JokaKuu
Platinum Member
- Jul 31, 2006
- 30,441
- 55,017
Binafsi yangu kutokana na experience niloiona ktk nchi hizi sidhani kama Jumuiya ya EA inaweza kutusaidia badala ya kutuongezea matatizo pande zote. Tazama jinsi Jokakuu na Wakenya wanavyopelekana na hhata kutuhumiana ktk maswala na misimamo tofauti ya nchi hizi. Tazama migogoro tulonayo na Zanzibar badala ya kwenda mbele miaka yote tumekuwa na uhasama fulani ndani wakati wanaofaidika na Muungano huu ni Wazanzibar zaidi ya bara. Rwanda na Burundi wao wanataka ardhi zaidi maana nchi zao ndogo na umoja huu una faida kubwa kwao.
Kenya wamejijenga ktk viwanda na mteja wao mkubwa ni Tanzania na wakiweza kuongeza wigo la ku supply nchi nyingine tano zaidi watajiboresha zaidi kiuchumi. Binafsi yangu naamini kabisa Uchumi wa nchi kama Ureno, Spain na Greece umekufa kwa sababu walikuwa tegemezi wa nchi kama Uingereza, France na Germany ambao wali ongeza wigo la soko la mali zao. Na kifo cha nchi hizi kiucxhumi inaondoa soko lao pia hivyo wako tayari kutumia kiasi chochote cha fedha kuhakikisha uchumi za ya nchi hizi una boreka kwa lengo la kuhifadhi soko lao wakati nchi hizi zinaendelea kuwa wahitaji wa mali za nchi za Germany, Uingereza na Ufaransa, sasa wanasogea zaidi kwa nchi zilizokuwa ktk Russian federation.
Swala la kujiuliza sisi na hii EAC tutafaidika vipi na jumuiya hii iwe kuuza mazao yetu, usafiri au communication au chochote na tunachukua nguvu gani kuimarisha miradi hiyo maana vitu vyote hivi sisi tuko nyuma sana na bado ni wahitaji na sii wazalishaji. Na je Wabunge wetu wanaelewa fika wanatakiwa kusimamia mambo gani ambayo ndio nguzo ya tanzania kujiunga na EAC kama hatuna isipokuwa kufuata mkumbo kwa sababu ya mahitaji yetu wenzetu wakiwa supplier basi tumekwisha. Utaweza vipi kujenga kiwanda cha maziwa ikiwa Kenya wanaweza ku supply kwa bei nafuu na kutosheleza! - Ndio tutalijenga Taifa tegemezi hivyo.
Mkandara,
..hii jumuiya imegeuka kuwa kama utapeli vile.
..wananchi waliambiwa tunaungana ili tuweze kukabili ushindani wa kiuchumi na kibiashara dhidi ya mataifa ya nje.
..kinachotokea on the ground ni nchi wanachama wa EAC kukanyagana, kuhujumiana, na kushindana wenyewe kwa wenyewe.
..nakubaliana na wewe kwamba Tanzania tumekuwa soko la bidhaa za Kenya kwa muda mrefu sasa. Tunachotakiwa kujiuliza ni hali hiyo itaendelea kwa muda gani? What r we doing ili na sisi tuweze kuuza bidhaa za viwandani Kenya, Uganda, na kwingineko?
..wa-Tanzania hawataki UTUMWA na UKOLONI ndani ya East African community. Wako wenzetu ambao wanadhani wao wana haki juu ya wengine ndani ya jumuiya hii.
..