DUNIA ITAZIKA WATU WAPI?

DUNIA ITAZIKA WATU WAPI?

Hamissi Hamza Jr

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2020
Posts
528
Reaction score
1,045
Waungwana Habarini Za Asubuhi

Kwamujibu Wa Takwimu za United Nations kwa Makadilio ya Mwaka Huu 2026 Dunia ina Jumla ya Zaidi ya Watu Billion 8.3 Na Inakadiliwa Itafikia Zaidi ya Watu Billion 10 Kufikia Mwaka 2050,

Makadilo Ya Sasa Ya Umri Wa Kuishi/Life Expectancy Kwa Dunia Ni Miaka 73 Na Kwa Tanzania Ni Miaka 67,

Kwa Makadilio Miaka 80 Ijayo Asilimia 95% Ya Watu Tuliopo Sasa Tutakua Hatupo,Je Dunia Itazika Wapi Watu Billion 8.3?

Swali Langu Huenda Likawa La Kipuuzi ila Lina Maana Ukitafakari,Watu Wanaongezeka Ardhi Haiongezeki,Unaweza Jibu Watapata pakuzikwa Maeneo ya Wengine waliozwika awali kwasababu Watukua Walishaoza Lakini Hilo Haliwezekani Kwasababu Makaburi yanajengelewa.

Nafikilia Dunia Itajengeka Sana kwa Majengo na Miundombinu ila Itafikia Wakati Kwa Miaka Ijayo Majengo na Miundombinu itabomolewa ili zipatilkane Nafasi za Wapendwa Waliondoka Duniani Kuzikwa.
 
AU imefika Wakati Wa Dunia Kufata/Kuiga Utaratibu Wa Wachina/Wahindi Kuchoma Miili Maana Waliona mbali?
 
Uwe unatembelea makaburini nyakati za kuchimba makaburi. Eneo moja linaweza tumika kuzika watu wengi tu kwa nyakati tofauti. ukitembelea eneo la makaburi ya zamani utagundua wanaanza kuchumbi makaburi mapya juu ya yale ya zamani ambayo hayana hata anayeenda kuyatembelea.
 
Naomba kuuliza Kuhusu Hili la Kuchomwa,wanaozika kwa kuchoma Baada ya kuchomwa Yale mabaki/Majivu Hua wanatupa au Yanazikwa?
Mengine yanazikwa na kupandwa mti juu yake
Mengine yanahifadhiwa nyumbani
Mengine yanatupwa majini
Mengine yanahifadhiwa makaburini
 
Pamoja na wingi wa watu hao lakini bado dunia imepwaya!

Watu wote wa Duniania pamoja na wingi wao ukiwaleta Tanzania,Bado Tanzania haitojaa na bado watapwaya!

Hakuna wa kuijaza dunia hadi wakakosa pakuzika!

Wala hupaswi kuwazia hilo!
 
Back
Top Bottom