Dr Slaa kuunguruma leo Dar!

Dr Slaa kuunguruma leo Dar!

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Katibu Mkuu CHADEMA Dr Willbroad Slaa kesho anatarajiwa kuzindua tawi la Umoja wa Wanafunzi wa CHADEMA - (CHASO) Chuo kikuu Muhimbili.

Uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa Don Bosco Upanga Mashariki kuanzia saa 8 mchana.

Habari kubwa iliyotanda hapa Chuoni na viunga vyake ni kuhusu uzinduzi huo wa kesho ikitarajiwa Idadi kubwa ya wanafunzi kuwahi kutokea kuhudhuria mkutano huo!

Katika uzinduzi Mtendaji huyo Mkuu wa CHADEMA anatarajiwa kuzungumzia mambo mazito yanayolikabili Taifa kwa sasa hasa likiwemo suala la Katiba mpya.

Itakumbukwa ni hapo Jana tu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba Samwel Sitta amejiapisha kuchakachua Kanuni za Bunge Maalum la Katiba ili kukomoa UKAWA na kupitisha Katiba itakayokuwa na Maslahi pekee kwa CCM bila kujali maoni ya wananchi.

Wanafunzi wa hapa Muhimbili wana hamu kubwa kumsikia Dr Slaa atasema nini akiwa kama mmoja wa Viongozi wenye nguvu ndani ya UKAWA.

UPDATES....

Dr Slaa ameingia ndani yaukumbi madr wamejipanga vema nitawapa kinachoendelea


Simu inaishiwa Umeme ila Dr kaifananisha CCM na Adolf H. Kuwa alikifa kutokana na ukatiri wake hata kaburi lake halijulikani lilipo ndivyo itakavyokuwa kwa CCM kutokana na ukatiri wake kuwanyanyasa wanafunzi kuwafukuza vyuo kufunga vyuo bila sababu hii nikuuwa kizazi cha wasomi matokeo yake CCM itakufa kama gaidi Hitla na kaburi lake kutokuonekana

Anazungumzia bunge LA katiba kifupi msimamo niule ule kutokurudi bungeni kama hawatakubali kujadili maoni ya wananchi

Maoni ya wananchi kwanza maslai yawatu binafsi baadaye
 
Dr makini anaeitendea haki taaluma yake na kipaji chake alichopew na mwenyezi mungu bila kuwalaghai na kuwanyanyasa watz kama wafanyavyo wengine waliolaaniwa kama vile kina dr. Chimbi na nhemba
 
Hivi Dr Slaa hadhi yake ni kuzindua matawi ya chadema? Hii ni aibu kubwa na ni fedheha kwake
 
Katibu Mkuu CHADEMA Dr Willbroad Slaa kesho anatarajiwa kuzindua tawi la Umoja wa Wanafunzi wa CHADEMA - (CHASO) Chuo kikuu Muhimbili.

Uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa Don Bosco Upanga Mashariki kuanzia saa 8 mchana.

Habari kubwa iliyotanda hapa Chuoni na viunga vyake ni kuhusu uzinduzi huo wa kesho ikitarajiwa Idadi kubwa ya wanafunzi kuwahi kutokea kuhudhuria mkutano huo!

Katika uzinduzi Mtendaji huyo Mkuu wa CHADEMA anatarajiwa kuzungumzia mambo mazito yanayolikabili Taifa kwa sasa hasa likiwemo suala la Katiba mpya.

Itakumbukwa ni hapo Jana tu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba Samwel Sitta amejiapisha kuchakachua Kanuni za Bunge Maalum la Katiba ili kukomoa UKAWA na kupitisha Katiba itakayokuwa na Maslahi pekee kwa CCM bila kujali maoni ya wananchi.

Wanafunzi wa hapa Muhimbili wana hamu kubwa kumsikia Dr Slaa atasema nini akiwa kama mmoja wa Viongozi wenye nguvu ndani ya UKAWA.

Sita akichakachua kanuni ajue Urais mwakani ni kwa heri. Hajui watu wengi ndani ya CCM tunataka Tanganyika yetu ajaribu aone.
 
Rais wa mioyoni mwa watanzania
hakika Mungu amjalie maisha marefu.
Ona kwa sala zetu,anazidi kuwa na akili km kijana wa miaka 45,hakika ikulu inakusubiria
naamini una maono ya Mungu kuitoa Tz chini ya mikono ya ibilis/ccm
 
Back
Top Bottom