Sote tunalifahamu hili. Lakini kwa kukumbushana tu, Dr. Aliondoka CHADEMA kwa sababu ya Ukaribisho wa Lowasa ambao ulikuwa ni kinyume na utashi wake. Hoja kuu ilikuwa kwamba Lowasa ni fisadi na hakupashwa kutendewa na upinzani namna alivyotendewa.
Dr Slaa hakuishia kuondoka tu, bali pia alikwenda hatua moja mbele ya kusaliti upinzani na kupigia kampeni Chama Cha Mapinduzi akiamini kwamba kwa kuondoka kwa LOwasa, basi ufisadi umekwisha ccm. Bila shaka aliamini kwamba yeye na CCM sasa watakuwa wakiongea lugha moja, wakitembea njia moja, na kushare vision.
Lakini hivi punde, Mwenyekiti wa CCM ametamka suala linaloonyesha kwamba Lowasa hana hatia yoyote na anastahili kuenziwa kwa mambo makuu aliyolifanyia taifa hili.
Ninaomba kusikia kutoka kwa Dr. Slaa. Nini msimamo wako Dr kwa sasa, juu ya ubia wako na ccm, ccm inayotangaza kumuenzi Lowasa kwa kuwa ni mtu safi, mtu safi kwa rafiki zako CCM ambao umeingia nao ubia wa imani ambao wanamsifu mtu unayeamini ni mbaya kiasi cha kubadilisha kwa sehemu kubwa ndoto za maisha yako?
Uliamini wa haraka haraka kwamba CCM without Lowasa ni takatifu. CCM hiyo hiyo inatangaza kumuenzi Lowasa kwa ubora wake. Unajisikiaje baada ya hapa?
CCM wote, semeni, Lowasa ni fisadi ama si fisadi?
Dr Slaa hakuishia kuondoka tu, bali pia alikwenda hatua moja mbele ya kusaliti upinzani na kupigia kampeni Chama Cha Mapinduzi akiamini kwamba kwa kuondoka kwa LOwasa, basi ufisadi umekwisha ccm. Bila shaka aliamini kwamba yeye na CCM sasa watakuwa wakiongea lugha moja, wakitembea njia moja, na kushare vision.
Lakini hivi punde, Mwenyekiti wa CCM ametamka suala linaloonyesha kwamba Lowasa hana hatia yoyote na anastahili kuenziwa kwa mambo makuu aliyolifanyia taifa hili.
Ninaomba kusikia kutoka kwa Dr. Slaa. Nini msimamo wako Dr kwa sasa, juu ya ubia wako na ccm, ccm inayotangaza kumuenzi Lowasa kwa kuwa ni mtu safi, mtu safi kwa rafiki zako CCM ambao umeingia nao ubia wa imani ambao wanamsifu mtu unayeamini ni mbaya kiasi cha kubadilisha kwa sehemu kubwa ndoto za maisha yako?
Uliamini wa haraka haraka kwamba CCM without Lowasa ni takatifu. CCM hiyo hiyo inatangaza kumuenzi Lowasa kwa ubora wake. Unajisikiaje baada ya hapa?
CCM wote, semeni, Lowasa ni fisadi ama si fisadi?