Elections 2010 Dr.slaa na chadema twendeni mahakamani ushahidi upo tele!!!!

makoye2009

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
2,638
1,218
Hili swala la CCM,NEC,UWT(Usalama wa Taifa) KUCHAKACHUA matokeo ya kura za Urais na Ubunge liko wazi kabisa na ushahidi upo.

Mifano halisi ni ucheleweshaji wa kutangaza matokeo kwenye maeneo yenye nguvu kubwa ya Upinzani hasa CHADEMA. Hii haikutokea kwa bahati mbaya ni MAKUSUDI. Angali kilichotokea Dar,Arusha,Mwanza,Mbeya,Shinyanga na maneneo mengine mengi.

Majimbo ya Nyamagana,Ilemera,Arusha Mjini,Karatu,Shinyanga Mjini kura zake mpaka jana Usiku NEC walikuwa bado HAWAJAZIJUMLISHWA KWENYE IDADI YA KURA ZA DR.SLAA KWA MAKUSUDI wakti tayari wasimamizi wa majimbo walizitangaza kwa SHINIKIZO ZA WANANCHI. Nec wamefanya kusudi kuchelewesha kujumlisha ili Kiwete aonekana kuwa anaongoza kwa mbali.

HAINGII AKILINI MTU UMPIGIE KURA MBUNGE WA CHADEMA HALAFU KURA YA URAIS UMPE MGOMBEA WA CCM KIWETE. MTU UNACHAGUA SERA ZA CHAMA SIYO SURA YA MTU. MIFANO:

JIMBO: CHAMA:----------------------------UBUNGE:-------------------RAIS:

ARUSHA MJINI CHADEMA................................56,208..........................54,208
CCM...........................................................36,107..........................39,107

MBEYA MJINI CHADEMA.................................46,411........................42,917
CCM...........................................................24,236........................32,249

MWANZA-NYAMAGANA CHADEMA......................38,171.........................30,991
CCM.............................................................27,883........................32,320


MWANZA-ILEMERA CHADEMA............................31,256..........................29,701
CCM..............................................................26,870........................9,143

MASWA MAGH CHADEMA.........................17,456.........................11,742
CCM....................................................12,824.........................17,104

MASWA MASH CHADEMA......................17,075.........................12,203
CCM............................. 17,014.........................21,150


Kali zaidi ni hii ya JIMBO LA Musoma mjini: Kutoka KURA 14,723 za Mbunge wa CCM na kuongezwa kufikia KURA 49,858 za KIKWETE.

MUSOMA MJINI CHADEMA....................21,335........................23,211
CCM.................................................14,723........................49,858???

Hii ni zaidi ya mara 3 ya kura za Mbunge.Haingii akilini mtu amkatae mbunge wa chama halafu ampe Rais wa chama cha mbunge huyu aliyemkataa. Labda kama mtu huyo anachagua SURA na siyo SERA!!!!!!!!!!!!!!


Mpaka sasa ukiingia kwenye WEBSITE YA TUME: http:/www.nec.go.tz Bado KURA HIZO HAZIONEKANI KWENYE MTANDAO. KWANINI HAWATAKI KUZIJUMLISHA? WANOGOPA NINI?

Soma hizi nukuu toka Gazeti la MWANANCHI toleo la leo 5/11/2010:

''..............Nao wasomi wameungana na madai ya Dk Slaa wakisema kuwa uchakachuaji matokeo ya kura nchini umekuwa aibu kwa taifa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam jana, wasomi hao walisema kuna dalili zinazotia shaka kwamba matokeo ya urais yamechakachuliwa kwa kuwa hawaoni sababu kucheleweshwa kutangazwa.
"Tunajua kuwa hata kama CCM ingeshinda, isingeshinda kwa kura nyingi kiasi hicho. Kwa nini tumsifie mtu kuwa ameshinda kwa kishindo na huku amechakachua matokeo?"alisema Dk Fairles Ilomo, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa.
Dk Ilomo alisema haiingii akilini kuelezwa kuwa matokeo yamechelewa kutangazwa kwa sababu ya matumizi ya kompyuta katika hatua ya kuhesabu kwani wakati wa upigaji, wananchi hawakutumia kompyuta.

"Kwanini matokeo yasubiri kompyuta? Hakuna logic (mantiki) kusema kuwa kuingiza data kwenye kompyuta kulisababisha ucheleweshaji maana hata uchaguzi wa Marekani, walitumia kompyuta na matokeo yakawahi kutolewa," alisema Dk Ilomo.
"Ni kweli uchaguzi ulifanyika vizuri na kulikuwa na amani lakini katika hatua ya kuhesabu kura na kutangaza matokeo kulikuwa na uchakachuaji hasa katika maeneo nyeti.
"Rais aapishwe, lakini Dk Slaa ana haki ya kuendelea na malalamiko yake. Kama malalamiko hayo yakionekana yana ukweli, maamuzi mengine yafuate."

..............Mhadhiri mwingine chuoni hapo Harod Tairo alisema amestuka kuona matokeo hayo yanaonyesha kuwa watu wengi wamewapigia kura wabunge wa Chadema lakini si mgombea wake wa urais, yaani Dk Willibrod Slaa
"Mimi naamini kwamba wabunge wengi wa Chadema walichaguliwa kwa juhudi za Dk Slaa. Wananchi hawawezi kuchagua mbunge wa Chadema halafu rais wamchague wa CCM. Mimi naona matokeo hayaakisi halihalisi," alisema Tairo.

Hawa wasomi na Wahadhiri naungana nao kwa 100%.
 
Ulichosema ninakubaliana nacho.

Swali: Twende mahakama ipi? Maana hapa kwetu kila kitu kipo chini ya Mkwere
 
Mpaka sasa hivi nawaza hawa jamaa wanawaona Watanzania ni mbumbubu??

This is ridiculous shame on you NEC
 
Nadhani itakuwa ni kupoteza muda kuanza kufukuza fursa iliyopotea. Nadhani wakati huu ni wakati wa kujipanga kwa ajiri ya kurekebisha kasoro zilizopo katika tume na mfumo mzima wa upatikanaji wa takwimu za NEC kupitia harakati.
Kazi nyingine ambayo inatakiwa kufanywa ni kuimalisha chama kuanzia kwa wananchi na hasa hasa vijijini.

Kama kutakuwa na ulazima wa kwenda mahakamani basi iwe kushinikiza mabadiriko katika mfumo wa uchaguzi, muundo wa tume na mambo mengine yaliyosababisha kura zetu kuibiwa ama watu kupotoshwa kwa propaganda za uwongo.
 
swali la msingi hapa chadema waende mahakama gani coz wote ni wale wale nafikiri issue ya mgombea binafsi mliona kilichotokea hata friends of court nao walichakachuliwa sembuse hili:bowl:
 
Hili swala la CCM,NEC,UWT(Usalama wa Taifa) KUCHAKACHUA matokeo ya kura za Urais na Ubunge liko wazi kabisa na ushahidi upo.

Mifano halisi ni ucheleweshaji wa kutangaza matokeo kwenye maeneo yenye nguvu kubwa ya Upinzani hasa CHADEMA. Hii haikutokea kwa bahati mbaya ni MAKUSUDI. Angali kilichotokea Dar,Arusha,Mwanza,Mbeya,Shinyanga na maneneo mengine mengi.

Majimbo ya Nyamagana,Ilemera,Arusha Mjini,Karatu,Shinyanga Mjini kura zake mpaka jana Usiku NEC walikuwa bado HAWAJAZIJUMLISHWA KWENYE IDADI YA KURA ZA DR.SLAA KWA MAKUSUDI wakti tayari wasimamizi wa majimbo walizitangaza kwa SHINIKIZO ZA WANANCHI. Nec wamefanya kusudi kuchelewesha kujumlisha ili Kiwete aonekana kuwa anaongoza kwa mbali.

HAINGII AKILINI MTU UMPIGIE KURA MBUNGE WA CHADEMA HALAFU KURA YA URAIS UMPE MGOMBEA WA CCM KIWETE. MTU UNACHAGUA SERA ZA CHAMA SIYO SURA YA MTU. MIFANO:

JIMBO: CHAMA:----------------------------UBUNGE:-------------------RAIS:

ARUSHA MJINI CHADEMA................................56,208..........................54,208
CCM...........................................................36,107..........................39,107

MBEYA MJINI CHADEMA.................................46,411........................42,917
CCM...........................................................24,236........................32,249

MWANZA-NYAMAGANA CHADEMA......................38,171.........................30,991
CCM.............................................................27,883........................32,320


MWANZA-ILEMERA CHADEMA............................31,256..........................29,701
CCM..............................................................26,870........................9,143

MASWA MAGH CHADEMA.........................17,456.........................11,742
CCM....................................................12,824.........................17,104

MASWA MASH CHADEMA......................17,075.........................12,203
CCM............................. 17,014.........................21,150


Kali zaidi ni hii ya JIMBO LA Musoma mjini: Kutoka KURA 14,723 za Mbunge wa CCM na kuongezwa kufikia KURA 49,858 za KIKWETE.

MUSOMA MJINI CHADEMA....................21,335........................23,211
CCM.................................................14,723........................49,858???

Hii ni zaidi ya mara 3 ya kura za Mbunge.Haingii akilini mtu amkatae mbunge wa chama halafu ampe Rais wa chama cha mbunge huyu aliyemkataa. Labda kama mtu huyo anachagua SURA na siyo SERA!!!!!!!!!!!!!!


Mpaka sasa ukiingia kwenye WEBSITE YA TUME: http:/www.nec.go.tz Bado KURA HIZO HAZIONEKANI KWENYE MTANDAO. KWANINI HAWATAKI KUZIJUMLISHA? WANOGOPA NINI?

Soma hizi nukuu toka Gazeti la MWANANCHI toleo la leo 5/11/2010:

''..............Nao wasomi wameungana na madai ya Dk Slaa wakisema kuwa uchakachuaji matokeo ya kura nchini umekuwa aibu kwa taifa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam jana, wasomi hao walisema kuna dalili zinazotia shaka kwamba matokeo ya urais yamechakachuliwa kwa kuwa hawaoni sababu kucheleweshwa kutangazwa.
“Tunajua kuwa hata kama CCM ingeshinda, isingeshinda kwa kura nyingi kiasi hicho. Kwa nini tumsifie mtu kuwa ameshinda kwa kishindo na huku amechakachua matokeo?”alisema Dk Fairles Ilomo, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa.
Dk Ilomo alisema haiingii akilini kuelezwa kuwa matokeo yamechelewa kutangazwa kwa sababu ya matumizi ya kompyuta katika hatua ya kuhesabu kwani wakati wa upigaji, wananchi hawakutumia kompyuta.

"Kwanini matokeo yasubiri kompyuta? Hakuna logic (mantiki) kusema kuwa kuingiza data kwenye kompyuta kulisababisha ucheleweshaji maana hata uchaguzi wa Marekani, walitumia kompyuta na matokeo yakawahi kutolewa," alisema Dk Ilomo.
“Ni kweli uchaguzi ulifanyika vizuri na kulikuwa na amani lakini katika hatua ya kuhesabu kura na kutangaza matokeo kulikuwa na uchakachuaji hasa katika maeneo nyeti.
“Rais aapishwe, lakini Dk Slaa ana haki ya kuendelea na malalamiko yake. Kama malalamiko hayo yakionekana yana ukweli, maamuzi mengine yafuate."

..............Mhadhiri mwingine chuoni hapo Harod Tairo alisema amestuka kuona matokeo hayo yanaonyesha kuwa watu wengi wamewapigia kura wabunge wa Chadema lakini si mgombea wake wa urais, yaani Dk Willibrod Slaa
“Mimi naamini kwamba wabunge wengi wa Chadema walichaguliwa kwa juhudi za Dk Slaa. Wananchi hawawezi kuchagua mbunge wa Chadema halafu rais wamchague wa CCM. Mimi naona matokeo hayaakisi halihalisi,” alisema Tairo.

Hawa wasomi na Wahadhiri naungana nao kwa 100%.

Umesahau K.

Mengine uko sahihi kabisa,japo sheria zetu hazitupi mwanya wa kujitetea.Hapo wamechakachua haswa...
 
Hii NEC chini ya serikali na chama tawala ndio matatizo. Kikubwa ni kushinikizwa Tume iwe na wateuliwa kutoka vyama vyote.
 
MUSOMA MJINI CHADEMA....................21,335................. .......23,211
CCM............................................... ..14,723........................49,858???

Jumla ya wapiga kula ilikuwa ngapi?
 
jamani from my understanding, Rais akisha apishwa haiwezekani kumfungulia kesi mahakamani, na pia haiwezekani kufungua kesi kama hauna uhakika na matokeo hadi watakapo mwapisha, na akiapwishwa haiwezekani kutenguliwa.

mimi nadhani tuifuate haki yetu mtaani maana penye sheria hatuwezi kufika, maana ndo hao hao.
 
MBEYA MJINI CHADEMA.................................46,411........................42,917
CCM...........................................................24,236........................32,249

MWANZA-NYAMAGANA CHADEMA......................38,171.........................30,991
CCM.............................................................27,883........................32,320


MWANZA-ILEMERA CHADEMA............................31,256..........................29,701
CCM..............................................................26,870........................9,143

MASWA MAGH CHADEMA.........................17,456.........................11,742
CCM....................................................12,824.........................17,104

MASWA MASH CHADEMA......................17,075.........................12,203
CCM............................. 17,014.........................21,150


Kali zaidi ni hii ya JIMBO LA Musoma mjini: Kutoka KURA 14,723 za Mbunge wa CCM na kuongezwa kufikia KURA 49,858 za KIKWETE.

MUSOMA MJINI CHADEMA....................21,335........................23,211
CCM.................................................14,723........................49,858???

Ukiangalia hesabu ya kura za ubunge na urais hazina uwiano. Inaonekana wapiga kura wengi zaidi walipiga kura za urais kuliko za ubunge. Tume ituambie idadi ya wapiga kura waliojitokeza kupiga kura vs matokeo. Na si blabla tu. Mfano Musoma mjini, kura za DR. Slaa na JK ni 73,069 na za wabunge wa ccm na chadema ni 36,058 hivyo kuna kura 37,011 ambazo ama zilienda kwa wagombea ubunge wengine, au wapiga kura hao waliamua kupiga kura za urais pekee. Bila kujumlisha kura walizopigiwa wagombea urais wengine, kura za ziada pekee zinatosha kubadili matokeo ya kura za ubunge katika jimbo hilo. Kwanini tusiamini kwamba matokeo ya urais ni batili?
 
Mbaya zaidi ni kwamba kura za JK zinaongezeka kwa majimbo ambayo CHADEMA imeongoza tu. Hii trend si sawa logically.
 
mi naona twendeni mahakama ya kimataifa ushahidi si tunao jamani

Mtuflani nakubaliana na wewe kabsaaa.
Hata mimi naona tumtafute Ocampo anayeshughulikia mgogoro wa Uchaguzi wa Kenya 2007.

CHADEMA tuna wanasheria makini sana kama Mabere Marando na Tundu Lisu. Tukiwatumia hawa jamaa kesi yetu itawahenyesha CCM mpaka wajute kwanini walichakachua kura zetu.
 
Kwa kila hali inaonekana uchakachuaji ndo umempa urais,kwa hiyo Dr ndio rais wa kuteuliwa na huyu aliyetangazwa ni rais wa kuchakachuliwa.
 
HILI NI SWALA LA WAZI KUWA KURA ZILIIBWA NA KUWEKWA KAMA WANAVYOTAKA WENYEWE,ILA TATIZO WALILOFANYA NI KUTOKUTUMIA AKILI VIZURI ILI KU-BALANCE MAENEO YOTE,HAPO TU NDIO IMEKULA KWAO,WANGEMPA KIKWETE HATA 48% ISINGEKUWA MBAYA SANA,LAKINI WALICHOTAKA ILIKUWA WALAU REDET/SYNOVATE inashabihana....:nono:
 
Katiba 'yenu' hairuhusu kuhoji matokeo ya urais! Hivyo la msingi ni kuhangaikia mabadiliko ya katiba yatayohakikisha kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi na uchaguzi ulio huru na haki. Kung'ang'ania kubishania matokeo ni kupoteza muda - kwa hali ilivyo katiba inawakingia kifua. Wahenga hawakukosea "maji yakishamwagika hayazoleki".
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom