Barua ambayo AG ametuma Congress pamoja na kuwemo maoni ya AG na Deputy AG, imebeba summary ya 'principle conclusions' zilizofikiwa na Special Counsel mwenyewe na matokeo ya uchunguzi wake.
Russia Collusion Hoax ni Case Closed:
Page no.2 ya barua, paragraph ya pili, AG ametoa nukuu (quotation) kutoka kwenye ripoti ya Muller kwamba "The investigation did not establish that members of the Trump campaign conspired or coordinated with the Russian government in its election interference activities."
Hapo bado wengine wanasema kwamba furaha ya Trump ni kumalizika kwa uchunguzi! au taarifa ya Barr imepokewa kwa ubaridi na Republicans! Ama kwamba hiyo ni summary ya maoni ya AG Barr! Kazi kweli!
Kwa wanaoelewa, case ya Russia Collusion imeshindwa chali! Hata Democrats wenye akili zao hawaizungumzii.
Tukumbushe tu, Russia collusion hoax imechunguzwa mara nne kuanzia ilipoanza, walichunguza FBI wakahitimisha kuwa hamna kitu, wakaja Senate na House Intelligence Committees nao hola!, akamalizia Mueller naye hajaona ushahidi! Bado wengine wanasema hayo ni maoni ya AG na Deputy AG!!!! Amazing!
Kuhusu Obstruction of Justice:
Special Counsel ameshindwa kufikia hitimisho kuwa kulikuwa na 'Obstruction' kwa sababu ya kile alichokiita "difficult issues" kwenye sheria.
Kwa sheria, kanuni, na sera za DOJ, katika case kama hiyo, AG ndo anatakiwa atoe hitimisho na yeye na Rod Rosenstein wamehitimisha kuwa hakuna ushahidi wa kutosheleza wa Trump kupatikana na hatia! Mueller ni "Special Counsel" na sio "Independent Counsel" ndio maana anaripoti DOJ.
Sasa kunakuwaje na Obstruction of Justice by the President wakati hata hakushiriki katika kosa lenyewe analotuhumiwa nalo? Democrats wanaoelewa wanajua hapo hamna kitu!
Ripoti ya Mueller kuwekwa hadharani:
AG Barr amezungumzia hili nalo kwenye barua yake kwenda Congress. Kwa sheria, kanuni na sera za DOJ kuna taarifa ambazo zipo kwenye ripoti ya Mueller ambazo haziwezi kuwekwa wazi kwa mfano taarifa za "grand jury" zilizo kwenye uchunguzi na mshtaka ya jinai, kuna baadhi ya "executive priviledges" na taarifa za watu ambao hawakupatikana na hatia kwenye uchunguzi ambazo lazima zilindwe.
AG Barr amesema atafanya kazi na Mueller ili kutambua hizo taarifa na ku-process ripoti ya Mueller na kuitoa hadharani kulingana na sheria, kanuni na sera za DOJ.
AG Barr anachofanya ni kufuata sheria inasemaje. Kumuita Congress kufafanua ni siasa tu!
Democrats wanachotaka sio ripoti ya Mueller iwekwe hadharani kana kwamba kuna kitu kimefichwa na AG Barr! Hapana!.Democrats wanachotaka ni kutafuta chochote kwenye ripoti ya Mueller cha kuanzishia uchunguzi mwingine dhidi ya Trump ili kumuondoa madarakani (impeachment)! Kwa sababu wamesema waziwazi! Na hili hata Mitch McConnell na Republicans wanalifahamu.
Democrats hawana "talking points" kwenye uchaguzi wa 2020 ukizingatia Trump amefanya vizuri kwenye indicators zote za uchumi wa U.S. na ashaanza kupata hela za kujengea ukuta kutoka Pentagon.
Sent using
Jamii Forums mobile app