Dumu la lita 20 mafuta ya kupikia sasa ni Tshs 90,000, bado yanaenda juu

Kwa style tunayoenda nayo Magufuli lazma akumbukwe bila kupenda.

1. Tozo
2. Bei ya vitu kupaa
3. Serikali haina kauli 1 tena.
4. Wakazi wa Dodoma
5. Wenyeji wa Chato

Yaani mwanaume mwanaume tu. Wengi tulimchukia sana Magufuli lakini hata kama hatokumbukwa lakini kimoyo moyo lazma umkumbuke.
Ile hali ya JK imesharudi rasmi ndani ya utawala.
  • Toka serikali iliposema inafatilia mambo ya tozo hakuna mrejesho mpaka leo.
  • Toka tume ya kuchunguza kuungua kwa soko la Kariakoo hatujapata mrejesho wa tume hiyo na siku za nyongeza 7 walizopewa sasa tupo zaidi ya 21 hakuna wa kuuliza watu wako bize kusafiri tu.

Kweli sikumpenda JPM ila namkumbuka tu sio kama napenda ila nalazimika kumkumbuka.
We ni mjinga tu, alitupandishia bei ya mafuta,sukari na sembe ni fashisti mwenyewe, iweje leo useme ni Mama
 
Nakumbuka tukiwa watoto wazazi wetu walikuwa wanatengeneza mafuta ya kupikia kwa kutumia Samli. Pia walibanika samaki na kuchukua mafuta yake. Inabidi turudi kwenye uasili Kama kutupika kwa Samli n.k
Kimjini mjini haifai
 
We ni mjinga tu, alitupandishia bei ya mafuta,sukari na sembe ni fashisti mwenyewe, iweje leo useme ni Mama
Kwenye mada Umeona hoja 1 tu basi? Na umejuaje kama sikumkosoa JPM kwenye kasoro zake?
 
Tu
Lipa Kodi kwa maendeleo ya nchi yako,pesa inayopatikana kupitia shughuli hizo za bishara baadae utaona maji, umeme,nk

Tuwe wazalendo ndugu zangu.
Tunapenda sana kuwa wazalendo na hakika ni nia ya kila mtanzania kulipa kodi kwa mujibu wa sheria zinazohusu kodi.
Tatizo linakuja kwenye wasimamizi was hizi kodi zetu....wana sifa zifuatazo:
1. Wezi
2. Wabinafsi
3. Wanaturingishia
4. Wanatuona wazembe
5. Sio wazalendo.

In short ni MAFISI.....
 
Inflation!!hata ukiongeza watu mishahara,,hiyo nyongeza inaenda kununua vitu Vilevile.... Nashangaa NBS hawatoi statistics siku hizi
 
ni muhimu watawala wetu WALE VIZURI, WATEMBEELEEE MA V 8, WATIBIWE VIZURI WAO NA FAMILIA ZAO IKIBIDI WAENDE INDIA NA KULALA 5 STAR HOTELS HUKU WAKITIBIWA, WAISHI VIZURI ili waweze kutuletea maendeleo tusilalamike sana ..LAZIMA TUUMIE ILI NCHI IENDELEEE
 
hivi unauhakika wengi walimchukia JPM? wakati akifanya ziara mikoani ilikuwa ukiangalia, au mikutano yake. msiba wake uliona watu pamoja na viongozi waliomzika. TZ hakuna rais aliependwa kama JPM
Usiseme tz tu sema nchi nyingi zinazojua nini maana ya maendeleo walimpenda sana. Bora umesema wewe, ningesema mimi ningetukanwa kila tusi.
 
ni muhimu watawala wetu WALE VIZURI, WATEMBEELEEE MA V 8, WATIBIWE VIZURI WAO NA FAMILIA ZAO IKIBIDI WAENDE INDIA NA KULALA 5 STAR HOTELS HUKU WAKITIBIWA, WAISHI VIZURI ili waweze kutuletea maendeleo tusilalamike sana ..LAZIMA TUUMIE ILI NCHI IENDELEEE
Ni kweli kabisa tunasubiria LC300 soon mtaziona mtaani!
 
Ni kweli kabisa tunasubiria LC300 soon mtaziona mtaani!
801d4354-0323-4d5a-843d-03895cee0fa8.jpg
6f15b2ea-bd3a-406b-a1fd-fc985961fb60.jpg
3f47b2ae-cfea-4847-848f-3d1317b2cf3a.jpg
b4c07b5d-9bdf-4634-b4e5-b627ad2cc51f.jpg
62677992-14fa-428b-9024-5f1c926fb069.jpg
ba95acee-2709-4c48-a80a-760f3d5fcba4.jpg
 
We ni mjinga tu, alitupandishia bei ya mafuta,sukari na sembe ni fashisti mwenyewe, iweje leo useme ni Mama
Mafuta ya kupikia yamefika 90,000/- ..!!! Mrejesho wa hela zilizotoka BoT kati ya Januari hadi Machi 2021 kimyaaa..!!
 
Daah hatari kweli tunasumbuka na sukari na mafuta ya kupikia 2021 wenzetu wamepeleka rover sayari ya mars kuleta sample za mawe kutoka kule...
 
Back
Top Bottom