Duniani wawili wawili, Rais Magufuli kama Trump

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,854
35,861
Mabibi na mabwana inasemekana kila mtu kwa namna moja au nyingine hufanana na mtu mwingine angalau mmoja hapa duniani.

Ukimwangalia Trump jinsi alivyoshuighulikia misingi iliyokuwa inabeba utambulisho wa taifa la Marekani duniani kisha ukamwangalia Magufuli na iliyokuwa misingi ya utambulisho wa Mtanzania, haichukui muda mwingi kutambua kuwa wawili hawa ni baba mmoja, mama mmoja.

Kwamba leo Marekani kuna Rais ambaye walio wengi wana mtazamo ule walio nao kumwelekea yeye?

Kwamba leo Marekani pana Rais akifungua mdomo, hali ya hewa inaweza isitabirike?

Kwamba leo Marekani iliyokuwa mshirika muhimu katika amani, haki na Uhuru wa dunia wana rais asiyetabirika kiasi kile?

Kwamba leo rais wa Marekani akifungua mdomo hakuna ajuaye atakachosema kinaweza kuwa na madhara gani, kwa kiasi gani na hadi wapi?

Hiyo si Marekani iliyokuwa ikijulikana kama taifa kubwa, super power na custodian wa nguvu za nyuklia ambazo wapuuzi wengine hawakuruhusiwa kuwa nazo kwa usalama wa dunia yote.

Kwamba leo Tanzania tuliokuwa na ushawishi ule wa kuwafanya wengine duniani kujifunza kutoka kwetu, leo ndiyo hapa tulipo kidiplomasia?

Kwamba leo nchi hii ambayo hatukuwahi kuwa na mtu yeyote ukimbizini, leo hii wenzetu kwa usalama wa maisha yao ni heri wakatafuta hifadhi nje ya nchi na mapema iwezekanavyo?

Kwamba leo umuhimu wa kukaa mezani kutanzua tofauti zetu haupo tena. Ila marungu na risasi za moto za vyombo vya dola dhidi ya watu wasio na hatia?

Kwamba tuliokuwa machampioni wa kutetea haki za binadamu na kuwa wa kupigiwa mfano kote duniani, leo hii ndiyo tumekuwa wa kunyooshewa vidole kwa uvunjifu wa haki hizo uliopitiliza tokea duniani kote?

Kwamba leo chaguzi si zinazotupelekea kupata viongozi bali hao wanaweza kutangazwa hata wasipochaguliwa?

Kwamba badala ya uchaguzi kumekuwa ni vilio. Kuna waliokamatwa, kupigwa na hata kuuwawa na mamlaka katika jitihada zao za kutetea uhuru na haki tu katika uchaguzi huu?

Kwamba nini tusikie kwenye vyombo vya habari au nini tusome kwenye mitandao, limekuwa la kuamriwa na mamlaka? Kwamba Magufuli anatumia Twitter lakini hataki sisi tusikie wala kufika huko?

Tuliokuwa vinara wa kuhamasisha, kushawishi na hata kusimamia maridhiano kwingine, leo yametushinda. Tumekuwa watu kubebeana nyundo za chuma kuuwana bila ya huruma wala aibu?

Marekani kwao wameliona na kulitanzua bila ya kusubiri tena. Wameshamfunga paka kengele. Alipo kesha tulizwa kikasuku! Pongezi kwao kwa hilo zimetolewa tokea kwa viongozi wengi duniani na ati na Magufuli akiwamo.

Sisi Je? Aaaah Wapi!

Ni muhimu tukashirikiana sote akiwamo mh. Magufuli mwenyewe. Misingi ya utanzania wetu si ya kufanyiwa mchezo hata kidogo.

Kwa hakika misingi ya taifa letu tunalolipenda sote tuliyoachiwa na mwasisi wetu siyo hii tunayo iishi sasa!
 
Mjadala ambao unafanana na huu nimetaka kuuleta muda mrefu sana ila kuna sababu za msingi zimekuwa zinanikwamisha.

Kiufupi nadhani 'political strategists' wa CCM wangependelea zaidi Trump ashinde kuliko Biden.

Ila ngoja tuone itakavyokuwa.
 
Mjadala ambao unafanana na huu nimetaka kuuleta muda mrefu sana ila kuna sababu za msingi zimekuwa zinanikwamisha.

Kiufupi nadhani ' political strategists' wa CCM wangependelea zaidi Trump ashinde kuliko Biden. Ngoja tuone itakavyokuwa.
Wala hujakosea hata kidogo.
 
Wote wana hulka za udikteta, tamaa ya madaraka, na Pia ni wabaguzi!

Maslahi binafsi, wenyewe hutaka yachukuliwe kuwa ni ya kitaifa, na yeyote mwenye kufikiri tofauti, ni adui wa Taifa!

Kama ilivyokuwa nderemo na vifijo kwa Marekani bwana Trump alipokikwaa kisiki, hivyo hivyo itakuwa kwetu.
 
Endeleeni kuota
Ila kumbuka
Wiki iliyopita ilikuwa ya mafanikio kwa watu wawili wenye nguvu ya majina J
Joseph wa Tanzania
Joseph wa Marekani

Na mbaya kwa T
Trump
Tundu

Ukipenda boga usisahau na ua lake.

Ua lake ndiyo huo udikteta, ukanda, ukabila, ubinafsi, tamaa ya madaraka, ukandamizaji, fikira finyu (myopic), ushamba na yote ya namna hiyo aliyo nayo.

Usiache pia kuyapenda jombi ndiyo maua yake hayo.
 
Mabibi na mabwana inasemekana kila mtu kwa namna moja au nyingine hufanana na mtu mwingine angalau mmoja hapa duniani.
Duniani wawili wawili, Rais Magufuli kama Trump
Ila kuna tofauti kubwa moja katika kuzaliwa...moja alizaliwa mchana watu wakiwa macho huku mwenzake akizaliwa gizani watu wakiwa wamelala.
 
Hahaaahaa ha haaa. Labda kama ulimaanisha mmojawapo ni mwaanga!

Hiiii bagosha!

Amini nakwambia wote walikuwa "one term presidents."

Trump system ingekuwa kama kwetu leo angekuwa kazindua bunge na yule bwana angekuwa supika.

Hali kadhalika jiwe ingekuwa mambo hadharani, mbona angeshakata "one way ticket chattle" kwenda kuchunga ng'ombe na farasi wake?
 
Majina yenye mafanikio na yasiyo na mafanikio kutoka Tanzania Hadi Marekani

Majina yanayoanza na Herufi J, ndio yaliyofanikiwa

J = Jonhn Magufuli
J = Jo berden

Majina ambayo si ya kufanikiwa

Ni Herufi T"

T = Trampo
T = Tundu

Cc #Katakashekadm
 
Majina yenye mafanikio na yasiyo na mafanikio kutoka Tanzania Hadi Marekani

Majina yanayoanza na Herufi J, ndio yaliyofanikiwa

J = Jonhn Magufuli
J = Jo berden

Majina ambayo si ya kufanikiwa

Ni Herufi T"

T = Trampo
T = Tundu

Cc #Katakashekadm

Summary sahihi kuhusiana na hii mada ni kuwa Trump na Magu wanafanana sana:

"Wote wawili ni wavurugaji."

Chini ya Trump Marekani imerugwa na leo ilipo si Marekani tena. Utadhani Whitehouse kuliingia Morani. Kumevurugika hakuna mbele wala nyuma.

Tanzania chini ya jiwe hali ni hiyo hiyo. Kumeingia mshamba magogoni. Looh. Tanzania ya Nyerere (rip), katu siyo hii!

"Trump na jiwe wote hawa ni wavurugaji vurugaji tu"
 
Trump amefanikiwa sana kuboresha uchumi wa Marekani na kuongeza ajira kabla ya janga la corona, Huyu mwingine kwenye uchumi ni sifuri kabisa.
 
Mabibi na mabwana inasemekana kila mtu kwa namna moja au nyingine hufanana na mtu mwingine angalau mmoja hapa duniani.

Ukimwangalia Trump jinsi alivyoshuighulikia misingi iliyokuwa inabeba utambulisho wa taifa la Marekani duniani kisha ukamwangalia Magufuli na iliyokuwa misingi ya utambulisho wa Mtanzania, haichukui muda mwingi kutambua kuwa wawili hawa ni baba mmoja, mama mmoja.

Kwamba leo Marekani kuna Rais ambaye walio wengi wana mtazamo ule walio nao kumwelekea yeye?

Kwamba leo Marekani pana Rais akifungua mdomo, hali ya hewa inaweza isitabirike?

Kwamba leo Marekani iliyokuwa mshirika muhimu katika amani, haki na Uhuru wa dunia wana rais asiyetabirika kiasi kile?

Kwamba leo rais wa Marekani akifungua mdomo hakuna ajuaye atakachosema kinaweza kuwa na madhara gani, kwa kiasi gani na hadi wapi?

Hiyo si Marekani iliyokuwa ikijulikana kama taifa kubwa, super power na custodian wa nguvu za nyuklia ambazo wapuuzi wengine hawakuruhusiwa kuwa nazo kwa usalama wa dunia yote.

Kwamba leo Tanzania tuliokuwa na ushawishi ule wa kuwafanya wengine duniani kujifunza kutoka kwetu, leo ndiyo hapa tulipo kidiplomasia?

Kwamba leo nchi hii ambayo hatukuwahi kuwa na mtu yeyote ukimbizini, leo hii wenzetu kwa usalama wa maisha yao ni heri wakatafuta hifadhi nje ya nchi na mapema iwezekanavyo?

Kwamba leo umuhimu wa kukaa mezani kutanzua tofauti zetu haupo tena. Ila marungu na risasi za moto za vyombo vya dola dhidi ya watu wasio na hatia?

Kwamba tuliokuwa machampioni wa kutetea haki za binadamu na kuwa wa kupigiwa mfano kote duniani, leo hii ndiyo tumekuwa wa kunyooshewa vidole kwa uvunjifu wa haki hizo uliopitiliza tokea duniani kote?

Kwamba leo chaguzi si zinazotupelekea kupata viongozi bali hao wanaweza kutangazwa hata wasipochaguliwa?

Kwamba badala ya uchaguzi kumekuwa ni vilio. Kuna waliokamatwa, kupigwa na hata kuuwawa na mamlaka katika jitihada zao za kutetea uhuru na haki tu katika uchaguzi huu?

Kwamba nini tusikie kwenye vyombo vya habari au nini tusome kwenye mitandao, limekuwa la kuamriwa na mamlaka? Kwamba Magufuli anatumia Twitter lakini hataki sisi tusikie wala kufika huko?

Tuliokuwa vinara wa kuhamasisha, kushawishi na hata kusimamia maridhiano kwingine, leo yametushinda. Tumekuwa watu kubebeana nyundo za chuma kuuwana bila ya huruma wala aibu?

Marekani kwao wameliona na kulitanzua bila ya kusubiri tena. Wameshamfunga paka kengele. Alipo kesha tulizwa kikasuku! Pongezi kwao kwa hilo zimetolewa tokea kwa viongozi wengi duniani na ati na Magufuli akiwamo.

Sisi Je? Aaaah Wapi!

Ni muhimu tukashirikiana sote akiwamo mh. Magufuli mwenyewe. Misingi ya utanzania wetu si ya kufanyiwa mchezo hata kidogo.

Kwa hakika misingi ya taifa letu tunalolipenda sote tuliyoachiwa na mwasisi wetu siyo hii tunayo iishi sasa!
Mbona kama trump na lisu ndio Wana fanana vile mana wote wanaamin Demokrasi ni wao kushinda?
 
Back
Top Bottom