Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,172
Kuna tetesi kuwa Dr. Slaa atamaliza kampeni zake kwa Sugu (Mbeya Mjini).
Yuko sahihi.
Lakini chondechonde Dokta. Usiache kwenda jimbo la Songwe. Watu wa jimbo la Songwe nadhani wamerogwa kama si kulaaniwa.
Jimbo la Songwe ni jimbo masikini kuliko yote mkoa wa Mbeya. (Kuna dhahabu. Wamepigwa marufuku kulima pamba, japo ni zao linalostawi huko. Wamekubali kijinga). Elimu hovyo, barabara hovyo, afya hovyo, kipato cha mtu mmoja-mmoja hovyo, maji hovyo. Taja kila kitu cha hovyo, utakipata jimbo la Songwe.
Kuna wakati walikuwa na mbunge anaitwa Ntwina. Jamaa ana kiburi. Hazungumzi kitu bungeni kama EL. Akizungumza anazungumza pumba. Kuna kipindi alileta utapeli. Akajifanya analeta umeme. Akarundika nguzo kipindi chote cha awamu ya pili ya Mkapa. Hakuna umeme. Wananchi wakapandwa hasira. Wakazichoma moto nguzo za umeme. Nikadhani labda wamepata somo. Kipindi cha Awamu ya kwanza ya JK, wakachagua mbunge mwingine. Kama kawaida. Tapeli. Amepigwa chini uchaguzi huu. Kinachonishangaza ni kwamba wameshindwa kujua kuwa tatizo siyo wabunge wanaowachagua.....tatizo ni CCM. Hapo ndipo tatizo lipo. Heri wanaopewa hongo ya fulana; hawa wakwetu wanahongwa mataputapu. Aibu!
(Ukiondoa familia yetu) Hawa jamaa wamerogwa kama si kulaaniwa. Nasikia wamepitisha mbunge wa CCM bila kupingwa.
Dr. Slaa naomba upite huko. Japo dakika 15. Kura ya baba ni ya kwako 100%. Usijali naomba uende. Japo hutaenda, utakapokuwa Mbeya, lipe jimbo la Songwe japo aya moja kwenye hotuba yako maridhawa.
Pamoja tutaikomboa Tanzania.
Yuko sahihi.
Lakini chondechonde Dokta. Usiache kwenda jimbo la Songwe. Watu wa jimbo la Songwe nadhani wamerogwa kama si kulaaniwa.
Jimbo la Songwe ni jimbo masikini kuliko yote mkoa wa Mbeya. (Kuna dhahabu. Wamepigwa marufuku kulima pamba, japo ni zao linalostawi huko. Wamekubali kijinga). Elimu hovyo, barabara hovyo, afya hovyo, kipato cha mtu mmoja-mmoja hovyo, maji hovyo. Taja kila kitu cha hovyo, utakipata jimbo la Songwe.
Kuna wakati walikuwa na mbunge anaitwa Ntwina. Jamaa ana kiburi. Hazungumzi kitu bungeni kama EL. Akizungumza anazungumza pumba. Kuna kipindi alileta utapeli. Akajifanya analeta umeme. Akarundika nguzo kipindi chote cha awamu ya pili ya Mkapa. Hakuna umeme. Wananchi wakapandwa hasira. Wakazichoma moto nguzo za umeme. Nikadhani labda wamepata somo. Kipindi cha Awamu ya kwanza ya JK, wakachagua mbunge mwingine. Kama kawaida. Tapeli. Amepigwa chini uchaguzi huu. Kinachonishangaza ni kwamba wameshindwa kujua kuwa tatizo siyo wabunge wanaowachagua.....tatizo ni CCM. Hapo ndipo tatizo lipo. Heri wanaopewa hongo ya fulana; hawa wakwetu wanahongwa mataputapu. Aibu!
(Ukiondoa familia yetu) Hawa jamaa wamerogwa kama si kulaaniwa. Nasikia wamepitisha mbunge wa CCM bila kupingwa.
Dr. Slaa naomba upite huko. Japo dakika 15. Kura ya baba ni ya kwako 100%. Usijali naomba uende. Japo hutaenda, utakapokuwa Mbeya, lipe jimbo la Songwe japo aya moja kwenye hotuba yako maridhawa.
Pamoja tutaikomboa Tanzania.