Duu,wanawake wa mjini noooomaaaaaa!!!

Duu,wanawake wa mjini noooomaaaaaa!!!

mchajikobe

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2009
Posts
2,678
Reaction score
1,279
Leo wakati natoka kwenye mihangaiko yangu,kama kawaida barabara za mjini zinauhusiano mzuri sana na foleni,wakati tupo kwenye foleni kuna gari kama latatu mbele yetu lilikuwa limezimika katikati ya barabara,aliyekuwa anaendesha gari hiyo ni binti mmoja mrembo,bila kuomba msaada alibaki ndani ya gari na kuanza kupiga simu,hata hivyo kulikuwa hamna usumbufu kwetu kwasababu hata hiyo foleni ilikuwa haisogei,mara wakatokea vijana wawili wakaja kuisukuma ile gari ili kuiweka pembezoni mwa barabara,yule dada hakutoa shukrani wala kuongea nao chochote,zaidi ya kuendelea kupiga simu tuu,wale vijana walipoondoka yule dada akashuka akiwa ametilia kimini cha hatari na kufungua boneti kisha kufunga bila kufanya chochote,akaingia tena ndani ya gari na kuendelea kupiga simu.Mara ikatokea AUDI nyeusi akashuka mwanaume mmoja mtanashati mkononi anagalon la mafuta la lita tano wakaweka yale mafuta kisha yule dada akaiwasha ile gari kama anataka kuondoka na yule jamaa ambaye alionekana kama ni mume au mpenzi wake akaondoka,lakini cha kushangaza nikwamba yule mwanamke alilizima gari nakuendeleaa kukaa pale pale,haukupita muda mrefu ikaja prado akashuka mwanaume mwingine huku akiwa amebeba galon kama yule wa mara ya kwanza,yule mwanamke akafanya vilevile,jamaa akaondoka mwanamke akazima gari na kuendelea kubaki hapo hapo,kitu ambacho kilinishangaza ni kwamba lilikuja Mercedes benzi na mbaba mmoja naye akashuka na galon ya mafuta akamuongezea kisha akampa yule mwanamke kitu mkononi bila shaka ni hela kisha jamaa akaondoka,na yule dada naye akaingia ndani ya gari na kuondoka,hii ni kitu iliyotokea jioni ya leo maeneo ya kinondoni karibu na Hugo Bar!!Sasa huyu mwanamke inaelekea muda wote aliokuwa anaongea na simu alikuwa anamdanganya mmoja mmoja kuwa ameishiwa mafuta mpaka mwisho ametoka na lita kumi na tano,duu wanawake wa mjini hawafai,na unaweza kukuta hapo alikuwa na appointment na mwanaume mwingine!!!!
 
duh ipo siku watashuka wote wakati mmoja akicheza hiyo gemu ya kutojaza mafuta ya kutosha.
 
duh ipo siku watashuka wote wakati mmoja akicheza hiyo gemu ya kutojaza mafuta ya kutosha.

Wanawake wangekuwa kama wanaume sijui ingekuaje ile tabia ya kutongoza mpaka miaka 60, uzuri wao hapo alipo na kimini chake atazila za hao majamaa ila baada ya miaka kama mitano mbele kama asipou-control mwili wake na thamani yake inashuka hata wa kumwekea lita 2 atakosekana.
 
Hapa ndio mjini....ukijifanya unajua kupenda watu wanakutizama tu...uyo mchuchu unakuta kuna mbishi wa town anatafuna free mandela.

Kuna mtu hapo anachukua mzigo kiulaini with no cost na viwanja vyote wanakwenda hana zaidi ya neno nakupenda na kumsaidia kubeba handbag na kumsifia hapa na pale bila kusahau kumpigia simu mara kwa mara wakati wengine wanazama kwenye ATM kila kukicha lakini ndio hivyo mifuko imetofautiana maana unaweza kukuta mtu amehonga nyumba ukamcheka kumbe mwenzako ametoa asilimia 3 ya kipato chake na yule aliyeonga laki moja ukaona ndogo kumbe ametoa 80% ya kipato chake cha siku 20 hapo kimahesabu alietoa nyingi ni wa laki moja maana ana kazi ya ziada kutafuta hela ya kufidia.
 
Story ya kutunga! "..magari hayasogei,.. kuikaja Aud..ikaja prado..ikaja benz.." ungeniambia ulikua nje ya folen unashuhudia angalau kidogo ungeeleweka japo nayo ingetia shaka kwani kwa hali halisi ya folen ya dar, kuwaita watu 3 toka sehemu tofauti wakaja inachukua muda mrefu
 
Story ya kutunga! "..magari hayasogei,.. kuikaja Aud..ikaja prado..ikaja benz.." ungeniambia ulikua nje ya folen unashuhudia angalau kidogo ungeeleweka japo nayo ingetia shaka kwani kwa hali halisi ya folen ya dar, kuwaita watu 3 toka sehemu tofauti wakaja inachukua muda mrefu

Hata kama ya kutunga....ni uongo mtamu sana...

Na hizi tabia ni kweli kabisa wanawake wa dar town wanazo
 
Wenye mioyo ya kupenda kweli mbona karne hii hatuponi.Daaa.... Hapa bongo usiombe demu wako awe mweupe alfu angalau awe mrefu hata kidogo uone waleta mafuta watavyokuwa wengi.
 
  • Thanks
Reactions: LD
Tutafika, nakubaliana na wewe! Sasa kupiga mzinga 5lts za petrol mtu anaendesha audi? Haiingii akilini aisee! Manake sms tu ya 'darling nimeishiwa, sijui hata kama mafuta yatanifikisha home' ingetosha kuhusisha mpesa (kwa yule mwenye suzuki) ama sms banking kwa wenye audi na prado,lol!

Mnatafuta kutusakama tu! Hata sie tunahonga wapenzi wetu sana tu, lakini hatulalamiki! Mtoa mada wakaka hata wakichangishwa 11,000 tu kila mmoja wewe unalalamika! Kha!
 
Last edited by a moderator:
Wanawake wangekuwa kama wanaume sijui ingekuaje ile tabia ya kutongoza mpaka miaka 60, uzuri wao hapo alipo na kimini chake atazila za hao majamaa ila baada ya miaka kama mitano mbele kama asipou-control mwili wake na thamani yake inashuka hata wa kumwekea lita 2 atakosekana.

Ha ha ha ha ha ha ha.
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.
 
kwani tatizo ninini? kwanza sh almost ni kama 11200/= kweli inawatoa jasho na kuwafanya mpoteze muda kudiscuss.

wewe unapiga mznga ama unahongwa sh ngapi na madem zako? mbona siye huwa tunahonga sana tu?mbona hatulalamik? naboreka sana pale tunaposakamwa kwa mtu kuhongwa sh 33600/=na wanaume 3 tofauti na pia naona kma ni kweli bint hajui technique manake just an sms moja ya " hny ma dearest love you so much., ma gas tank is drained and i dont have enough banks sweetie" yaani in afraction of a minute lazima mpesa oe crdb cardless ma nmb pesa fasta ingehusu.
 
chezeiya daslam weye!!! mjini kuna wenyewe baba!
 
Na muda wote huo ulikua unamuangalia tu?
 
Wanawake wanajua sana kuchuna pesa mbele wapo kimslahi zaid
 
Story ya kutunga! "..magari hayasogei,.. kuikaja Aud..ikaja prado..ikaja benz.." ungeniambia ulikua nje ya folen unashuhudia angalau kidogo ungeeleweka japo nayo ingetia shaka kwani kwa hali halisi ya folen ya dar, kuwaita watu 3 toka sehemu tofauti wakaja inachukua muda mrefu

Hilo ndilo lililokuja kwenye kichwa changu, ni bora angetuambia yeye ni muuza miwa alikuwa pembeni ya barabara!
 
Mi nashindwa kuzielewa akili za wanawake,badala ya kuzungumzia ujinga wa huyo mwanamke mwenzao wa kushindwa kuwa mwaminifu wao wanaletj excuse. . . . . . . .. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Hapa mtoa mada hajazungumzia kiasi cha bei ya mafuta wala hela alizolipiwa mafuta.Pia hajazungumzia kuhongwa,yeye amezungumzia namna huyo mwanamke alivyo wa hovyo kwa kuwapanga wanaume!
 
Story ya kutunga! "..magari hayasogei,.. kuikaja Aud..ikaja prado..ikaja benz.." ungeniambia ulikua nje ya folen unashuhudia angalau kidogo ungeeleweka japo nayo ingetia shaka kwani kwa hali halisi ya folen ya dar, kuwaita watu 3 toka sehemu tofauti wakaja inachukua muda mrefu

Mkuu hapa kikubwa sio facts za kesi,kikubwa ni kwamba je tumejifunza nini tokana na hii riwaya?
Binafsi nimeshuhudia mara nyingi mwanamke ana collude na landlord na matokea yake wanaume wanne watano wanamlipia mwanamke kodi ya nyumba hiyo hiyo kisha hela wanagawana na mwenye nyumba,au mwanamke anauguliwa bili ya hospitali analipa bishanga Erickb52 na Asprin bila kujijua,mambo haya yapo aisee.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom