Kiongozi wa Upinzani nchini Dr Wilbroad P.Slaa kesho anatarajiwa kuunguruma mkoani Shinyanga.Kiongozi huyo ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CHADEMA atatikisa katika mkutano wa kumnadi mgombea Udiwani wa CDM katika kata ya Mwawaza.
Habari za awali zinasema kuwa baba mzazi wa mgombea udiwani wa CDM anatarajiwa pia kupanda jukwaani kuelezea jinsi alivyohongwa ili amsingizie mwanae ni mwizi katika moja ya mikutano ya CCM.
Kuna shamrashamra kubwa hapa Shinyanga kuashiria ujio wa kiongozi huyo mashuhuri nchini.Mpaka sasa tathmini za awali zinaonyesha CDM ina uwezo wa kushinda kata hiyo kwa idadi kubwa ya kura.
Habari za awali zinasema kuwa baba mzazi wa mgombea udiwani wa CDM anatarajiwa pia kupanda jukwaani kuelezea jinsi alivyohongwa ili amsingizie mwanae ni mwizi katika moja ya mikutano ya CCM.
Kuna shamrashamra kubwa hapa Shinyanga kuashiria ujio wa kiongozi huyo mashuhuri nchini.Mpaka sasa tathmini za awali zinaonyesha CDM ina uwezo wa kushinda kata hiyo kwa idadi kubwa ya kura.