Katibu Mkuu CHADEMA Dr Willbroad Slaa kesho anatarajiwa kuzindua tawi la Umoja wa Wanafunzi wa CHADEMA - (CHASO) Chuo kikuu Muhimbili.
Uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa Don Bosco Upanga Mashariki kuanzia saa 8 mchana.
Habari kubwa iliyotanda hapa Chuoni na viunga vyake ni kuhusu uzinduzi huo wa kesho ikitarajiwa Idadi kubwa ya wanafunzi kuwahi kutokea kuhudhuria mkutano huo!
Katika uzinduzi Mtendaji huyo Mkuu wa CHADEMA anatarajiwa kuzungumzia mambo mazito yanayolikabili Taifa kwa sasa hasa likiwemo suala la Katiba mpya.
Itakumbukwa ni hapo Jana tu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba Samwel Sitta amejiapisha kuchakachua Kanuni za Bunge Maalum la Katiba ili kukomoa UKAWA na kupitisha Katiba itakayokuwa na Maslahi pekee kwa CCM bila kujali maoni ya wananchi.
Wanafunzi wa hapa Muhimbili wana hamu kubwa kumsikia Dr Slaa atasema nini akiwa kama mmoja wa Viongozi wenye nguvu ndani ya UKAWA.
UPDATES....
Uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa Don Bosco Upanga Mashariki kuanzia saa 8 mchana.
Habari kubwa iliyotanda hapa Chuoni na viunga vyake ni kuhusu uzinduzi huo wa kesho ikitarajiwa Idadi kubwa ya wanafunzi kuwahi kutokea kuhudhuria mkutano huo!
Katika uzinduzi Mtendaji huyo Mkuu wa CHADEMA anatarajiwa kuzungumzia mambo mazito yanayolikabili Taifa kwa sasa hasa likiwemo suala la Katiba mpya.
Itakumbukwa ni hapo Jana tu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba Samwel Sitta amejiapisha kuchakachua Kanuni za Bunge Maalum la Katiba ili kukomoa UKAWA na kupitisha Katiba itakayokuwa na Maslahi pekee kwa CCM bila kujali maoni ya wananchi.
Wanafunzi wa hapa Muhimbili wana hamu kubwa kumsikia Dr Slaa atasema nini akiwa kama mmoja wa Viongozi wenye nguvu ndani ya UKAWA.
UPDATES....
Dr Slaa ameingia ndani yaukumbi madr wamejipanga vema nitawapa kinachoendelea
Simu inaishiwa Umeme ila Dr kaifananisha CCM na Adolf H. Kuwa alikifa kutokana na ukatiri wake hata kaburi lake halijulikani lilipo ndivyo itakavyokuwa kwa CCM kutokana na ukatiri wake kuwanyanyasa wanafunzi kuwafukuza vyuo kufunga vyuo bila sababu hii nikuuwa kizazi cha wasomi matokeo yake CCM itakufa kama gaidi Hitla na kaburi lake kutokuonekana
Anazungumzia bunge LA katiba kifupi msimamo niule ule kutokurudi bungeni kama hawatakubali kujadili maoni ya wananchi
Maoni ya wananchi kwanza maslai yawatu binafsi baadaye