Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 17,415
- 21,110
Hii title ya Undisputed Champion kiuhalisia sidhani kama kuna bondia yeyote alishawahi kuipata.
Undisputed Champion ni yule bondia anayemiliki mikanda yote mikubwa zaidi kidunia ambayo kiidadi ipo minne ambayo ni WBC, WBA, WBO na IBF.
Mabondia wengi huishia kumiliki mikanda miwili au mitatu kati ya hiyo mikanda minne hivyo huishia kupata title ya Unified Champion.
Unified Champion ni yule bondia anayemiliki mikanda miwili au zaidi miongoni mwa mikanda hiyo minne (WBC, WBA, WBO na IBF) .
Mabondia wengi hushindwa kumiliki mikanda yote minne kwa sababu wengi hubadili uzito mara kwa mara (MF kutoka feather weight mpaka bantamweight,middle weight nk) .
Floyd isingekuwa kubadili uzito mara kwa mara ili apate mpinzani bora zaidi ili aingize pesa nyingi zaidi angekuwa tayari ameshapata hiyo Title ya Undisputed zamani sana kwa sababu title ya unified champion ameipata mara nyingi sana kwenye uzito tofauti tofauti ambao alikuwa anapigana (5 Weight Division), mpaka pambano lake na Manny Pacquiao ,Floyd alifanikiwa kumiliki mikanda mitatu (WBC,WBA na WBO )miongoni mwa hiyo minne hivyo alibakisha mmoja tu (IBF)ili kuwa Undisputed Champion ,
Sasa tukija upande wa heavyweight tunamuona bondia Anthony Oluwafemi Olaseni Joshua ukipenda muite Femi Boy au kwa kifupi AJ kama anavyojulikana na wengi, AJ anamiliki mikanda mitatu ambayo ni WBA,WBO na IBF hana mkanda mmoja tu ambao ni WBC ili akamilishe mikanda minne ili title ya Undisputed Champion.
Mkanda huo wa WBC unamilikiwa na Lineal Champion ambaye ni Tyson Fury ambaye amerudisha title hiyo ya U lineal baada ya kumtwanga bondia Deontay Wilder ,huku AJ yeye akiwa na title ya Unified Champion.
Kwa hiyo kitaalamu pambano tutasema Unified Champion vs Lineal Champion mshindi atakayepatikana atapata title ya Undisputed Champion.
Bondia AJ amekuwa akimkimbia Wilder mara kwa mara, alikuwa anasubiri tu Wilder apoteze pambano ili bondia atakayempiga Wilder apambane naye yeye na si yeye kumface Wilder moja kwa moja.
Hili limedhihirika baada ya pambano la pili kati ya Wilder na Tyson Furry ambapo Tyson aliibuka kidedea, team AJ wakiongozwa na promota wao Eddie Hearn walikuwa haraka sana kuhitaji pambano jambo ambalo halikuwa kawaida hapo mwanzoni.
Tyson Furry alituma kama ujumbe hivi kwenda team AJ baada ya kuonekana akitafuna Sticker yenye logo ya nchi ya Nigeria ambayo ndiyo asili ya Anthony Joshua kabla ya kubadili uraia.
Lakini mpaka sasa bado kuna sintofahamu katika pande zote mbili.
Kwa upande wa AJ, WBO waliagiza Alexander Usyka awe Mandatory Challenger dhidi yake baada ya Usyka ambaye ni bingwa wa WBO uzito wa Cruiserweight kuamua kupanda mpaka Heavyweight baada ya kumtwanga kwa Knockout swahiba wa Anthony Joshua ambaye ni Anthony Bellew.
Huyu bondia Anthony Bellew alishawahi kuwa trainer wa muda wa bondia Hassan Mwakinyo kwenye pambano lake lililofanyika Kenya chini ya udhamini wa Sportpesa.
Kwa upande wa Tyson Fury (Gypsy King) yeye mpaka sasa hajajulikana atapambana na nani maana kabla ya pambano ,WBC walitoa amri kwa bingwa atakayepatikana kwenye pambano lao atapambana na Mandatory Challenger ambaye ni Dillian Whyte.
Mbali na hilo, Deontay Wilder pia ameomba marudiano ya pambano la tatu (Trilogy Fight) jambo ambalo linauwezekano mkubwa kutokea kwa sababu promota wa Tyson Furry ambaye ni Bob Arum alifungua milango ya maombi kwa Team Wilder ndani ya siku 30 kama bado anahitaji
marudiano.
Bila kusahau huyu Bob Arum alishawahi kuwa promota wa Floyd Mayweather,Floyd alipomfukuza kazi na kuamua kusimamia mwenyewe mapambano yake,Bob Arum alienda kuwa promota wa Manny Pacquiao.
Floyd aliwahi kumshawishi Pacquiao amfukuze kazi Bob Arum kisha ajisimamie mwenyewe mapambano yake ili atengeneze pesa zaidi la sivyo ataendelea kunyonywa tu na Bob Arum.
Undisputed Champion ni yule bondia anayemiliki mikanda yote mikubwa zaidi kidunia ambayo kiidadi ipo minne ambayo ni WBC, WBA, WBO na IBF.
Mabondia wengi huishia kumiliki mikanda miwili au mitatu kati ya hiyo mikanda minne hivyo huishia kupata title ya Unified Champion.
Unified Champion ni yule bondia anayemiliki mikanda miwili au zaidi miongoni mwa mikanda hiyo minne (WBC, WBA, WBO na IBF) .
Mabondia wengi hushindwa kumiliki mikanda yote minne kwa sababu wengi hubadili uzito mara kwa mara (MF kutoka feather weight mpaka bantamweight,middle weight nk) .
Floyd isingekuwa kubadili uzito mara kwa mara ili apate mpinzani bora zaidi ili aingize pesa nyingi zaidi angekuwa tayari ameshapata hiyo Title ya Undisputed zamani sana kwa sababu title ya unified champion ameipata mara nyingi sana kwenye uzito tofauti tofauti ambao alikuwa anapigana (5 Weight Division), mpaka pambano lake na Manny Pacquiao ,Floyd alifanikiwa kumiliki mikanda mitatu (WBC,WBA na WBO )miongoni mwa hiyo minne hivyo alibakisha mmoja tu (IBF)ili kuwa Undisputed Champion ,
Sasa tukija upande wa heavyweight tunamuona bondia Anthony Oluwafemi Olaseni Joshua ukipenda muite Femi Boy au kwa kifupi AJ kama anavyojulikana na wengi, AJ anamiliki mikanda mitatu ambayo ni WBA,WBO na IBF hana mkanda mmoja tu ambao ni WBC ili akamilishe mikanda minne ili title ya Undisputed Champion.
Mkanda huo wa WBC unamilikiwa na Lineal Champion ambaye ni Tyson Fury ambaye amerudisha title hiyo ya U lineal baada ya kumtwanga bondia Deontay Wilder ,huku AJ yeye akiwa na title ya Unified Champion.
Kwa hiyo kitaalamu pambano tutasema Unified Champion vs Lineal Champion mshindi atakayepatikana atapata title ya Undisputed Champion.
Bondia AJ amekuwa akimkimbia Wilder mara kwa mara, alikuwa anasubiri tu Wilder apoteze pambano ili bondia atakayempiga Wilder apambane naye yeye na si yeye kumface Wilder moja kwa moja.
Hili limedhihirika baada ya pambano la pili kati ya Wilder na Tyson Furry ambapo Tyson aliibuka kidedea, team AJ wakiongozwa na promota wao Eddie Hearn walikuwa haraka sana kuhitaji pambano jambo ambalo halikuwa kawaida hapo mwanzoni.
Tyson Furry alituma kama ujumbe hivi kwenda team AJ baada ya kuonekana akitafuna Sticker yenye logo ya nchi ya Nigeria ambayo ndiyo asili ya Anthony Joshua kabla ya kubadili uraia.
Lakini mpaka sasa bado kuna sintofahamu katika pande zote mbili.
Kwa upande wa AJ, WBO waliagiza Alexander Usyka awe Mandatory Challenger dhidi yake baada ya Usyka ambaye ni bingwa wa WBO uzito wa Cruiserweight kuamua kupanda mpaka Heavyweight baada ya kumtwanga kwa Knockout swahiba wa Anthony Joshua ambaye ni Anthony Bellew.
Huyu bondia Anthony Bellew alishawahi kuwa trainer wa muda wa bondia Hassan Mwakinyo kwenye pambano lake lililofanyika Kenya chini ya udhamini wa Sportpesa.
Kwa upande wa Tyson Fury (Gypsy King) yeye mpaka sasa hajajulikana atapambana na nani maana kabla ya pambano ,WBC walitoa amri kwa bingwa atakayepatikana kwenye pambano lao atapambana na Mandatory Challenger ambaye ni Dillian Whyte.
Mbali na hilo, Deontay Wilder pia ameomba marudiano ya pambano la tatu (Trilogy Fight) jambo ambalo linauwezekano mkubwa kutokea kwa sababu promota wa Tyson Furry ambaye ni Bob Arum alifungua milango ya maombi kwa Team Wilder ndani ya siku 30 kama bado anahitaji
marudiano.
Bila kusahau huyu Bob Arum alishawahi kuwa promota wa Floyd Mayweather,Floyd alipomfukuza kazi na kuamua kusimamia mwenyewe mapambano yake,Bob Arum alienda kuwa promota wa Manny Pacquiao.
Floyd aliwahi kumshawishi Pacquiao amfukuze kazi Bob Arum kisha ajisimamie mwenyewe mapambano yake ili atengeneze pesa zaidi la sivyo ataendelea kunyonywa tu na Bob Arum.