Hivi kuna dhambi kubwa na ndogo?
Mbona mtu akidhini mnachukulia like big sin ila mtu akisema uongo, akiiba , asipowaheshimu wazazi wake mnachukulia poa tu!!!!
Mm nadhani hapa ndipo lilipo tatizo our perceptions abt sin.
Ni kweli inatazamiwa kiongozi wa kiroho lazima awe kioo cha jamii ili kumwakilisha Mungu anayemhubiri na kutaka jamii imfuate, lazima adhibitishe huyo Mungu anayeweza kuwasaidia wengine, amemsaidia yeye kwanza ili kuifanya imani kuwa ni zao la matendo na siyo nadharia tu.
Ila tukumbuke mifumo ya kuwapata hawa viongozi wa kidini ndiyo ina weaknesses sana, kwani ni mfumo wa kibinadamu wa kuwajaza maarifa na kuhtimu kama vile unafanya coz ya ufundi mwashi, ukishapata cheti regardless of motive behind tayari unaanza tumika madhabahuni.
Nachotaka ukione, paroko au mchungaji ni mtu kama wewe na wala usitegemee makubwa sana kutoka kwao, tunasaidiana wote ili tufikie malengo.
Neno la mungu ktk biblia kitabu kimoja cha injili kuna maneno kama haya
" mafalsayo na waandishi wameketi kwenye kiti cha Musa, wasikilizeni wanayofundisha ila msitende kwa kadri ya matendo yao.....
Pengine aliwaita viongozi vipofu.....
Hii inamaanisha kuwa msingi wa imani zetu lazima ujengwe kwenye mafundisho ya imani zetu na sio watu wafundishao imani zetu.
Nikishindwa kuizuia dhambi haina maana Yesu alishindwa na dhambi.
Yesu alikuja kutuokoa ss na dhambi zetu hivyo mwenye dhamana na imani yako ni yesu na wala si baba paroko.
Hivyo jitafakari huko wapi msingi wa imani yako?
Je ni kwa mchg au paroko?
Au ni kwa Mungu wako?