Kiongozi wa upinzani nchini ambaye pia ni Katibu mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa leo anatarajiwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Igunga kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano waliyokionyesha chama chake mpaka pale mahakama ilipotengua ubunge wa CCM ambao haukuwa halali.
Dr Slaa ambaye anaongoza operesheni M4C mkoani Morogoro imemlazimu kuwaacha makamanda wengine huku yeye na baadhi ya maafisa wakielekea Igunga.Kiongozi huyo amefuatana na Mkiti wa chama mkoa wa Tabora Kansa Mbarouk.
Mara baada ya kuunguruma Igunga leo ataondoka kurejea Morogoro ambapo Jumatatu atakuwa mgeni rasmi katika hitimisho la M4C mkoani Morogoro kwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Morogoro,mkutano unaotarajiwa kuutikisa mkoa mzima na kanda ya kati kwa ujumla kutokana na shauku kubwa wananchi waliyo nayo.
Source:Tanzania Daima.