Dunia inatutizama tunavyochezea Demokrasia

Dunia inatutizama tunavyochezea Demokrasia

MIGNON

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2009
Posts
4,114
Reaction score
5,114
Tangu baada ya uchaguzi wa 2015 ni ukweli usiofichika kuwa Demokrasia ya vyama vingi imepitia katika mtihani mkubwa.

Zuio la shughuli za kisiasa kwa vyama pinzani,hamahama ya waliochaguliwa toka upinzani kwenda kuunga mkono juhudi, kesi za hapa na pale, uondoaji wa viongozi wa kisiasa katika halmashauri au majiji yanayoongozwa na upinzani, ukosefu wa jukwaa huru kwa vyama vya upinzani kunadi sera zao na kadhalika.

Tuna miezi minne kabla ya uchaguzi na hakuna dalili za kuiboresha hali zaidi ya kuongeza hofu.

Wakati yote yanafanyika dunia imeelekeza taa yake kubwa kwetu (Makonda kuzuiwa kuingia USA) na mengine.

Tujitafakari na njia tunayochukua. Je, itakuwa na tija kwa Taifa letu?
 
Unataka demokrasia kama ile ya mababeberu mapolisi wanaoua watu hadharani?

Hatutaki demokrasia inayokuja na utamaduni wa Mabeberu, makonda amewekewa vikwazo Kwasababu aliwanyima mashoga ya Dar demokrasia kina Lissu wakaenda kumsemea.

Demokrasia yetu lazima izingatie utamaduni wetu
 
Unataka demokrasia km ile ya mababeberu mapolisi wanaoua watu hadharani ?

Hatutaki demokrasia inayokuja na utamaduni wa Mabeberu ,makonda amewekewa vikwazo Kwasababu aliwanyima mashoga ya dar demokrasia kina lissu wakaenda kumsemea

Demokrasia yetu lazima izingatie utamaduni wetu
Vipi kuhusu platform sawa kwa vyama vyote vya siasa?
 
Kwa hali ilivyo na muda uliobaki sidhani kama uchaguzi utakuwepo na hata kama ukiwepo tusitegemee kitu kinachoitwa UCHAGUZI katika uhalisia wake.

Jr
Uchaguzi lazima uwepo hilo halipongiki! Msitafute visingizio!.
 
Tangu baada ya uchaguzi wa 2015 ni ukweli usiofichika kuwa Demokrasia ya vyama vingi imepitia katika mtihani mkubwa.

Zuio la shughuli za kisiasa kwa vyama pinzani,hamahama ya waliochaguliwa toka upinzani kwenda kuunga mkono juhudi, kesi za hapa na pale, uondoaji wa viongozi wa kisiasa katika halmashauri au majiji yanayoongozwa na upinzani, ukosefu wa jukwaa huru kwa vyama vya upinzani kunadi sera zao na kadhalika.

Tuna miezi minne kabla ya uchaguzi na hakuna dalili za kuiboresha hali zaidi ya kuongeza hofu.

Wakati yote yanafanyika dunia imeelekeza taa yake kubwa kwetu (Makonda kuzuiwa kuingia USA) na mengine.

Tujitafakari na njia tunayochukua. Je, itakuwa na tija kwa Taifa letu?
Unanadi sera kipindi cha kazi na siasa zisha kwisha,siasa isubiri kipindi cha siasa,demokrasia kwanza ni kitu gani ktk bara la Africa maana na yenyewe ni njia ya kutufanya tuwe masikini tu, tunahangaika na demokrasia ktk bara masikini linalo hitaji kufanya kazi kwa bidii ili litoke kwenye umasikini ninyi mnatuambia kuna mdudu anaitwa demokrasia
 
Unanadi sera kipindi cha kazi na siasa zisha kwisha,siasa isubiri kipindi cha siasa,demokrasia kwanza ni kitu gani ktk bara la Africa maana na yenyewe ni njia ya kutufanya tuwe masikini tu, tunahangaika na demokrasia ktk bara masikini linalo hitaji kufanya kazi kwa bidii ili litoke kwenye umasikini ninyi mnatuambia kuna mdudu anaitwa demokrasia
Ni kweli kabisa uliyozungumza lakini nina maswali mawili,ni nani alitulazimisha tukubali siasa za vyama vingi?La pili ni wapi ambapo Maendeleo yalifanikiwa bila kuwa na demokrasia(Germany under Hitler-Miundombinu ya nguvu,uchumi mkubwa at last uka collapse na vita,Libya mpaka pesa ya kuolea unapewa na nyumba ya kuishi lakini bila demokrasia wameishia wapi,Urusi inameguka vipande vipande etc etc.)
 
Kila chama kipo huru ndio maana kule Chadema, Mbowe kapiga bilion 8 hakuna wa kumuuliza
Usimtaje Mbowe,Mbowe ni mtu mdogo sana katika Taifa hili.Tunaangalia Taifa sio individual kama Mbowe
 
Unataka demokrasia kama ile ya mababeberu mapolisi wanaoua watu hadharani?

Hatutaki demokrasia inayokuja na utamaduni wa Mabeberu, makonda amewekewa vikwazo Kwasababu aliwanyima mashoga ya Dar demokrasia kina Lissu wakaenda kumsemea.

Demokrasia yetu lazima izingatie utamaduni wetu
Ili mradi umechangia: tu?
 
Unataka demokrasia kama ile ya mababeberu mapolisi wanaoua watu hadharani?

Hatutaki demokrasia inayokuja na utamaduni wa Mabeberu, makonda amewekewa vikwazo Kwasababu aliwanyima mashoga ya Dar demokrasia kina Lissu wakaenda kumsemea.

Demokrasia yetu lazima izingatie utamaduni wetu
Kwn polisi wetu hawaui?? wa huku kwetu wakiua wanapandishwa na vyeo...au umesahau
 
Kosa lilianzia ktk nyakati za nyuma sana,na kosa hilo likirekebishwa leo tutakaa salama. Makosa makubwa matatu ni-:

1. Kukubali kuimega Africa badala ya kua moja

2. Kukubali elimu iliyo jaa misingi ya kigeni isiyo msaidia muafrika kua mtu mwenye uwezo wa kufikiri na kutenda na badala yake kua mtu tegemezi

3. Kukubali hiyo demokrasia ilihali haina maana sana ktk bara masikini

Tuna mambo makubwa ya kufanya kama kufanya kazi kwa bidii tukitumia ardhi tuliyonayo,kuondoa mipaka yote ya nchi na nchi na kuifanya Afrika kua moja yenye majimbo machache kama East Africa yote ikangozwa na Gavana mmoja, South pia ukijumuisha nchi zake zote na kwingineko isipokua tukawa na RAIS wetu mmoja.

Ok jambo hilo linaonekana ni gumu lakini ni lazima taratibu tuanze kuondoa fikra za kushindwa na hawa watu weupe na tuige baadhi ya viongozi wachache kama Magufuli, Ghadafi, Nkuruma,na wengine. Tukijikuta tunairudisha Africa kua moja na lugha moja haijalishi hata kama ni hicho hicho kingereza chao lakini utawaona wanaanza kuja kwa adabu na tutafanya nao biashara itokanayo na ardhi tuliyo nayo na tutafanikiwa sanaaaaa,mimi na wewe hatutakuwepo lakini vitukuu vyetu vitafurahia,tatizo letu tunatazama kesho tu badala ya kuitazama kesho kutwa yetu,watu wengi wanaopigia kelele demokrasia ni walafi tu wanao hitaji Ikulu kwa faida ya matumbo yao na familia zao,kabisa kabisa. Wala hatuna haja ya hiki kitu kinaitwa vyama vingi,vya nini?watu wanaacha kufanya kazi wanaongea siasa mitaani kutwa nzima
Ni kweli kabisa uliyozungumza lakini nina maswali mawili,ni nani alitulazimisha tukubali siasa za vyama vingi?La pili ni wapi ambapo Maendeleo yalifanikiwa bila kuwa na demokrasia(Germany under Hitler-Miundombinu ya nguvu,uchumi mkubwa at last uka collapse na vita,Libya mpaka pesa ya kuolea unapewa na nyumba ya kuishi lakini bila demokrasia wameishia wapi,Urusi inameguka vipande vipande etc etc.)
 
Tangu baada ya uchaguzi wa 2015 ni ukweli usiofichika kuwa Demokrasia ya vyama vingi imepitia katika mtihani mkubwa.

Zuio la shughuli za kisiasa kwa vyama pinzani,hamahama ya waliochaguliwa toka upinzani kwenda kuunga mkono juhudi, kesi za hapa na pale, uondoaji wa viongozi wa kisiasa katika halmashauri au majiji yanayoongozwa na upinzani, ukosefu wa jukwaa huru kwa vyama vya upinzani kunadi sera zao na kadhalika.

Tuna miezi minne kabla ya uchaguzi na hakuna dalili za kuiboresha hali zaidi ya kuongeza hofu.

Wakati yote yanafanyika dunia imeelekeza taa yake kubwa kwetu (Makonda kuzuiwa kuingia USA) na mengine.

Tujitafakari na njia tunayochukua. Je, itakuwa na tija kwa Taifa letu?
Mpaka Burudi wametuzidi demokrasia
 
Tatizo kubwa LA viongozi Wa nchi yetu Ni kukosa uzalendo Wa dhati kabisa toka moyoni.Dhambi kubwa wanayoifanya Ni kupuuza maagano ya taifa ikiwemo katiba ya taifa letu.viongozi Wa mihimili mikuu ya dola wameonyesha mfano mbaya Wa kuilinda Na kuitii katiba ya nchi yetu.Sio rais, spika wala jaji Mkuu, wote hao wamevunja katiba Na sheria ya nchi yetu kwa nyakati tofauti.Wasio Na hatia wamehukumiwa, wenye hatia wamesamehewa.Kangi lugola pamoja Na tuhuma zote za uhujumu uchumi yuko mtaani anakula bata, huku mdude nyagali na wengineo wamebambikiziwa kesi kisa tu kutofautiana mtazamo Na watawala. Mbaya zaidi vyombo vyetu vya dola vimegeuzwa vyombo vya kisiasa vya kutumiwa Na wanasiasa.Hakuna kitu kizuri kwa viongozi kama kujali haki za wenzako hata kama hawakuungi mkono.Huo ndo uzalendo Wa kweli.
 
Tatizo kubwa LA viongozi Wa nchi yetu Ni kukosa uzalendo Wa dhati kabisa toka moyoni.Dhambi kubwa wanayoifanya Ni kupuuza maagano ya taifa ikiwemo katiba ya taifa letu.viongozi Wa mihimili mikuu ya dola wameonyesha mfano mbaya Wa kuilinda Na kuitii katiba ya nchi yetu.Sio rais, spika wala jaji Mkuu, wote hao wamevunja katiba Na sheria ya nchi yetu kwa nyakati tofauti.Wasio Na hatia wamehukumiwa, wenye hatia wamesamehewa.Kangi lugola pamoja Na tuhuma zote za uhujumu uchumi yuko mtaani anakula bata, huku mdude nyagali na wengineo wamebambikiziwa kesi kisa tu kutofautiana mtazamo Na watawala. Mbaya zaidi vyombo vyetu vya dola vimegeuzwa vyombo vya kisiasa vya kutumiwa Na wanasiasa.Hakuna kitu kizuri kwa viongozi kama kujali haki za wenzako hata kama hawakuungi mkono.Huo ndo uzalendo Wa kweli.
Hakika umenena mkuu...
 
Tangu baada ya uchaguzi wa 2015 ni ukweli usiofichika kuwa Demokrasia ya vyama vingi imepitia katika mtihani mkubwa.

Zuio la shughuli za kisiasa kwa vyama pinzani,hamahama ya waliochaguliwa toka upinzani kwenda kuunga mkono juhudi, kesi za hapa na pale, uondoaji wa viongozi wa kisiasa katika halmashauri au majiji yanayoongozwa na upinzani, ukosefu wa jukwaa huru kwa vyama vya upinzani kunadi sera zao na kadhalika.

Tuna miezi minne kabla ya uchaguzi na hakuna dalili za kuiboresha hali zaidi ya kuongeza hofu.

Wakati yote yanafanyika dunia imeelekeza taa yake kubwa kwetu (Makonda kuzuiwa kuingia USA) na mengine.

Tujitafakari na njia tunayochukua. Je, itakuwa na tija kwa Taifa letu?

Makonda alizuiwa kwenda USA ni hasara kiasi gani tumepata kama nchi?
 
Kila chama kipo huru ndio maana kule Chadema, Mbowe kapiga bilion 8 hakuna wa kumuuliza
Mkuu ingekuwa vivo tusingeona vyombo vya dola vikihangaika kufanya kazi ya ccm badala ya nchi, muda wote mnahangaika kubambikia kesi wakosoaji Wa serikali mkitumia mahakimu wenu kina simba.
 
Km mtu ameuza madawa ya kulevya aachwe mtaani ?

Acheni kutetea jinai
Mkuu ingekuwa vivo tusingeona vyombo vya dola vikihangaika kufanya kazi ya ccm badala ya nchi, muda wote mnahangaika kubambikia kesi wakosoaji Wa serikali mkitumia mahakimu wenu kina simba.
 
Back
Top Bottom