Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
1. Ni kesi gani ilifunguliwa Mahakama Kuu Kitengo cha Biashara mwezi Dec 2010 inayohusu Dowans? Mbona kesi hiyo haipo tena?
2. Ni kesi gani imefunguliwa Mahakama Kuu Masjala ya Kawaida (Normal Registry) na ni nani ameifungua kesi hiyo? Ni wakili gani amepeleka hizo Documents? Kama ni Rex Attorney kwa nini wamepeleka na wao si mawakili wa Dowans?
3. Je Rex walihusikaje katika kuhaulisha mkataba kutoka Richmond kwenda Dowans? Na walihusikaje katika kuvunjwa kwa mkataba huo? Na kwa nini wameshauri Dowans walipwe? Walishiriki vipi kwenye kesi ICC?
4. Je kabla ya Rex kuhamia kwenye jengo lao waliwahi kuwa wapangaji kwenye jengo la Rostam? Wanamfahamu vipi Rostam?
5. Kwa nini serikali iko tayari kulipa bila hata kupata baraka za mahakama? Sheria zetu za nchi ziko wazi. Dowans wanajua au wanapaswa kujua kwamba hukumu waliyopata lazima isajiliwe kwenye Mahakama yetu na wanasheria wake waitetetee. Hakuna kuvunja sheria za kimataifa hapo. Ni kuheshimu sheria za nchi kama ambavyo tunatakiwa kuheshimu sheria za kimataifa.
6. Kwa nini serikali inataka kudharau sheria za nchi kwa kusingizia kuheshimu sheria za kimataifa? Suala la Dowans si sheria ya kimataifa, ni makubaliano ya kibiashara kwamba tukigombana tutapeleka ugomvi wetu ICC. Atakayeshinda atafuata sheria kama zilivyo. Sheria ni kwamba hukumu lazima isajiliwe. Tatizo liko wapi kufuata sheria?
Tafadhali Dr. Slaa. Nisaidie kuuliza hayo maswali. Kilio cha watanzania kinaishia hewani. Machozi ya samaki!!!
Wasalaam diwani wako!
2. Ni kesi gani imefunguliwa Mahakama Kuu Masjala ya Kawaida (Normal Registry) na ni nani ameifungua kesi hiyo? Ni wakili gani amepeleka hizo Documents? Kama ni Rex Attorney kwa nini wamepeleka na wao si mawakili wa Dowans?
3. Je Rex walihusikaje katika kuhaulisha mkataba kutoka Richmond kwenda Dowans? Na walihusikaje katika kuvunjwa kwa mkataba huo? Na kwa nini wameshauri Dowans walipwe? Walishiriki vipi kwenye kesi ICC?
4. Je kabla ya Rex kuhamia kwenye jengo lao waliwahi kuwa wapangaji kwenye jengo la Rostam? Wanamfahamu vipi Rostam?
5. Kwa nini serikali iko tayari kulipa bila hata kupata baraka za mahakama? Sheria zetu za nchi ziko wazi. Dowans wanajua au wanapaswa kujua kwamba hukumu waliyopata lazima isajiliwe kwenye Mahakama yetu na wanasheria wake waitetetee. Hakuna kuvunja sheria za kimataifa hapo. Ni kuheshimu sheria za nchi kama ambavyo tunatakiwa kuheshimu sheria za kimataifa.
6. Kwa nini serikali inataka kudharau sheria za nchi kwa kusingizia kuheshimu sheria za kimataifa? Suala la Dowans si sheria ya kimataifa, ni makubaliano ya kibiashara kwamba tukigombana tutapeleka ugomvi wetu ICC. Atakayeshinda atafuata sheria kama zilivyo. Sheria ni kwamba hukumu lazima isajiliwe. Tatizo liko wapi kufuata sheria?
Tafadhali Dr. Slaa. Nisaidie kuuliza hayo maswali. Kilio cha watanzania kinaishia hewani. Machozi ya samaki!!!
Wasalaam diwani wako!