DSTV wapandisha bei


DORA Millioni 600 ndio nini mkuuu....
 
kisa na mkasa haswa cha kupandisha being nice nini
 
Hivi siwezi Kuchagua channels ninazotaka nikalipia hizo............?.......maana huwa situmiagi zote.........mimi sana sana ni Cheaters na Jerry Springer ..........hizo channel zinazoonyesha hizi show............zinaweza kuwa sh ngapi.........?.........
 
Binafsi huwezi kunitenganisha na DSTV' kwangu mimi Dstv ni shule...dunia ya leo naiona ndogo kama kijiji kwahajili ya Dstv.
Channel kama za Super Sport,CI, Dis ID,Cheaters na Natinal Geograghic channels ni moja ya starehe zangu za kila siku niwapo ofisini na nyumbani... Sisi wengine hata wakipandisha hadi laki mbili kwa mwezi tutahakikisha tunajibana kwenye matumizi mengine ili tukalipie Dstv. Dstv ni moja ya sehemu ya maisha yangu ya kila siku.
 
continental wanaonesha bure channel 24 ikiwepo Emmanuel tv, citizen, ktn aljazra....bbc ....france...cctv....voa....etc....sijawahi lipia hata centi

Tunachohitaji wenzako ni live football, hasa ligi ya Uingereza na hispania iliyosheheni mastaa kibao. Hizo channel ulizotaja si chochote kwa mpenda soka.
 

Kinachopandisha bei ya dstv ni live soccer siyo hizo channel unazotaja. Kama kweli huhitaji soka kwa nini uhangaike na DSTV?
 
Kinachopandisha bei ya dstv ni live soccer siyo hizo channel unazotaja. Kama kweli huhitaji soka kwa nini uhangaike na DSTV?

Nataka kuangalia tamthilia........sio lazima kila mtu apende mpira........nahitaji kuona.....My heart beats for Lola..... Saloni.....Laali......Hollywood Ex wives......Ellen DeGeneres show.......etc......
Khaaaaa.......
 
ligi ya uingereza imeuzwa kwa mabilion kwa sky na bt sports si ongezo hilo ni kuanzia msimu ujao si msimu huu ni majanga wakuuu ila naskia azam wanataka warushe epl

J kama Azam au mbadala wa Super Sport atafanikiwa kushusha bei??? Ikiwa kama yeye atakuwa mchuuzi wa TB na Sky Sport, na hata Supersport kwa ukanda huu wa A. Mashariki. Labda atoze kwa siku, wiki, na mwezi.
 
walitoa ofa ya vingamuzi vyao kwa elfu 99,000 kumbe wanakuja kufidia kwa kupandisha bei duh
 
Wenye hela za mawazo mtuachie wenye uwezo nyie nendeni huko STAR TIMES. Sisi tuendelee na yetu DSTV. Mpyuuuuuu........STAREHE GHARAMA. Unapenda starehe hela unaichungulia mfukoni nyie vipi? au mnafikir wao hizo channel wanapata bure? Wabaneni viongozi wenu kushuka kwa thamani ya "HELA YA MADAFU" dhidi ya Dola. Na hivi uchaguzi unakaribia tarajieni 1 USD = 3000 TSH. ndo mtajua MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA NI NINI!!!
 

Watu kama nyie ndio huangalia vibanda umiza hapa mnajishaua.
 
ligi ya uingereza imeuzwa kwa mabilion kwa sky na bt sports si ongezo hilo ni kuanzia msimu ujao si msimu huu ni majanga wakuuu ila naskia azam wanataka warushe epl

Kweli Azam wanataka kurusha epl na champions league na nyinginezo ila wanasafari ndefu sana kuwatoa hawa DSTV, na wanajua hilo! si leo wala kesho mkuu! tuendelee kuvumilia na kuomba miujiza itokee....
 
Kuwatoa pale walipo dstv ni safari ndefu
 
Kinachopandisha bei ya dstv ni live soccer siyo hizo channel unazotaja. Kama kweli huhitaji soka kwa nini uhangaike na DSTV?

Abeeee?!! Channel za Discovery na National Geographic tu baaas, soccer sina shida nayo hata kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…