May 16, 2019
Dar -es-Salaam, Tanzania
Ndege ya ATCL aina ya Boeing 787 Dreamliner yaenda Sudan kupeleka wanajeshi ktk jimbo la Darfur kulinda amani. Boeing 787 Dreamliner ya ATCL ni ndege mahsusi ya abiria yenye uwezo wa kwenda masafa marefu lakini hii ni mara ya kwanza kushiriki ktk operesheni za kijeshi kwa ajili ya ulinzi wa amani.
Akizungumzia ushiriki wa Tanzania ktk kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa, mkuu wa operesheni na mafunzo ktk JWTZ, Major General Alfred Fabian Kapinga amesema huu ni mwaka wa 12 mfululizo toka Tanzania ihusike ktk kampeni za ulinzi wa amani chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa.
Tanzania ina vikosi chini ya Umoja wa Mataifa kulinda amani ktk nchi za Lebanon, Central African Republic, Sudan na DR Congo. Na katika kupeleka vikosi imekuwa ikitumia ndege za JWTZ na zingine zilizokodishwa na Umoja wa Mataifa. Hii ni mara ya kwanza ATCL kutumika na kutakuwepo mwendelezo wa ATCL kutumika ktk misheni za ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa ATCL amesema wamefarijika shirika kupata tenda ya Umoja wa Mataifa kusafirisha walinzi wa amani. Amelishukuru jeshi JWTZ na wadau wengine waliofanikisha kupata kazi hii inayoshindaniwa na mashirika mengi ya ndege duniani ktk kufanya kazi za Umoja wa Mataifa.
Dar -es-Salaam, Tanzania
Ndege ya ATCL aina ya Boeing 787 Dreamliner yaenda Sudan kupeleka wanajeshi ktk jimbo la Darfur kulinda amani. Boeing 787 Dreamliner ya ATCL ni ndege mahsusi ya abiria yenye uwezo wa kwenda masafa marefu lakini hii ni mara ya kwanza kushiriki ktk operesheni za kijeshi kwa ajili ya ulinzi wa amani.
Akizungumzia ushiriki wa Tanzania ktk kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa, mkuu wa operesheni na mafunzo ktk JWTZ, Major General Alfred Fabian Kapinga amesema huu ni mwaka wa 12 mfululizo toka Tanzania ihusike ktk kampeni za ulinzi wa amani chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa.
Tanzania ina vikosi chini ya Umoja wa Mataifa kulinda amani ktk nchi za Lebanon, Central African Republic, Sudan na DR Congo. Na katika kupeleka vikosi imekuwa ikitumia ndege za JWTZ na zingine zilizokodishwa na Umoja wa Mataifa. Hii ni mara ya kwanza ATCL kutumika na kutakuwepo mwendelezo wa ATCL kutumika ktk misheni za ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa ATCL amesema wamefarijika shirika kupata tenda ya Umoja wa Mataifa kusafirisha walinzi wa amani. Amelishukuru jeshi JWTZ na wadau wengine waliofanikisha kupata kazi hii inayoshindaniwa na mashirika mengi ya ndege duniani ktk kufanya kazi za Umoja wa Mataifa.
