Dr. Slaa siyo wa kupuuzwa

Dr. Slaa siyo wa kupuuzwa

Egnecious

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2015
Posts
894
Reaction score
994
Baada ya Dr. Slaa kutoa hotuba nzito kuonesha kuwa Edo hafai kuwa Rais wa Tanzania, wanasiasa wa upinzani na vyombo vya habari vinavyoandika kwa mrengo wa siasa za upinzani Tanzania wameibuka na kauli ya kuwataka Watanzania wampuuze Dr. Slaa pamoja na hotuba yake.

Tuhuma za kununuliwa zilipelekwa kwa katibu huyu aliyestaafu siasa hivi karibuni huku wakihoji kapata wapi pesa ya kuvilipia vyombo vya habari na wengine wakatengeneza sauti za uongo kuonesha kuwa baadhi ya viongozi wa chama cha Mapinduzi waliingia serena hotel kabla ya kuanza kwa hotuba yake ingawa uchunguzi wa kina unaonesha kuwa video hiyo ni ya kuzushwa.

Lakini je, katika kipindi hiki cha kumchagua Rais wa kuiongoza nchi yetu ni jambo la busara kuanza kuhoji ni wapi mzungumzaji kapata pesa ya kuwalipa waandishi wa habari badala ya kuuhoji ukweli wa kile alichokisema?

Baadhi ya watu wamefungwa macho na ushabiki wa vyama vyao hadi wakazibwa masikio wasione chochote kinachofanyika dhidi yao na kuzibwa masikio wasiwe tayari kusikia kisemwacho.

Madhara ya haya yote yanatukkumba Watanzania wote nikiwemo mimi na wewe. Tuyatafakari maneno yale yaliyozungumzwa kwa takribani dakika 60 yakifuatiwa na ushahidi mzito juu yake

Kuna utofauti mkubwa sana kati ya mwanasiasa na mwanachi wa kawaida kwakua madhara ya matendo ya wanasiasa hayawadhuru wanasiasa wenyewe, ila huwakumba wenye maisha ya kawaida pamoja na maskini wasio na namna yoyote ya kujikomboa

Tafakari kisha uchukue hatua ya kukataa viongozi walaghai, wasaliti na mafisadi waliokithiri. Chaguo bora ni John Magufuli. Kama hujamuelewa Dr. Slaa sasa hivi basi utamuelewa baada ya uchaguzi mkuu
#HapaKaziTU
 
Mtakuja na kila njia ila sasa ni dhahiri mmeshajua umma umeichoka ccm uko tayari kwa lolote ili mradi tu ccm ing'oke. Andaeni jeshi la kuua umma ila ccm tumeichoka. Mpeni hata Mbowe hongo aiponde cdm lakini atajikuta alipo Slaa, ccm tumeichoka na mkichakachua tutajuana tabia. Mlidhadhani mlipokuwa mnaleta ushabiki wa kipuuzi bungeni na BMK ingeishia pale?
 
Waandishi wa Tz waliwahi kutukanwa na waandishi wa habari wa Kenya japokuwa waliona kama wameonewa vile, Rais mkapa aliwatukana kwa kuwa majuha pia na wakakasirika sana, lakini ni ukweli amabo unaishi daima, waandishi wa habari wa Tz ni mizigo, wanajua kuandika tu na kupiiga picha, zaidi ya hapo hawana kitu. Ni mabomu na sumu inayoua kuliko ile ya panya. Wanaandika kwenye magazeti eti badala ya kujadiri facts alizoongea mtu wao wako busy wanataka kujua nani kalipia ukumbi, huu ni uandishi mbovu kuliko wakati ule wa Sparta na athens ya akina plato, enzi za ujima. Kwani inajalisha nini mtu akiongea amekaa juu ya mti, ama akiongea anakunywa chain? ama akiongea anakula Karanga? mimi ambaye sikuwepo wakati wa tukio sihitaji kujua aliyekuwa anaongea alivaa nguo gani, alikuja na usafiri gani, ama alitokea kula chakula gani kwasababu watu siku zote tunajadiri facts, tunajadiri mambo yaliyozungumzwa kwa kuyachambua, lakini leo tunaandikiwa eti gharama za mkutano, mara nani kalipia ukumbi, hizi ndo facts?
 
Baada ya Dr. Slaa kutoa hotuba nzito kuonesha kuwa Edo hafai kuwa Rais wa Tanzania, wanasiasa wa upinzani na vyombo vya habari vinavyoandika kwa mrengo wa siasa za upinzani Tanzania wameibuka na kauli ya kuwataka Watanzania wampuuze Dr. Slaa pamoja na hotuba yake.

Tuhuma za kununuliwa zilipelekwa kwa katibu huyu aliyestaafu siasa hivi karibuni huku wakihoji kapata wapi pesa ya kuvilipia vyombo vya habari na wengine wakatengeneza sauti za uongo kuonesha kuwa baadhi ya viongozi wa chama cha Mapinduzi waliingia serena hotel kabla ya kuanza kwa hotuba yake ingawa uchunguzi wa kina unaonesha kuwa video hiyo ni ya kuzushwa.

Lakini je, katika kipindi hiki cha kumchagua Rais wa kuiongoza nchi yetu ni jambo la busara kuanza kuhoji ni wapi mzungumzaji kapata pesa ya kuwalipa waandishi wa habari badala ya kuuhoji ukweli wa kile alichokisema?

Baadhi ya watu wamefungwa macho na ushabiki wa vyama vyao hadi wakazibwa masikio wasione chochote kinachofanyika dhidi yao na kuzibwa masikio wasiwe tayari kusikia kisemwacho.

Madhara ya haya yote yanatukkumba Watanzania wote nikiwemo mimi na wewe. Tuyatafakari maneno yale yaliyozungumzwa kwa takribani dakika 60 yakifuatiwa na ushahidi mzito juu yake

Kuna utofauti mkubwa sana kati ya mwanasiasa na mwanachi wa kawaida kwakua madhara ya matendo ya wanasiasa hayawadhuru wanasiasa wenyewe, ila huwakumba wenye maisha ya kawaida pamoja na maskini wasio na namna yoyote ya kujikomboa

Tafakari kisha uchukue hatua ya kukataa viongozi walaghai, wasaliti na mafisadi waliokithiri. Chaguo bora ni John Magufuli. Kama hujamuelewa Dr. Slaa sasa hivi basi utamuelewa baada ya uchaguzi mkuu
#HapaKaziTU

wengine tulishampuuza siku nyingi na nina imani hata mawe yamempuuza. kama unamwona wa maana chukua peleka nyumbani kwako. yaani mpaka mnalazimisha mnalipa vijana wenu ili waandame ionekane slaa ana watu lakini sio wanachadema? slaa ni mwepesi na mweupe kama karatasi iliyotoka kiwandani
 
Doctor anayeshindia mihogo leo ana fedha za kukodi Serena!? Muamini mwenyewe, shauri yako.
 
Ccm hamuwezi kushinda uchaguzi kwa kutemea propanda na wanasema ukitaka kumuua nyani usimuangalie usoni kwasababu watanzania wanataka mabadiliko hawezi kuanza kusikiliza maneno yenu kwasababu kwa sasa ccm hamuaminiki tena
 
Washenga waliotoka CCM na kuhamia CDM wanakimaliza chama....
 
wenyewe akili tumeluelewa na lowasa hatumpi...tutampa slaa
 
Baada ya Dr. Slaa kutoa hotuba nzito kuonesha kuwa Edo hafai kuwa Rais wa Tanzania, wanasiasa wa upinzani na vyombo vya habari vinavyoandika kwa mrengo wa siasa za upinzani Tanzania wameibuka na kauli ya kuwataka Watanzania wampuuze Dr. Slaa pamoja na hotuba yake.

Tuhuma za kununuliwa zilipelekwa kwa katibu huyu aliyestaafu siasa hivi karibuni huku wakihoji kapata wapi pesa ya kuvilipia vyombo vya habari na wengine wakatengeneza sauti za uongo kuonesha kuwa baadhi ya viongozi wa chama cha Mapinduzi waliingia serena hotel kabla ya kuanza kwa hotuba yake ingawa uchunguzi wa kina unaonesha kuwa video hiyo ni ya kuzushwa.

Lakini je, katika kipindi hiki cha kumchagua Rais wa kuiongoza nchi yetu ni jambo la busara kuanza kuhoji ni wapi mzungumzaji kapata pesa ya kuwalipa waandishi wa habari badala ya kuuhoji ukweli wa kile alichokisema?

Baadhi ya watu wamefungwa macho na ushabiki wa vyama vyao hadi wakazibwa masikio wasione chochote kinachofanyika dhidi yao na kuzibwa masikio wasiwe tayari kusikia kisemwacho.

Madhara ya haya yote yanatukkumba Watanzania wote nikiwemo mimi na wewe. Tuyatafakari maneno yale yaliyozungumzwa kwa takribani dakika 60 yakifuatiwa na ushahidi mzito juu yake

Kuna utofauti mkubwa sana kati ya mwanasiasa na mwanachi wa kawaida kwakua madhara ya matendo ya wanasiasa hayawadhuru wanasiasa wenyewe, ila huwakumba wenye maisha ya kawaida pamoja na maskini wasio na namna yoyote ya kujikomboa

Tafakari kisha uchukue hatua ya kukataa viongozi walaghai, wasaliti na mafisadi waliokithiri. Chaguo bora ni John Magufuli. Kama hujamuelewa Dr. Slaa sasa hivi basi utamuelewa baada ya uchaguzi mkuu
#HapaKaziTU

Kipi kipya Slaa alichozungumza? Ushahidi gani? Kama ushahidi mzito upo nini kinawafnaya ccm wachelewe kwenda mahakamani?
 
Hata mm nasikitika sana, kwanza kwa maswali niloyasikia wakimmuiliza Dr.Slaa unaweza kusikitika sana sana, mpaka muulizwa maswali na yy akachoka kwa maana ya kuona uwezo wao, napata tabu sana kwa wandishi wetu, hata tv zetu bado pia ni mzigo kweli kweli, mfano mdogo tu, ctz tv ya kenya wanafanya kazi hadi mtizamaji unapata raha kwa taarifa zao- mfano swala la Sumaye kuhamia chadema, kwanza alisikika akisema akichaguliwa fisadi atahama chama, baada ya huyo jamaa yake kuhama na yeye pia kamfuata- na hizo clip zipo, Dr.Slaa alichosema miaka 7 iliyopita na bado karudia vilevile, ss unapojaribu kuwakumbusha wananchi miaka iliyopita na kauli za viongozi, unamfungua mwanchi ili aweze kuwaelewa wagombea wetu na jinsi wanavyokuwa vigeugeu.

Sielewi tunakokwenda watz, ukiona hadi wanachakachua hotuba za baba wa taifa na wanahabari wako kimya kabisa na tv zetu wala hazina noma kabisa, nadhani tumefikia hatua mbaya sana, mfano hotuba ya baba wa taifa kwamba wananchi wanataka mabadiliko, wao hawaweki maelezo ya mwanzo kuwa- watanzania wamechoka na rushwa. Maana yake ni kwamba ukiweka hiyo clip jinsi ilivyo maana yake wapo wapenda rushwa tena kubwa sana. Ss hiyo itawafanya wananchi wawashtuke ndo maana wanachakachua.
 
Slaa amekwisha kupuuzwa, tunasonga mbele!!!! Slaa anajifanya eti ndiyo mtakatifu kuliko Watanzania wote, wakati ni fisadi mkubwa wa kupora wake za watu, akarudishe kwanza mke wa mtu ndipo aendelee na longolongo zake. Hatudanganyiki, ni Lowassa tu, ije mvua lije jua.
 
Hakuna cha maana alichokisema dokta mzinzi na muasherati.

Mambo yq richmond tunayajua tokq 2008, hakuna mpya, sisi tulishamsamehe lowassa na tunasonga mbele,watu hutenda dhambi na husamehewa

Tulichoamua ni kumpa urais, mqmbo mengine ni porojo tu hazina msingi,nani asiejua richmond,sio kitu kipya kwetu, ibueni tuhuma mpya sio hiyo iliyochuja.
 
Kama ni kweli niyasomayao humu kwamba Mzee Slaa hajaleta mtikisiko wowote kwa fisadi Lowasa na Genge lake, ni kwa nini sasa hamkai kimya na kumpotezea?

Ni kwa nini siku nzima JF yote imejaa habari kumhusu Mzee Slaa, kumkashifu na kumtukana?
Unawezaje kupoteza muda wako kumkashifu na kumtukana mtu ambaye hakuathiri kwa lolote? Ni kwanini Mbatia alienda kuongea na Wahandishi wa Habari? Ni kwa nini mnahangaika na kusema sijui mmeandika barua kwa Wazungu kumhusu Mzee Slaa na familia yake, sasa yote haya ni ya nini kama mnajua aliyoyasema hayajamuathiri fisadi Lowasa na Genge lake?
 
Lowassa kanunuliwa na ndo maana anapata nafasi ya kuwanunua wengine
 
Kama ni kweli niyasomayao humu kwamba Mzee Slaa hajaleta mtikisiko wowote kwa fisadi Lowasa na Genge lake, ni kwa nini sasa hamkai kimya na kumpotezea?

Ni kwa nini siku nzima JF yote imejaa habari kumhusu Mzee Slaa, kumkashifu na kumtukana?
Unawezaje kupoteza muda wako kumkashifu na kumtukana mtu ambaye hakuathiri kwa lolote? Ni kwanini Mbatia alienda kuongea na Wahandishi wa Habari? Ni kwa nini mnahangaika na kusema sijui mmeandika barua kwa Wazungu kumhusu Mzee Slaa na familia yake, sasa yote haya ni ya nini kama mnajua aliyoyasema hayajamuathiri fisadi Lowasa na Genge lake?
Kama Lowassa hajaleta mtikisiko CCM mbona heading za vyombo vya habari na mikutano yenu ni LOWASSA TU?
 
aliyosema Dr.Slaakuhusu lowasa sio mageni tofauti na viongozi wengine wa chadema ambao walijaribu kupindisha ukweli kuwa lowasa hakuwa fisadi ila mfumo huku wakisahau kuwa mfumo unawekwa na watu na watu ambao wananufaika na mfumo huo kitu ambacho lowasa amekionyesha kuwa hata alipohamia ukawa hawezi kubadilika
 
Back
Top Bottom