Dreamliner ATCL yatumwa Sudan

Dreamliner ATCL yatumwa Sudan

nikiona wanajeshi mi muda wote Naona kama wako ktk mateso hawana amani,sjui hata kwanini nawaoneaga Huruma!
 
1100491


Maafisa na Askari wa jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), wanaoshiriki Ulinzi wa Amani katika Jimbo la Darfur nchini Sudan kwa Mara ya kwanza kwa kipindi cha Miaka 10 ya Ulinzi wa Amani Jimboni humo wametumia Ndege ya Shirika la Ndege ya Serikali ya Air Tanzania.

Wamefanya hivyo ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu katika kulifanya Shirika hilo linapiga hatua zaidi kwa maslahi ya Shirika na Taifa kwa ujumla.
 
Kufa kufaana, wapigane ndege yetu ipate trip, nimekumbuka ishu ya mahindi!!
 
Hii habari mbona ya kitambo au umetoka leo kwa msamaha wa Rais!
 
That is a charter flight....Atcl itakuwa imekula hela ndefu kama hamna ufahamu na baadhi ya field bora upite kama upepo bila kutoa comment
Kwa hiyo hadi litokee dili jingine la kusafirisha wajeda au minofu ya sangara ndo litaruka, tuliwaambia acheni watu na makampuni binafsi wafanye biashara. mbona serikali ni mwanahisa kwenye makampuni kibao na wala haihusiki moja kwa moja kwenye management?
 
Vilevile Mhandisi Matindi aliongeza kuwa Ndege ya Dream Liner ina uwezo wa kusafiri kwa saa 12 bila kusimama, hivyo kwa kutumia saa tatu kusafiri kutoka hapa mpaka nchini Sudan ni sehemu ndogo ya Uwezo wake na ni nafasi ya kuwajaribisha watendaji wa Ndege wa ATCL katika kuhudumia safari Ndefu.

Hiyo para nmeelewa, maana ila kwa gharama Ni upumbavu kutumia ndege yetu maaana inaenda kurudi tupu,(wakati UN watakuwa wamelipia kwenda TU)........
Itarudi na maafisa na askari wa idadi hiyo waliomaza zamu yao huko Dufur
 
Nadhani lipo kwenye taratibu za mwisho kupewa jeshi kama ile ngalawa letu pendwa
 
Linayo na karibu litaanza, sasa hivi "lina-trot" kwanza


Hiyo route ni ya wapi Mkuu maana dege letu halieleweki,linapigwa pigwa picha tu likifanya kasafari kadogo
 
That is a charter flight....Atcl itakuwa imekula hela ndefu kama hamna ufahamu na baadhi ya field bora upite kama upepo bila kutoa comment
Hizo hela ndefu Nani anatoa!!?? Kwani UN hawana bajeti,hawajui Bei ya tikeki ya ndege dar to darfuu,hawajui idadi ya manajeshi wa tz wambao ambao watenda huko.............

Wao wametoa nauli ya ndege kufika darfuu, mitembea/basi/treni/gari binafsi juu yenu, ilimradi mfike darfuu kwa wakati....
 
Sipendi huu msemo "kuunga mkono juhudi" unapotumika hata kama ni kwenye jambo zuri mi huona kama ulaghai tu na kutafuta sifa
 
May 16, 2019
Dar -es-Salaam, Tanzania

Ndege ya ATCL aina ya Boeing 787 Dreamliner yaenda Sudan kupeleka wanajeshi ktk jimbo la Darfur kulinda amani. Boeing 787 Dreamliner ya ATCL ni ndege mahsusi ya abiria yenye uwezo wa kwenda masafa marefu lakini hii ni mara ya kwanza kushiriki ktk operesheni za kijeshi kwa ajili ya ulinzi wa amani.

Akizungumzia ushiriki wa Tanzania ktk kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa, mkuu wa operesheni na mafunzo ktk JWTZ, Major General Alfred Fabian Kapinga amesema huu ni mwaka wa 12 mfululizo toka Tanzania ihusike ktk kampeni za ulinzi wa amani chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa.

Tanzania ina vikosi chini ya Umoja wa Mataifa kulinda amani ktk nchi za Lebanon, Central African Republic, Sudan na DR Congo. Na katika kupeleka vikosi imekuwa ikitumia ndege za JWTZ na zingine zilizokodishwa na Umoja wa Mataifa. Hii ni mara ya kwanza ATCL kutumika na kutakuwepo mwendelezo wa ATCL kutumika ktk misheni za ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa ATCL amesema wamefarijika shirika kupata tenda ya Umoja wa Mataifa kusafirisha walinzi wa amani. Amelishukuru jeshi JWTZ na wadau wengine waliofanikisha kupata kazi hii inayoshindaniwa na mashirika mengi ya ndege duniani ktk kufanya kazi za Umoja wa Mataifa.
Linaingiza faida?
 
Back
Top Bottom