Egnecious
JF-Expert Member
- Jul 8, 2015
- 894
- 994
Baada ya Dr. Slaa kutoa hotuba nzito kuonesha kuwa Edo hafai kuwa Rais wa Tanzania, wanasiasa wa upinzani na vyombo vya habari vinavyoandika kwa mrengo wa siasa za upinzani Tanzania wameibuka na kauli ya kuwataka Watanzania wampuuze Dr. Slaa pamoja na hotuba yake.
Tuhuma za kununuliwa zilipelekwa kwa katibu huyu aliyestaafu siasa hivi karibuni huku wakihoji kapata wapi pesa ya kuvilipia vyombo vya habari na wengine wakatengeneza sauti za uongo kuonesha kuwa baadhi ya viongozi wa chama cha Mapinduzi waliingia serena hotel kabla ya kuanza kwa hotuba yake ingawa uchunguzi wa kina unaonesha kuwa video hiyo ni ya kuzushwa.
Lakini je, katika kipindi hiki cha kumchagua Rais wa kuiongoza nchi yetu ni jambo la busara kuanza kuhoji ni wapi mzungumzaji kapata pesa ya kuwalipa waandishi wa habari badala ya kuuhoji ukweli wa kile alichokisema?
Baadhi ya watu wamefungwa macho na ushabiki wa vyama vyao hadi wakazibwa masikio wasione chochote kinachofanyika dhidi yao na kuzibwa masikio wasiwe tayari kusikia kisemwacho.
Madhara ya haya yote yanatukkumba Watanzania wote nikiwemo mimi na wewe. Tuyatafakari maneno yale yaliyozungumzwa kwa takribani dakika 60 yakifuatiwa na ushahidi mzito juu yake
Kuna utofauti mkubwa sana kati ya mwanasiasa na mwanachi wa kawaida kwakua madhara ya matendo ya wanasiasa hayawadhuru wanasiasa wenyewe, ila huwakumba wenye maisha ya kawaida pamoja na maskini wasio na namna yoyote ya kujikomboa
Tafakari kisha uchukue hatua ya kukataa viongozi walaghai, wasaliti na mafisadi waliokithiri. Chaguo bora ni John Magufuli. Kama hujamuelewa Dr. Slaa sasa hivi basi utamuelewa baada ya uchaguzi mkuu
#HapaKaziTU
Tuhuma za kununuliwa zilipelekwa kwa katibu huyu aliyestaafu siasa hivi karibuni huku wakihoji kapata wapi pesa ya kuvilipia vyombo vya habari na wengine wakatengeneza sauti za uongo kuonesha kuwa baadhi ya viongozi wa chama cha Mapinduzi waliingia serena hotel kabla ya kuanza kwa hotuba yake ingawa uchunguzi wa kina unaonesha kuwa video hiyo ni ya kuzushwa.
Lakini je, katika kipindi hiki cha kumchagua Rais wa kuiongoza nchi yetu ni jambo la busara kuanza kuhoji ni wapi mzungumzaji kapata pesa ya kuwalipa waandishi wa habari badala ya kuuhoji ukweli wa kile alichokisema?
Baadhi ya watu wamefungwa macho na ushabiki wa vyama vyao hadi wakazibwa masikio wasione chochote kinachofanyika dhidi yao na kuzibwa masikio wasiwe tayari kusikia kisemwacho.
Madhara ya haya yote yanatukkumba Watanzania wote nikiwemo mimi na wewe. Tuyatafakari maneno yale yaliyozungumzwa kwa takribani dakika 60 yakifuatiwa na ushahidi mzito juu yake
Kuna utofauti mkubwa sana kati ya mwanasiasa na mwanachi wa kawaida kwakua madhara ya matendo ya wanasiasa hayawadhuru wanasiasa wenyewe, ila huwakumba wenye maisha ya kawaida pamoja na maskini wasio na namna yoyote ya kujikomboa
Tafakari kisha uchukue hatua ya kukataa viongozi walaghai, wasaliti na mafisadi waliokithiri. Chaguo bora ni John Magufuli. Kama hujamuelewa Dr. Slaa sasa hivi basi utamuelewa baada ya uchaguzi mkuu
#HapaKaziTU