lazima pia tutazame mfumko wa bei za bidhaa ili kuhalalisha ama kutohalalisha matumizi ya hizo Tsh 80,000 kwa siku na sio tu kuchukua asilimia 80 ya pato lake Mkandara hujirusha ndio maana anakwenda chini. Sasa ukija punguza matumizi haya unakuta kumbe unapunguza hata nauli ya mtoto kwenda shule, Kupungua safari na matumizi ya gari hata kwenda kazini, mke kusuka na kutengneza kucha (unaharibu ndoa), nyama choma (unafukuza marafiki) na kadhalika ambayo kumbe ni muhimu sana ktk ujenzi wa familia yangu...

Haya ndio yanayotokea Greece, Ureno na Spain mkuu wangu nchi hizi hazina cha kuuza EU zaidi ya wao kuwa tegemezi na ktk maswala wanayoambiwa wakate matumizi ambayo ndio muhimu zaidi kwa wananchi wake. Na ukitazama kiuchumi kama huna uwezo huna budi kuachia baadhi ya lakini Germany, UK na France wao wanendelea kujirusha kwa sababu biashara zao kubwa kubwa bado zina soko kubwa ktk soko la Ulaya na dunia tofauti na hawa wangineo..Kama kweli Germany, UK na France wanataka umoja wa nchi za Ulaya basi wafanye wawe na mfuko mkoja wa KItaifa ktk kukusanya mapato uone kama hayo mataifa makubwa watakubali... Nchi maskini zote zitapenda hivyo lakini Germany, France na UK watapinga vikali na pengine hata kuondoka ktk ushirikiano huu huu kulinda maslahi yao. Siasa za kiuchumi na Ubepari zina mfumo wa CHANGU CHANGU, CHAKO CHANGU hasa ukiwa mhitaji..

Maadam sisi Tanzania ni Wahitaji hatuna sababu wala haraka ya kujiunga na EAC maana hatuna kitu cha kuuza huko isipokuwa siasa za ujanja ujanja. Nyie nambieni tukiweka sarafu moja itatusaidia nini kiuchumi?..Kujiunga kwetu EAC inatusaidia nini kiuchumi ikiwa bandari zetu mbovu kuliko Kenya, reli yetu mbovu, usafiri wa anga mbaya, Utalii Kenya wamejiweka vizuri zaidi, mazao ya chakula - Kilimo kwanza kime fail, hatuna viwanda isipokuwa tuna soko kubwa la mahitaji toka sindano hadi vifaa vya ujenzi na huduma za jamii kama simu, shule, Hospitali, vyakula, mavazi, na kadhalika...

Naomba sana nambieni sisi tutafaidika vipi na EAC haswa!...
 
Ni ruhusu tu niseme, tofauti ya matumizi ya fedha kati ya Spain na Germany ni kubwa. Tatizo ni Ugerumani walipoboresha sekta yao ya uuzaji na ununuzi wa bidhaa uhuispania wangalijaribu kufuata mfano huo. Hivi Uhispania walijaribu kubishana na ndovu (Ugerumani) kunia na ndio jambo likawatumbukiza kwenye shimo la deni. Serikali nchini Ujerumani ni ya kisocilaisti kama Uhispania na mengine EU. Na hili ndilo tatizo pia na Ureno na Ireland.. Italia wanaweza samehewa lakini si kwa muda mrefu.
Hilo la Usoshalisti sio kweli mkuu wangu sisi tumefundishwa tofauti kabisa hizi siasa za Kiuchumi. Usoshalist wa nchi za Kibepari hauna maana uchumi unaendeshwa na serikali hii dhana imekwisha siku nyingi sana hakuna kitu hicho. Sasa hivi neno usoshalist unahusu tofauti ya VIPAUMBELE ktk kukuza uchumi wa nchi. Nchi hizi za Greece, Spain na Ureno ni mabepari kama mabepari wengine, isipokuwa usoshalist wao wanaweka mkazo ktk ustawi wa jamii meaning - The means justify the end.

Hata Marekani wapo ktk usoshalist kwa mtazamo huo na hata enzi ya Clinton walikuwa ktk usoshalist lakini waliweza vipi kufanya vizuri. Hivyo Hata France sasa hivi aloshika nchi ni Msoshalist, Germany vyama vingi viko kushoto isipokuwa CDU/CSU hivyo muda mwingi wamekuwa chini ya vyama shiriki ya Ushirika wa vyama vya kisoshalist unaoitwa - Party of European Socialists, lakini wote wanaendesha uchumi wao Kibepari isipokuwa Vipaumbele vyao viko wapi.

Ukweli unabakia kwamba Ureno, Spain na Greece hawana cha kuuza ktk jumuiya hii wao ni wahitaji na hawawezi hata kushindana isipokuwa wao wamefungua soko zaidi la mali za nchi tajiri kama Uingereza, Germany na France kuuzika nchi hizo. Waingereza, Wahjarumani na Wafaransa walichofuata nchi hizi ni soko na uwezo wa kununua nyumba za summer camp au kujiandaa ktk retirement ktk visiwa na sehemu za beach na ndicho kilichopandisha bei za nyumba sehemu hizo. it's Only a limited demand tofauti na Gernmany, UK au France ambao nyumba zao zinajengwa kwa sababu vijana wengi wanakimbia Greece, Spain na hata Ureno kwenda tafuta kazi na malipo mazuri nchi hizo kubwa. Ni rahisi kuwalaumu Greece kwa matumizi makubwa lakini pia watatengeneza kipi ambacho Germany, France na UK hawatengenezi na kipo ktk market na jina kubwa tayari?.

Ukiwa mhitaji siku zote upo ktk disadvantage ya kuwa wewe unawatengenezea wengine soko na hili ndio naliona kwa Tanzania. Kama tutaweza kuuza kitu chochote nje iwe Kenya ama Uganda nambieni ni kitu gani maana nijuavyo viwanda hatuna, huduma mbovu yaani tuna soko kubwa la wahitaji na sii wazalishaji wanaotafuta soko nje labda hiyo Ardhi maana ndio pekee tulichobakia nacho na wanaitaka sana. Na ukisema tuwe na sauti ya pamoja ktk maswala ya Kijumuiya huu ni uongo mara ngapi Kenya wametuacha nje ktk maamuzi ambayo yalikuwa na faida kwetu wakajiunga upande wa pili? African leaders wanaweza kuhongwa na wakakuuza - Hatuaminiki.
 
Kabaridi said:
Hatuwezi lenga kushughulika kuleta mambo ya kujenga wakati kuna sekta zingine zimeorodheshwa duni. Ni heri EAC kama muungano uvunjwe maana licha ya kujaribu kuondoa vikodi, haileti manufaa maana kila nchi ina sera zake. Ninavoona katika siku za baadaye, EAC itabaki tawi unganishi la SADC. Manake tukitarajia kuingilia intergration na kuruhusu uhuru wa uhamiaji, mataifa yote EAC yatakubali lakini, isiwe moja ya mataifa inakataa huku ikitumia ardhi kama sababu. Hali hii haifai kuwa ngumu kama wadau wengine wanjaribu kuonyesha. Mradi tu kuna viwanda na biashara inaoendelea, labor-force ya Afrika mshariki itakuwa rasimali yenye maana.

Kabaridi,

..sasa hivi contribution ya wa-Tanzania kwenye EA ni kilimo ktk kuzalisha raw materials zinazo-feed viwanda vya Kenya.

..hivi mkiwanyang'anya ardhi wa-Tanzania je contribution yao kwenye EAC itakuwa ni nini?

..je mtawapeleka wapi 70% ya wa-Tanzania ambao wanategemea ardhi na kilimo for their living?

..hakuna sector yoyote ile inayokuwa hapa Tanzania ambayo unaweza kusema itachukua labor force ya wananchi wataokosa ardhi ikiwa tutaweka suala la ardhi ktk EAC.

..wengine tunapopinga suala la ardhi we r not speaking for ourselves but on behalf of wananchi wanyonge wasiona na sauti walioko vijijini.


 
Kabaridi,
Mku8u wangu umeeleza mambo madogo sana ambayo ni sura ya uchumi wa nchi hizi na sii sababu kubwa ya kuathirika kwa uchumi wa nchi hizo. Greece, Ureno na Spain zote zinaathirika kiuchumi kutokana na kuingia EU kichwa kichwa wakati kiujumlay hawakuwa na kitu

Siasa za kiuchumi na Ubepari zina mfumo wa CHANGU CHANGU, CHAKO CHANGU hasa ukiwa mhitaji..

Maadam sisi Tanzania ni Wahitaji hatuna sababu wala haraka ya kujiunga na EAC maana hatuna kitu cha kuuza huko isipokuwa siasa za ujanja ujanja. Nyie nambieni tukiweka sarafu moja itatusaidia nini kiuchumi?..Kujiunga kwetu EAC inatusaidia nini kiuchumi ikiwa bandari zetu mbovu kuliko Kenya, reli yetu mbovu, usafiri wa anga mbaya, Utalii Kenya wamejiweka vizuri zaidi, mazao ya chakula - Kilimo kwanza

Naomba sana nambieni sisi tunafaidika vipi na EAC haswa!...
Mkandara hayo malalamishi ya reli, viwanda, na bandari yenu kuwa duni/innefctive, ni jukumu la serikali ya siku kuhakikisha inaongeza miradi ya maendeleo na kuboresha/imarisha state-assets kama hizi. Maajabu ni pesa zinapokuja uzembe unaingia na pesa kugawanyishwa kwenye miradi bure..Hauwezi kusalia tu kwenye vilio kwamba hatuna hili, hatuna lile. Maana kuna Kodi, kuna ufadhili wa WB na Banks zingine na miradi hii inatarajia iwekwe katika uwazi wa matumizi ya fedha..Au njia nyignine pia mwafaka na imeonyesha matumaini ni nikutafuta bilateral trade patnerships/ushirikiano wa biashara/maendeleo ambazo ndio njia pekee naona zitasaidia nchi za Afrika mashariki. Mfano tafuta ushirikiano wa biashara na nchi zingine kama Dubai na na mataifa mengine.

Kutoka kitambo, tumekuwa na misaada na ufadhili kutoka ulaya na nchi zingine za magharibi zilizostawi...Lakini ajabu watu hawana ujasiri wa kuuliza pesa hizi baada ya kuletwa, zakwenda wapi. Zinasalia kwenye akaunti za ngambo zikingojea kutekeleza makampeini. Kuna ile taswira inaonekana kuwa Spain haina lolote/bidhaa za kuuza. Hiyo inaweza ibua tetesi kwa sababu mwanzo kuna watu kutoka spain ambao wamekuwa na desturi ya kuwekeza biashara/mali/hisa katika mataifa mengine. Jambo lingine pia muhimu ni..Ujerumani na Ufaransa tu katika EU wameimarisha SERA zao za foreign Direct investment/uwekezaji kutoka ngambo. Ndio unakuta pamoja na Ujerumani kuwa na Sekta ya biashara ya uuzaji na ununuzi ilioimarika wamefungulia uwekezaji kutoka bara kote Uropa.

kama wenyeji uhispania na ugiriki wangeonyesha taswira kinyume ya kuwekeza mali ya katika nchi zao, tungeshuhudia kinyume Mkandara. Lakini hii ni kuonyesha SERA ya multi-cultural policy katika SPAIN, GREECE na PORTUGAL imesusiwa kinyume na taswira tunayoona katika uchumi zilizostawi(Ujerumani na Ufaransa). Kwa kifupi nchi hizi zinazokabiliana na austerity zingeweza kurejelea kuunda upya kwa SERA hii ya multi-cultural policy, isihusishe tu masuala ya biashara, bali pia kuishi pamoja kawa raia wa nchi hizo na raia wengine iwe ni wawekezaji au la. Sera ambayo Ujerumani imeimarisha hivi juzi. Sio kama awali kulikuwa vigumu kuingi huko.

Mataifa mengi zilizostawi kiuchumi wamerejelea kuunda upya SERA hii katika sehemu nyingi na siyo biashara pekee, hata katika elimu ya ngazi ya juu. Kwa mfano Russia walifungua milango ya vyuo vikuu kuchukulia programmes. Mataifa mengi yenye "closed-door" multicultural policy ndio utakuta wanalalama kuhusu EU na wngi wafanya kazi wamo vijiweni mataifa mengine kutafuta kazi. Mfano Spain na Greece Halafu, usiseme lolote kuhusu Greece na Spain kukosa bidhaa za kuuza. Wale FDI foreign direct investors wa uhispania wako Marekani kule wamefungua makampuni/makubwa ya ajabu. Ujerumani kuna wawekezaji kutoka uhispania na hapa ndio Ujerumani inawapiga bao.

Huku uhispania ikililia msaada wote siku zote, uwekezaji hautanawiri nchini uhispania pasipo kurudi na kutunga upya sera ya aina hii. Inakuwa tena vigumu kuwekeza katika mataifa ambayo haina a strong business and investment culture. Uchina na serikali yao ya kisoshalisti ndio inaweza tamukwa kama "living success model". mengine mataifa na usoshalisti yametumbukia nyongo katika agenda zao.

@Jokakuu, hata sisi tunajitegemea kutoa raw materials zetu za kufeed viwanda na za kununuliwa Tanzania ni bunous ama surplus buying, hivi kama dhana yako nikuwa kenya haina source ya raw materials, naomba ujifikirie mwenyewe. Uganda wako na viwanda vyao upcoming sio ajabu kuona Uganda ikiipiku tanzania maana mwanya katia yake si kubwa.
 
Kabaridi said:
hata sisi tunajitegemea kutoa raw materials zetu za kufeed viwanda na za kununuliwa Tanzania ni bunous ama surplus buying, hivi kama dhana yako nikuwa kenya haina source ya raw materials, naomba ujifikirie mwenyewe. Uganda wako na viwanda vyao upcoming sio ajabu kuona Uganda ikiipiku tanzania maana mwanya katia yake si kubwa.

Kabaridi,

..Ur 100% correct.

..Industrialization is going on at a snails pace in Tanzania.

..Hiyo nayo inachelewesha wakulima "ku-graduate" frm using jembe la mkono, kwenda kuwa wakulima wa kati, and later on large scale farmers.

..Pia I dont believe in bringing in large scale farmers from outside. I think it is better kuwafundisha wakulima wetu and creating an environment and incentives kwa wakulima wetu kuzalisha zaidi na zaidi.

..Kwa kweli we have to put our house[Tanzania] in order. Viongozi wetu wamelala usingizi mzito. Watanzania hawafaidiki chochote kutokana na PEACE and RESOURCES ambazo tunazo.​


 
JokaKuu ukidhani kenya inawania kuingia na kuchukua mashamba lazima mufikirie tena. Chochote tanzania ina uwezo wa kupanda au kutengeneza/raw materials, kenya iko na uwezo na mashamba kwa wingi. Kwa mfano kenya angalia Agricultural based products kama kahawa na chai. Tizama pamba na mengine mengi.. Naongelea what is currently practical, yaani viwanda na bidhaa za agro-based. Tayari misingi ya viwanda iko imara kenya hivyo si swali la Kenya inawania kuleta land-grabbing.

Nadhani hii ndio msemo unaopotosha umati na uma kwa jumla wakati majadiliano yanapoendelea kuhusu Intergration. Tena kenya imeshapanda kwenye ngazi ingine....kumaanisha haitegemi Agrobased industries pekee kama msingi wa kuendesha uchumi wake. Kuna uwekezaji ya aina nyingi mpaka kwenye tovuti/BPO. Hivi mambo ndio yalivyo hapa kenya advancement imeendelea kiwango hicho. Nilipozungumza na mtanzania moja hapa JF aliniambia bado tanzania wanabeba hundi kwenye vigari. lol. Je! ni kweli matumizi ya kadi za plastiki/credit cards hazitumiki?



Kabaridi,

..Ur 100% correct.

..Industrialization is going on at a snails pace in Tanzania.

..Hiyo nayo inachelewesha wakulima "ku-graduate" frm using jembe la mkono, kwenda kuwa wakulima wa kati, and later on large scale farmers.

..Pia I dont believe in bringing in large scale farmers from outside. I think it is better kuwafundisha wakulima wetu and creating an environment and incentives kwa wakulima wetu kuzalisha zaidi na zaidi.

..Kwa kweli we have to put our house[Tanzania] in order. Viongozi wetu wamelala usingizi mzito. Watanzania hawafaidiki chochote kutokana na PEACE and RESOURCES ambazo tunazo.​
 
Kabaridi,
Sijakuelewa unapozungumzia multi-cultural policy? Maana hizi nchi zilikuwa na makoloni hadi Afrika na South America kama umewahi kufika Ureno au Spain hutaweza kusema haya uyasemayo. Hiyo Ugiriki wenyewe Wabongo sisi tumeanza kwenda Ulaya kirahisi a kupokelewa na kufanya kazi ni Ugiriki. Sasa haya maswala ya mult cultural yanatoka wapi ili hali hakuna nchi duniani wabaguzi kama Wajarumani iwe toka enzi ya Hitler hadi leo hii. Na naweza kusema ktk nchi za Ulaya sehemu za Wajarumani iwe Germany yenyewe Austria, Swiss ndio kuna mchanganyiko mdogo sana ikifuatiwa na wajomba zao Holland.

Umewahi kusikia neno la kiswahili 'Rohostoki' ikiwa na maana mtu mwenye roho mbaya?... Hili neno limetokana na mji mmoja Ujarumani wenye jina hili ambapo mabaharia weusi walikuwa hawaruhusiwi hata kutoka nje ya bandari...Je, unajua hayo. Leo hii Mchina anatupiga mabao vipi? kwani Marekani na UK hawawezi kutengeneza vitu hivyo na Mchina ana policies zipi kuhusu multi culturalism nyumbani kwake.


Halafu umezungumzia FDI wa Kihispania walioko Marekani na Ujarumani! this is exactly what Iam talking about.. Wahispania, wareno na Wagiriki wanaikimbia nchi yao wenyewe kwenda kuwekeza nje yaani wanaihama nchi yao wenyewe kutafuta green card nje. Haya unaambiwa 10 kati ya richest men in UK are Greek origin...Hata sisi Wakerewe tumekimmbia Ukerewe kutokana na kwamba opportunity za kutajirika ama kujiendeleza zaidi hakuna - sangara wamekwisha! ahahaha! haha!

Kuna habari nyingine inasema kiasi cha £10bn zimehamishwa na matajiri wa Ugiriki kwenda Uingereza toka hali mbaya ya uchumi itangazwe Bofya. Austerity measure walizopewa Ugiriki ni ktk kuwawezesha kuendelea kuwa wahitaji maana soko lao linahitajika kununua mali za nchi tajiri, yaani sawa na mkopo wa Benki kununua gari ambapo wenye magari ndio wawekezaji ktk Benki hiyo hiyo.

Benki inaingiza na wenye magari wanauza hivyo wewe unayenunua gari wakati huna kipato cha kukuwezesha kuishi kwa mkopo ndiye unajikamua... benki inakula interest na wenye magari wanauza hapa umepigwa mande. Hiki ndicho kilichotokea Greece, wanapewa mkopo kwa malengo ya kuzinufaisha benki na wawekezaji wake.. Kunamengi nyuma ya pazia ambayo wewe na mimi hatuonyeshwi.
 
JokaKuu ukidhani kenya inawania kuingia na kuchukua mashamba lazima mufikirie tena. Chochote tanzania ina uwezo wa kupanda au kutengeneza/raw materials, kenya iko na uwezo na mashamba kwa wingi. Kwa mfano kenya angalia Agricultural based products kama kahawa na chai. Tizama pamba na mengine mengi.. Naongelea what is currently practical, yaani viwanda na bidhaa za agro-based. Tayari misingi ya viwanda iko imara kenya hivyo si swali la Kenya inawania kuleta land-grabbing.

Nadhani hii ndio msemo unaopotosha umati na uma kwa jumla wakati majadiliano yanapoendelea kuhusu Intergration. Tena kenya imeshapanda kwenye ngazi ingine....kumaanisha haitegemi Agrobased industries pekee kama msingi wa kuendesha uchumi wake. Kuna uwekezaji ya aina nyingi mpaka kwenye tovuti/BPO. Hivi mambo ndio yalivyo hapa kenya advancement imeendelea kiwango hicho. Nilipozungumza na mtanzania moja hapa JF aliniambia bado tanzania wanabeba hundi kwenye vigari. lol. Je! ni kweli matumizi ya kadi za plastiki/credit cards hazitumiki?

Kabaridi,

..hata Tanzania service sector ina-contribution kubwa zaidi ktk uchumi kuliko kilimo.

..sasa tatizo ni kwamba more than 70% ya wa-Tanzania wako vijijini wanalima.

..kwa msingi huo u can see that the economic growth in Tanzania is "artificial" na ndiyo maana unasikia malalamiko yasiyokwisha.

..pia mimi nina uhakika kwamba ukienda kwenye supermarket yoyote ile hapo Nairobi ni nadra sana kukuta bidhaa imetengenezwa Tanzania.

..sasa pamoja na hayo juzi watawala walikuwa wanatuambia ati exports zetu kwenda Kenya zimeongezeka more than 100 folds toka kuanzishwa kwa EAC. I would like to know tunauza nini zaidi ya raw materials ambazo ni mazao ya kilimo??

..That reality ndiyo inayonisukuma mimi kuamini kwamba Tanzania tujielekeze ktk kuimarisha viwanda haswa agro-based ili kuwainua wakulima ambao ni more than 70% ya population.

NB:

..matumizi ya credit cards bado hayajashika kasi haswa ktk maeneo ya vijijini.

..tuna maeneo wananchi hawana maji ya bomba, au hawana hospitali kina mama wanajifungua njiani, sasa unazungumzia mambo ya credit card.

..there is a lot to be done in this country, tatizo viongozi wetu wako busy kujitajirisha wao na familia zao.
 
Mkandara
Ninaposema multi-cultural policy kwa ufupu namaanisha sheria za uhamiaji/immigration laws. Ni kweli kuhusu Rhostoki lakini hivi karibuni wamejaribu kurejelea/review hiyo sheria. Na taswira nitakayokupa ni ya bara Uropa. Tarehe 1st Januari 2005 Ujerumani walijaribu kuvutia wafanyi kazi wenye taaluma mbalimbali. Walifungua maprogramu za Green-card na wakaunda accord/Schengen Accord ambao unaruhusu uhamiaja kati ya mataifa (25 european nations) yalioweka mkataba huo. Ufaransa Kuna "European blue card" ambao ni pasi inaopewa wahamiaji kutoka third-world/Afrika. Pasi ambao unaweza kuwa renewed wakati wowote. Ufaransa pia utaweza kupata "naturalization" kwa sababu kuna sheria imeundwa kukubali wahamiaji kutoka nje kupata permanent residence ikiwa wanaweza kuelewa, zungumza na kutafsiri kifaransa.

Halafu nielezi vile mfumo wa Usoshalisti China unapiga bao mataifa mengi yenye mfumo huo. Wakati huu sekta ya uchumi China haifaidhiliwi na serikali/state-sponsored bali ni private capital kutoka makampuni na biashara/uwekezaji za watu binafsi ndio zinaimarisha uchumi. Ndiposa unaona serikali ya China katika misimu za hivi karibuni, wamekuwa wenye kutoa mikopo kwa mataifa ya Afrika maana hazina yao haina pressure yeyote. Ndio nikasema mfumo wa Usoshalisti China ndio ambao utasema a living-success model. Hata mataifa za Afrika zapasa wajiulize kuhusa hali ya hazina yao ya kitaifa.

Kwenye capital flights za ugiriki, wewe unakiri ni wao walisambartisha hazina za Banki za kwao kwa kuinvest £10bn kule uingereza. maadam kama wangewekeza kule kwao, ingekuwa hadithi nyingine tofauti. Sasa muungano wa EU iniaingilia kati kulaumiwa vipi. Hivi niwape tu siri. Watu wanapolalamika kuhusu interest-rates Kenya zikiwa zimepandishwa/25% wakati kuna upungufu wa fedha/inflation ni cha maana sababu huzuia mtu wowote kuja tu na kuchukua mikopo kwa wingi bila kujua njia mwafaka ya kuzilipa.

Kumalizia nitasema, makosa kubwa siyo muungano wa sarafu, ila ni matendo ya raia wa nchi hizo. Mfano Uhispania, mtu wowote tu aliyekuwa na uraia wa spain aliweza pata mikopo/mortgages kununua manyumba, pasipo collateral. Wakati sekta ya banks zinapeana mikopo na kumaliza hazina, kwanza biashara hutikiswa. Greece pia vilevile tatizo ni ile ile, capital flights kutoka kwa banks humo na wale wafanya kazi kupeleka kwenye nchi geni si makosa ya muungano. Portugl vilevile wamesalia kuuza hisa za kitaifa/sovereign bonds kubargain na Ujerumani kuwapa msaada/mkopo/bail-out. Nchi hizi zinaathirika mno na ufinyu wa bajeti. Mawizara zao pia zimesalia katika ufinyu wa bajeti.
 
Bravo Kabaridi, hivi Kiswahili umejifunza wapi? naona unajitahidi KWELI KWELI!!! Wiki mbili Arusha kwenye mkutano wa vijana ndio umekuwa bingwa hivi au unatoka TAVETA/Mombasa. Would U mind for a spin in my Brand new SUKHOI MK007 beast over the WEEKEND?
 
huh-uh....Safi sana Bukyanagandi, mimi ni mkenya lakini natoka sehemu za bara ingawa nimekaa na kufanya kazi mombasa for ten years. Nimeshaishi na wadigo/duruma na nawajua inje ndani. Kiswahili changu ni cha darasani/vintage ambacho nakazana kukiandika. Nakumbuka ulishawahi nialika kikombe cha chai hapo DSM. Nitafanya juhudi tukutane au sivyo.

Bravo Kabaridi, hivi Kiswahili umejifunza wapi? naona unajitahidi KWELI KWELI!!! Wiki mbili Arusha kwenye mkutano wa vijana ndio umekuwa bingwa hivi au unatoka TAVETA/Mombasa. Would U mind for a spin in my Brand new SUKHOI MK007 beast over the WEEKEND?
 
Back
Top Bottom