Droo ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE 2021/22 kuchezeshwa MARCH 18, 2022 Switzerland

Joseverest

JF-Expert Member
Sep 25, 2013
51,991
69,385
Droo ya robo fainali, nusu fainali na fainali ya msimu wa 2021/22 UEFA Champions League zote zitachezeshwa katika tukio moja.


Timu nane zilizobakia zitajua hatma yao kwa mashindano hayo makubwa kwa ngazi ya klabu barani ulaya huko Jijini Nyon, Uswizi (Switzerland)


''It is at this stage that the draw opens up, with no seeding or country protection – that means that any of the eight teams can be drawn against one another.''

Fainali ya mashindano haya itafanyika katika uwanja wa Stade de France katika kitongoji cha jiji la Paris, Ufaransa na hii ni baaada ya Uwanja wa St Petersburg uliopo Urusi kunyang'anywa haki ya kuchezesha mchezo huo wa fainali, lakini suala la timu mwenyeji litaamuliwa kwa "sababu za kikanuni"

Soma pia: UEFA yahamisha fainali ya Champions League kutoka Urusi kwenda Ufaransa



Vitu ambavyo unatakiwa kujua:

Lini na wapi Droo ya robo fainali na nusu fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE itafanyika?

Droo ya michezo yote iliyobakia kwa msimu wa 2021/2022 itafanyika siku ya ijumaa 18 Machi 2022 katika makao makuu ya UEFA, Nyumba ya Mpira wa Ulaya, Nyon Uswizi kuanzia saa 5 asubuhi kwa saa za huko (11 am GMT) na saa saba/nane mchana hapa Tanzania




Nawezaje kuangalia hiyo draw ikifanyika?

uefa.com watarusha matangazo ya moja kwa moja ya kinachoendelea Uswizi

Ni klabu zipi zipo kwenye Droo hiyo?

Washindi nane wa hatua ya 16 bora ya Ligi ya mabingwa wamesonga mbele hatua ya robo fainali:


  1. Manchester City (Uingereza)
  2. Real Madrid (Hispania)
  3. Bayern (Ujerumani)
  4. Liverpool (Uingereza)
  5. Chelsea (Uingereza)
  6. Villarreal (Hispania)
  7. Benfica (Ureno)
  8. Atlético Madrid (Hispania)


Ni lini hatua ya robo fainali na nusu fainali ya Ligi ya mabingwa itafanyika?


Robo fainali


Mkondo wa kwanza: 5/6 April 2022

Mkondo wa pili : 12/13 April 2022

Nusu fainali

Mkondo wa kwanza: 26/27 April 2022

Mkondo wa pili: 3/4 May 2022

Ni lini fainali ya Ligi ya mabingwa wa ulaya 2021/2022?

Fainali ya Ligi ya mabingwa itafanyika siku ya Jumamosi 28/5/2022 Katika uwanja wa Stade de France, uliopo jijini Paris Ufaransa wenye uwezo wa kujaza watazamaji 80,698.

Nini mtazmo wako kuhusiana na hili? Nani kubeba ndoo
 
uefa.png
 
Dah! Natamani chama langu la The Roman Empire a.k.a Chelsea The Blues likutane na Benfica, ili tuanze mapema maandalizi ya Nusu Fainali kuelekea Fainali, na hatimaye kuchukua Ubingwa kwa mara ya 2 mfululizo.
 
Chelsea vs ATM

Real Madrid vs Villarreal

Bayern munich vs Liverpool

Man city vs Benfica
 
Back
Top Bottom