Dr. Slaa, tuombe radhi CCM kwa kuita chama choo

Dr. Slaa, tuombe radhi CCM kwa kuita chama choo

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Pamoja na kutufarahisha kwa hotuba yako,unapaswa kutuomba radhi. Wengi wetu wamechekelea makombora ya hasara kwa Lowassa na wenzake ndani ya CHADEMA. Sasa Dr. Slaa ni lulu chamani na anapendwa kwelikweli.

Sasa anamiminiwa sifa na airtime ya kutosha. Leo ataunguruma tena. Kwa hapo,tunamshukuru na kumpenda. Lakini,anapaswa kutuomba radhi wanachama wa CCM.Hawezi kuachwa hivihivi.

Dr. Slaa ameiita CCM choo. Yaani nyumba ya uchafu mkuu. Yaani sisi ni maggots kwakuwa tupo kwenye kinyesi chooni. Haiwezekani. Haikubaliki. Ajitokeze mara moja kutuomba msamaha. Ama sivyo,tutamtenga!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Aombe radhi pia kwa kuihusisha CCM na ufisadi kwa miaka yote,kwa sababu CCM sio mafisadi wala hawajawahi kuwa na kashfa yoyote ya kifisadi ukitoa ile ya iliyomuhusisha yule Nyota ing'aayo alieingia UKAWA ambaye yeye Slaa ndio ametuambia ndieye fisadi pekee nchini(satire)
 
Pamoja na kutufarahisha kwa hotuba yako,unapaswa kutuomba radhi. Wengi wetu wamechekelea makombora ya hasara kwa Lowassa na wenzake ndani ya CHADEMA. Sasa Dr. Slaa ni lulu chamani na anapendwa kwelikweli.

Sasa anamiminiwa sifa na airtime ya kutosha. Leo ataunguruma tena. Kwa hapo,tunamshukuru na kumpenda. Lakini,anapaswa kutuomba radhi wanachama wa CCM.Hawezi kuachwa hivihivi.

Dr. Slaa ameiita CCM choo. Yaani nyumba ya uchafu mkuu. Yaani sisi ni maggots kwakuwa tupo kwenye kinyesi chooni. Haiwezekani. Haikubaliki. Ajitokeze mara moja kutuomba msamaha. Ama sivyo,tutamtenga!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Ni falsafa yake tu na kimsingi hakuna zambi kuhusu hilo.ni uamuzi wa mtu kutafsili apendavyo.
 
Habari za Slaa zimechosha sasa, hakuna jipya.
 
sasa kama ameamua kuwa mgombea binafsi si aanze kampeni nchi nzima.
 
Katika watu wenye furaha duniani kwa sasa ni Nape Nnauye.
Huyu bwana alimtukana matusi yote Dr na majina yote alimwita, alibakiza kumwita majina ya wanyama tuu.
Sasa wakati huu ambao Nape anakabiliwa na jukumu la kuhakikisha kule Mtama anafanikiwa kuupata ubunge, huku nyuma yule mzee aliyekuwa ana mtukana na kumkebehi ameamua kumfanyia kazi ile ya propaganda kwa nguvu mpya kabisa.
Kwa nini Nape asiwe na furaha maana yale tuu ya Mtama pekee yalikuwa yanamsumbua.
 
Watu wameanza kuhoji ilikuwaje Padre Slaa akapewa Ukatibu Mkuu wa TEC? maana yanayojiri sasa hayaonyeshi kama amewahi kupitia mafunzo ya KITUME, unless kuwe na ajenda ya siri kati ya KANISA na CCN!
 
dr slaa anatembea na orodha ya mafisadi wake 11 na juzi jnne alimchambua mmoja aliyehama, leo ataanza kuwachambua hao 10 waliobaki huko anakotaka kwenda
 
Pamoja na kutufarahisha kwa hotuba yako,unapaswa kutuomba radhi. Wengi wetu wamechekelea makombora ya hasara kwa Lowassa na wenzake ndani ya CHADEMA. Sasa Dr. Slaa ni lulu chamani na anapendwa kwelikweli.

Sasa anamiminiwa sifa na airtime ya kutosha. Leo ataunguruma tena. Kwa hapo,tunamshukuru na kumpenda. Lakini,anapaswa kutuomba radhi wanachama wa CCM.Hawezi kuachwa hivihivi.

Dr. Slaa ameiita CCM choo. Yaani nyumba ya uchafu mkuu. Yaani sisi ni maggots kwakuwa tupo kwenye kinyesi chooni. Haiwezekani. Haikubaliki. Ajitokeze mara moja kutuomba msamaha. Ama sivyo,tutamtenga!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
We nawe. Waambie kwanza CHADEMA wamuombe msamaha Lowassa kwa kumwita joka la mdimu king maker wa ufisadi hapa nchini. Na wakimaliza hapo waende tena wakapige magoti kwa Sumaye mtu waliyekuwa wanamwita kuwa ni waziri mkuu bomu kabisa aliyewahi kutokea katika nchi yetu, Fisadi na ambaye serikali yake ilisimamia mauaji ya Waislam wasiokuwa na hatia kule Zanzibar. Na wakimaliza hapo wahamie kwa......The list goes on and on. Kimsingi ninachotaka kusema ni kwamba hoja yako haina mashiko na ni ule ule ushabiki tuliouzoea siku zote!
 
Dunia adaa! Kwa hakika na ninasema kutoka moyoni mwangu sikujua kama Dr W. Slaa anaweza kuonesha umbea wa kike wenza kwa namna hii katika macho ya kadamnasi.
Shikamoo Dr. Slaa. Koleo waliita koleo. Matusi yetu yasikutishe. Ogopa auaye mwili na roho usiogope auaye mwili tu. Kama kuna mahali umekosea omba toba kwa aliyetuumba,ukisimamia kweli usiogope. Yohana aliuawa kwa kumwambia mfalme dhambi yake. Stephano alikufa kwa kusimamia ukweli. Mwokozi Wetu aliwambwa mtini na aliowapa mkate,tiba na toba.Hakulipiza aliwaombea msamaha.Baki na Kriso hutapotea milele.
 
Slaa ndio nani?. Nisaudieni jamani
 
Shikamoo Dr. Slaa. Koleo waliita koleo. Matusi yetu yasikutishe. Ogopa auaye mwili na roho usiogope auaye mwili tu. Kama kuna mahali umekosea omba toba kwa aliyetuumba,ukisimamia kweli usiogope. Yohana aliuawa kwa kumwambia mfalme dhambi yake. Stephano alikufa kwa kusimamia ukweli. Mwokozi Wetu aliwambwa mtini na aliowapa mkate,tiba na toba.Hakulipiza aliwaombea msamaha.Baki na Kriso hutapotea milele.

Abaki na Kristo na pia ahakikishe anaomba toba ya kutelekeza damu yake mwenyewe Emiliana na Linus.
 
Back
Top Bottom