Dunia kusimama kuelekea mpambano wa kukata na shoka kati ya Anthony Joshua na Wladimir Klitschko

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Sep 7, 2016
17,446
21,140
Achana na lile pambano lililobatizwa jina la "Pambano la karne" kati ya mwanamasumbwi machachali ambaye hana historia ya kupigwa wala kutoa sare tangu aanze ngumi za kulipwa, ajulikanaye kama Floyd Mayweather anayecheza stance ya Orthodox na Manny Pacquao anayecheza staili ya Southpaw


Sasa basi pambano lingine la kukata na shoka linawajia ni kati ya bondia Anthony Joshua na bondia Wladimir Klitschko


Wote hawa wanacheza stance moja ambayo ni Orthodox ,na wote rekodi zao si haba


Anthony Joshua amecheza jumla ya mapambano 18 na yote ameshinda kwa K.O na Wladmir Klitschko amecheza jumla ya mapambano 68 ,53 kashinda kwa K.O na amepoteza mapambano 4 na hajawahi kutoa sare


Anthony Joshua ni Muingereza mwenye asili ya Afrika kutoka nchi ya Nigeria ,wakati Klitschko ni Mu Ukraine


Kadri siku zinavyozidi kwenda homa juu ya pambano lao linazidi kupanda,macho na maskio yote kwa mashabiki wa masumbwi yameleekezwa kwenye pambano lao litakalo pigwa 29 April 2017 Wembley Stadium


Screenshot_2017-03-17-20-50-06_1.jpg



Screenshot_2017-03-17-20-50-00_1.jpg



Screenshot_2017-03-17-20-49-51_1.jpg



Kumekuwa na mvutano mkubwa kati ya hawa mabondia wawili upande mmoja ukidai kuwa Anthony Joshua hana experience ya kutosha ya kucheza na Klitshko lakini wakati huo huo upande mwingine unapinga vikali suala hilo kutokana na rekodi nzuri anayozidi kuionesha AJ kwa kushinda mapambano yake yote kwa knockouts


Mashabiki wa AJ walienda mbali zaidi kwa kudai kuwa baada ya kumsambaratisha Klitschko watataka pambano na Tyson Furry mbabe wa Klitschko ili na yeye wamsambaratishe


Sasa je AJ ataendeleza record yake ya unbeaten au Wladmir atalinda heshima yake ya kutopigwa na mtoto?

Majibu yote haya tunayangojea kwa hamu 29 April
 
Yeeeah, hapo ndio patamu sasa.

Ila hapo Klitschko ana advatage sana kwa nini,

Kwanza jamaaa ana uzoefu wa mapambano mengi (68, nyani mzee kacheza mishale mingi) . Pili amesha cheza under presha na kupigwa pia so kisaikolojia anakuwa kajengeka vema kabisa, atakuwa anapanic uwanjani. Hata akiona anaelemewa na mchezo, ile spirit ya kuweza kubadilisha matokeo still atakuw nayo.

Pia DOGO naye pia anaweza ashinde maana ya kuwa na stronge reason ya yeye kupigana hadi tone la mwisho,

Kwanza ata taka ku prove kwa watu kuwa ukongwe sio ishu, still damu mpya inanguvu na ndio watawala wa game.

Pia ata taka linda reputation yake aliyo jijengea na record ya unbeaten aliyoiweka.

HAPO

MKONGWE NA MZOEF VS MLINDA RECORD....

Pambano tamu sanaAa
 
Yeeeah, hapo ndio patamu sasa.

Ila hapo Klitschko ana advatage sana kwa nini,

Kwanza jamaaa ana uzoefu wa mapambano mengi (68, nyani mzee kacheza mishale mingi) . Pili amesha cheza under presha na kupigwa pia so kisaikolojia anakuwa kajengeka vema kabisa, atakuwa anapanic uwanjani. Hata akiona anaelemewa na mchezo, ile spirit ya kuweza kubadilisha matokeo still atakuw nayo.

Pia DOGO naye pia anaweza ashinde maana ya kuwa na stronge reason ya yeye kupigana hadi tone la mwisho,

Kwanza ata taka ku prove kwa watu kuwa ukongwe sio ishu, still damu mpya inanguvu na ndio watawala wa game.

Pia ata taka linda reputation yake aliyo jijengea na record ya unbeaten aliyoiweka.

HAPO

MKONGWE NA MZOEF VS MLINDA RECORD....

Pambano tamu sanaAa
Kama lile pambano la floyd na pacquiao waliliita pambano la karne basi hili sio mbaya wangeliita pambano la decade
 
Muda unazidi kujongea tu ,wapenzi wa boxing wapate ile kitu roho inapenda
NALISUBIRI KWA HAMU SANA PAMBANO HILO
MKUU...BINAFSI MM BOXING NDYO MCHEZO NAUPENDA......NI VITASA TU MKUU NI PM NAMBA YAKO SHABIKI MWENZANGU

OVA
 
Kweli ngumi zimekosa wababe siku hizi yaani Wradimir toka enzi za kina lewis bado ana hadhi ya kupigana uzito wa juu??..dah..enzi zile wababe kibao huku tyson kule lewis huku bruno pale evander kule oliver macall huku rahman pale botha huku nani sijui yaani ilikua ni ubabe mpaka mtu unatetemeka kuangalia mechi..lkn siku hizi eti joshua na mzee gani sijui linaitwa pambano la kihistoria
 
Achana na lile pambano lililobatizwa jina la "Pambano la karne" kati ya mwanamasumbwi machachali ambaye hana historia ya kupigwa wala kutoa sare tangu aanze ngumi za kulipwa, ajulikanaye kama Floyd Mayweather anayecheza stance ya Orthodox na Manny Pacquao anayecheza staili ya Southpaw


Sasa basi pambano lingine la kukata na shoka linawajia ni kati ya bondia Anthony Joshua na bondia Wladimir Klitschko


Wote hawa wanacheza stance moja ambayo ni Orthodox ,na wote rekodi zao si haba


Anthony Joshua amecheza jumla ya mapambano 18 na yote ameshinda kwa K.O na Wladmir Klitschko amecheza jumla ya mapambano 68 ,53 kashinda kwa K.O na amepoteza mapambano 4 na hajawahi kutoa sare


Anthony Joshua ni Muingereza mwenye asili ya Afrika kutoka nchi ya Nigeria ,wakati Klitschko ni Mu Ukraine


Kadri siku zinavyozidi kwenda homa juu ya pambano lao linazidi kupanda,macho na maskio yote kwa mashabiki wa masumbwi yameleekezwa kwenye pambano lao litakalo pigwa 29 April 2017 Wembley Stadium


View attachment 482466


View attachment 482467


View attachment 482469


Kumekuwa na mvutano mkubwa kati ya hawa mabondia wawili upande mmoja ukidai kuwa Anthony Joshua hana experience ya kutosha ya kucheza na Klitshko lakini wakati huo huo upande mwingine unapinga vikali suala hilo kutokana na rekodi nzuri anayozidi kuionesha AJ kwa kushinda mapambano yake yote kwa knockouts


Mashabiki wa AJ walienda mbali zaidi kwa kudai kuwa baada ya kumsambaratisha Klitschko watataka pambano na Tyson Furry mbabe wa Klitschko ili na yeye wamsambaratishe


Sasa je AJ ataendeleza record yake ya unbeaten au Wladmir atalinda heshima yake ya kutopigwa na mtoto?

Majibu yote haya tunayangojea kwa hamu 29 April
Hili litakuwa pambano zuri...nani atashinda? Kwa kuwafatilia kimchezo, ni ngumu kusema...wote wanapigana kwa nidhamu, na kwa kupanga, na wote wako "combative"....litakuwa pambano, zuri, classic, na gumu...!
 
Wladimir atapigwa bila wasiwasi na AJ......ukiangalia pambano lake la mwisho na Tyson Fury hakufanya vizuri kabisa,inaonesha Vladimir ameshachoka baada ya kuwa kwenye ulingo kwa miaka Mingi.
Siamini kama uzoefu wake unaweza kumsaidia kumshinda AJ.....uzoefu utamsaidia kufika japo round ya 5 mpk saba.
Kwa upande wa AJ ....kwa sasa ndiye heavyweight boxer mwenye kila kitu. ...mkono wake wa kulia anajua kuutumia. Sio mzoefu kama Vladimir lkn hio kwake sio sababu maana tumeshuhudia mapambano yake yaliyopita pamoja na wazoefu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom