Kwani mkuu unafikiri watumishi wa umma hawana vyama? Akikosa nafasi ya kisiasa anarudi kwenye utendaji ambacho hakiruhusiwi ni kuonesha maslahi ya Chama kwenye utendaji basi.
Naweza kuamini kuwa sasa umeshaanza kunogewa na vyeo. Ulianza kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Ukafuata kuwa kiongozi wa Kamati ya Bunge Maalum la Katiba. Kama hiyo haitoshi, ukateuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Sasa unataka Uspika wa Bunge.
Ukiwa ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, hukupaswa kujitokeza kisiasa na kugombea Uspika wa Bunge. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali si mtu mdogo. Ndiye Kaimu Mwanasheria Mkuu wa Serikali pale ambapo Bunge hufanyika kwakuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali huwa Bungeni Dodoma. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mtu wa kitaifa zaidi.
Kujianikaanika kama kada wa CCM si jambo jema wala vutizi. Kutakuwa na kitu na watu wanaosababisha. Nani kakutuma? Unataka nini hasa? Kwanini? Dr. Tulia, umejianika kama kada. Watumishi wa Ofisi yako na wananchi kwa ujumla watakuonaje ikiwa utaendelea kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali?
Ili kulinda heshima yako, jiuzulu Unaibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na urejee Shule Kuu ya Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ukahadhiri pale ambapo Uspika utagoma kupatikana. Ujiuzulu haraka!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Haya sasa kelele hizi ziishe rasmi!.
![]()
Uteuzi huu ni salaam za rais , Dr.John Pombe Joseph Magufuli kwa wabunge wa CCM kuwa anamtaka nani awe spika mpya wa Bunge!.
Hongera sana Dr. Tulia kwa kuwa mbunge wa kwanza wa kuteuliwa na rais na Spika Mpya (in waiting) wa Bunge la 11 la JMT!.
Pasco
Kuwa mwanasheria mkuu hakuzuii mtu kuwa mwanachama wa chama cha siasa. Tukisema tumilike hayo mambo ya kadi za chama...wapo majaji wa kichaga wana kadi za CHADEMA. Hapo vipi sasa?
Kitu unazungumza.
Kwani CHADEMA inawateua kushika nyadhifa za kiserikali? Elewa mada. Elimu elimu elimu
Eti... elimi elimu elimu....... Mwenzenu alijua kuwa hamna ndio maana akaja nayo kuwasaidia watu wa aina yako. mnafikri wote tu akili kama zenu. Wenzenu tunayo. Tunajitambua tangu zamani.
Sasa hivi huishi kumsifiaNaweza kuamini kuwa sasa umeshaanza kunogewa na vyeo. Ulianza kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Ukafuata kuwa kiongozi wa Kamati ya Bunge Maalum la Katiba. Kama hiyo haitoshi, ukateuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Sasa unataka Uspika wa Bunge.
Ukiwa ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, hukupaswa kujitokeza kisiasa na kugombea Uspika wa Bunge. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali si mtu mdogo. Ndiye Kaimu Mwanasheria Mkuu wa Serikali pale ambapo Bunge hufanyika kwakuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali huwa Bungeni Dodoma. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mtu wa kitaifa zaidi.
Kujianikaanika kama kada wa CCM si jambo jema wala vutizi. Kutakuwa na kitu na watu wanaosababisha. Nani kakutuma? Unataka nini hasa? Kwanini? Dr. Tulia, umejianika kama kada. Watumishi wa Ofisi yako na wananchi kwa ujumla watakuonaje ikiwa utaendelea kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali?
Ili kulinda heshima yako, jiuzulu Unaibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na urejee Shule Kuu ya Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ukahadhiri pale ambapo Uspika utagoma kupatikana. Ujiuzulu haraka!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)