Kwa wenye vichwa viguku tu
Kitendo cha taarifa za maandamano kutolewa miezi miwili kabla hasa kwa Tanzania nikitendo chakimkakati sana na aliyekiratibu anaonekana siyo tu anaujua Tanzania na watanzania wake kwa kiwango cha hali ya juu sana ,unajua ni kwanini?
1. Watanzania wengi hawajazoea vurugu na hivyo ni watu wenye mioyoni yenye baridi sana so kuwafanya wawe chai nilazima uwapike kwa muda mrefu
2. Lengo la pili nikuhakikisha wanawaondoa CCM kwenye njia , hili kila mmoja ni shuhuda , wewe unaona campaign za mwaka huu zimefanyika kwa viwango vile ? Full mipasho badala ya kuuza sera 🤣 wanafiiia hadi kukodisha wa Mexico huko kinyume na miaka mingine huwa wanasimamaga watanzania halisi kuisemea serikali iliyopo madarakani ila mwaka huu diaspora wote wapo side B which is very bad sign kwa upande wa watawala.
3 Tatu na kwakuhitimisha , lengo la kutoa muda mrefu halikuwa na pengine halitupendezi wengi kuona serikali na Taifa letu likiingia kwenye machafuko , sasa unaweza unajiuliza ,ikiwa hivyo ndivyo sasa nini msingi wa kuratibuwa kwa hayo maandamano ? Swali zuri ,jibu lilikuwa nikuitishia serikali na kwakuwa muda uliwekwa mkubwa ili itengeneze uwezekano wa meza ya duara , serikali ilete hoja ya majadiliano itakayojikuta kwenye kutengeneza umoja wakitaifa .
So nini kitatokea ikiwa serikali itajifanya inaendelea kuweka pamba masikioni?
CCM itakuwa imejitambulisha kama adui rasmi hivyo watakuwa wamezipa sababu taasisi nyingi kuamua kuingilia kati kwa kuwa upande wa watawaliwa.
Ikiwa itafikia hatua hiyo ,amini nakwambia , CCM inakwenda kuondoka madarakani ndani ya masaa machache baada ya jamii kuingia barabarani maana pressure itakuwa ni kubwa kuliko matarajio .
Ondoa hofu kuhusu matishio ya askari hao unaosikilizishwa sauti zao , hao wenyewe washalegea na ukweli wanaujua .
Achana na mikwara ya Jeshi , hakuna pale mwenye uwezo wa kukomaa na chama corrupt kama CCM ,kwa wasiyojua hiyo fursa inatamaniwa na Jeshi kuliko wewe na mimi tunavyodhani .
Kisa walilolifanya serikali ya CCM nikuwaonjesha pesa wanajeshi wa ngazi za juu ,kitendo hicho kinatoa tafasiri kuwa sasa niwakati wetu wakujichotea badala ya kusubiri kuchotewa ,hivyo ni sawa na mkulima kumpa paka panya mwenye chumvi .
Nikuhakikishie tu , siku ikitokea watanzania wametoka ,CCM wajue rasmi washapoteza mamlaka ,maana hapo CDF atagawanya kikosi mara nne
1. Kikosi cha watetezi
2. kikosi cha usuruhishi bandia .
Kikosi cha kuongoza watawaliwa kugusa maeneo yatakayoilazimisha serikali ijisalimishe .
4 na Kikosi cha mwishonikile kitakacho torosha viongozi
Then game over